Msaada, kuumwa kichwa (tatizo sugu)

Evelyn Salt

JF-Expert Member
Jan 5, 2012
62,196
106,687
Good morning jf....

Mi nasumbuliwa sana na kichwa, ni muda mrefu sasa kinaniuma, yani siku ninazo kaa bila kuumwa zinahesabika, hospital nishaenda nikipima sina shida yoyote, pain killers nishakunywa sana naona nmechoka sahivi kikiuma nalala tu.

Kuna siku naamka usingizini kichwa kinaniuma, nikikaa sehemu yenye hewa ndogo naumwa kichwa,nikihisi njaa kinauma, nikitembea juani naumwa, naweza kuwa na shida gani? Tiba yake ni nini?
 
Swali, je kinaume sehemu gani.
Jaribu hivi kama hujafanya. 1. Kapime macho 2. Jitahidi kunywa maji ya kutosha sio chini ya lita tatu kwa siku
 
Pima macho uvae miwani kitapona
Mwaka 2007 nilipima macho, nikavaa miwani mwaka mmoja naona kikapona kabisa, kimekuja kuibuka tena nikarudi kupima macho nikaambiwa sina tatizo.... Labda niende tena
Ahsante
 
Swali, je kinaume sehemu gani.
Jaribu hivi kama hujafanya. 1. Kapime macho 2. Jitahidi kunywa maji ya kutosha sio chini ya lita tatu kwa siku
Kinauma hapa mbele kwenye forehead...
Ahsante, mmh hizo lita tatu kuzimaliza siwezi nisiseme uongo
 
Mwaka 2007 nilipima macho, nikavaa miwani mwaka mmoja naona kikapona kabisa, kimekuja kuibuka tena nikarudi kupima macho nikaambiwa sina tatizo.... Labda niende tena
Ahsante
Nenda tena....ukiweza kama you dar nenda pale shoperzplazza kuna clinic ya macho ya wahindi fulan ni wazuri sana kwa matibabu na vipimo.
 
Mwaka 2007 nilipima macho, nikavaa miwani mwaka mmoja naona kikapona kabisa, kimekuja kuibuka tena nikarudi kupima macho nikaambiwa sina tatizo.... Labda niende tena
Ahsante
Ushasikia kitu inaitwa presha ya macho, sijasema kapime miwani, nimesema kapime macho. Watu wengi wanafikiri kupima macho ni miwani tu. tafuta wataalamu wanao juwa kazi kama alivyo sema bwana Who Cares? . Kuhusu swala la maji kama unataka kupona you have to drink, no more options.
 
Ushasikia kitu inaitwa presha ya macho, sijasema kapime miwani, nimesema kapime macho. Watu wengi wanafikiri kupima macho ni miwani tu. tafuta wataalamu wanao juwa kazi kama alivyo sema bwana Who Cares? . Kuhusu swala la maji kama unataka kupona you have to drink, no more options.
Ahsante, naomba unidokeze hiyo presha ya macho ni nini? Inakuaje?
 
Kama huko dar ne.da ccbrt au zahanati moja pale shoppers plaza ground floor.nahisi mishioa ya retina imelegea maumivu yake usipime
Hapo kwa hao wadosi wa shoperz vision plus ni balaaa...mie wife tulihangaika mpaka muhimbili piga mi ct scan na vurugu zoteee...macho alipimaga kwa wale wamarekani wa eye internationals clinique hawakuona kitu....kuja kwa mdoc fastaaa kapona mpaka Leo haamini coz tulishakata tamaa kabisaaa
 
Hapo kwa hao wadosi wa shoperz vision plus ni balaaa...mie wife tulihangaika mpaka muhimbili piga mi ct scan na vurugu zoteee...macho alipimaga kwa wale wamarekani wa eye internationals clinique hawakuona kitu....kuja kwa mdoc fastaaa kapona mpaka Leo haamini coz tulishakata tamaa kabisaaa
Alikua na shida gani? If you don't mind, alipewa dawa?
 
Mwanga wa simu unakudhuru maaana kutwa kucha unakesha kutafuta umbea Jamie forum. ...
 
Good morning jf....

Mi nasumbuliwa sana na kichwa, ni muda mrefu sasa kinaniuma, yani siku ninazo kaa bila kuumwa zinahesabika, hospital nishaenda nikipima sina shida yoyote, pain killers nishakunywa sana naona nmechoka sahivi kikiuma nalala tu.

Kuna siku naamka usingizini kichwa kinaniuma, nikikaa sehemu yenye hewa ndogo naumwa kichwa,nikihisi njaa kinauma, nikitembea juani naumwa, naweza kuwa na shida gani? Tiba yake ni nini?
Kwa uashauri tu ni bora ungeenda hospitali kubwa kufanya screening ya mwili wote kwa sababu kwenye maumivu kuna kitu kinaitwa referred pain yan unaweza kuwa unaskia maumivu begani kumbe ugonjwa upo tumboni hio inatokea kama structures zina embryonic origin moja.......sasa kwa case yako inawezekana tatizo sio macho ila ni kitu kingine tofauti au unaweza kukuta macho ni secondary problem kwahio ukitibu macho kichwa kinaweza kuacha kuuma lakin tatizo unakua hujalimaliza...
 
Good morning jf....

Mi nasumbuliwa sana na kichwa, ni muda mrefu sasa kinaniuma, yani siku ninazo kaa bila kuumwa zinahesabika, hospital nishaenda nikipima sina shida yoyote, pain killers nishakunywa sana naona nmechoka sahivi kikiuma nalala tu.

Kuna siku naamka usingizini kichwa kinaniuma, nikikaa sehemu yenye hewa ndogo naumwa kichwa,nikihisi njaa kinauma, nikitembea juani naumwa, naweza kuwa na shida gani? Tiba yake ni nini?
Pia jitahidi kunywa maji mengi kwa siku
 
Ngoja nimshauri ndugu yangu pia ana tatizo kama lako...pole sana eve
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom