Mbuna
JF-Expert Member
- Jul 3, 2013
- 269
- 71
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 23 Nina mke mmoja ambaye ni mjamzito, Tatizo langu maisha yangu yamekuwa na mikosi au kivingine mazingaumbwe, kila napofanikiwa kidogo napata matatizo makubwa sana kama kutokewa na nguvu za giza ndotoni au hata nikiwa kwenye pilikapilika.
Juzi kati Rafiki yangu tuliyekuwa tunafanya wote biashara kanitoa ofisini na kuniambia fanya mambo yako nami nifanye yangu baada ya biashara kukua sana ila pesa aliyonipa ni Mungu tu ndo anajua, Kanidhulumu na siwezi kumshtaki kwani hatujaandikiana.
Naombeni ushauri wenu kwa yoyote atakayekuwa na wazo la kunisaidia kwani sasa hivi sina chochote na huku mke wangu akikaribia kujifungua. Nimekata tamaa sijui nifanye nini?
Ila baada ya kutembelea hili jukwaa nikahamasika na ushauri unaotolewa, Nikaona kuliko kukaa kimya bora niombe msaada wa kimawazo kwenu.
Asanteni sana kwa msaada wa kimawazo mtakaonipa.
Juzi kati Rafiki yangu tuliyekuwa tunafanya wote biashara kanitoa ofisini na kuniambia fanya mambo yako nami nifanye yangu baada ya biashara kukua sana ila pesa aliyonipa ni Mungu tu ndo anajua, Kanidhulumu na siwezi kumshtaki kwani hatujaandikiana.
Naombeni ushauri wenu kwa yoyote atakayekuwa na wazo la kunisaidia kwani sasa hivi sina chochote na huku mke wangu akikaribia kujifungua. Nimekata tamaa sijui nifanye nini?
Ila baada ya kutembelea hili jukwaa nikahamasika na ushauri unaotolewa, Nikaona kuliko kukaa kimya bora niombe msaada wa kimawazo kwenu.
Asanteni sana kwa msaada wa kimawazo mtakaonipa.