Msaada kutokana na mateso

manka1

Member
Nov 4, 2014
11
23
Habari wana JF,

Mimi ni mwanamke mwenye ulemavu na nina umri wa miaka 45 sasa, nimeolewa nina watoto wawili. Nina miaka 15 sasa tangu niingie kwenye ndoa naona kila siku inavyosonga magumu ya maisha yananizidia.

Mume aliyenioa yeye huwa hayuko tayari kunisaidia shughuli yoyote iwe ya nyumbani au ya kijamii kama kwenda kwenye misiba au shughuli yeyote inayonihusu mimi

Mume huyu ana kazi ya kuajiriwa na mm pia nimeajiriwa siku yote yy husema kazi za nyumbani ni za wanawake naweka mtumishi wa kunisaidia lkn yeye hukataa kumlpa. Pindi akiwa hayupo inaniwia vigumu mno kwani kazi zote inabidi nifanye mimi na nina mguu mmoja mwingine umepooza.

Nimekuja kwenu kuomba msaada wa mawayo kwani hapa nilipo tuna kibanda ambacho nimekijenga mm ika kiwanja kinasoma majina mawili kwa vile niliona ni heshima kuandika jina langu na la mume wangu kwenye hati niliyoitafuta mwenyewe.

Natamani kwa mateso ninayopata niondoke tu nimuachie kila kitu ila nina madeni mengi niliyokopa kujenga na kusomesha watoto ambao hadi ss mmoja yuko sekondari na wa pili msingi.

Nikimtaka atoe hela kwa chochote madai yake hana hela ana madeni mengi ambayo ati amekopa kuamzisha miradi ambayo mimi siijui.Mimi nimesoma nina shahada ya ualimu ktk sayansi pia nina shahada ya uzamili ktk mambo ya ustawi wa jamii.

Natamani nipate kazi mahali fulani mbali nhame na watoto tumwache kwani wanangu wanaishi kwa mkazo rana wakimuomba hela ya matumizi yeyote anawatukana nikimwambia mm ananitukna, anarudi usiku anakula, kuoga na kulala hata kama hela hajatoa kwa madai kuwa ni nyumbani kwake.

Kama kuna yeyote anayeweza kunipa mchango wa mawazo. Nimeandika sasa kwani nina muda sina binti wa kazi narudi kazini nifanye kazi za nyumbani mguu unaniuma na mwenzangu halioni hilo wala hana msaada wowote kwangu.
 
World has no Mercy!

Pole sana Mama, Mungu akusaidie na akufanyie wepesi kwa masahibu hayo yote.
Huyo mumeo ngoja tumuweke kwenye Maombi, kwa jina la Yesu natumaini atarudi kwenye mstari tu.
 
Pole sana,huyo mume hana utu.

Kama unaweza kumudu kumlipa dada wa kazi mtafute akusaidie umlipe ww wala yy usimwambie kuepusha ugomvi. Akiongea maneno yake yapotezee maana unayeteseka ni wewe na watoto

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huku tunasema hiyo stori ya upande mmoja. Nayeye angekuja kusema ya upande wake huenda tungechambua. Mfano mimi niko kwenye kipindi kigumu sana kulingana na kazi yangu. Ila kwa kuwa wife alishazoea kupokea vitu toka kwangu na sasa havipati kama miezi miwili imekuwa kama nimemtelekeza. Maana ndo sms zake kila siku japo anakazi yake na hatuna hata mtoto. Yaani kuna kipindi nilitamani niuze hata simu ili nimtumie hela anayoitaka nione atamwandikia nani hizo sms. Ninadakika zaidi ya 350 za kupiga sim wiki nzima ila inaisha keshokutwa bila kumpigia na sina mpango bora zi expire tu. Niko umbali wa kilometa 8 kutoka nyumbani ila sitamani hata kupakanyaga toka tarehe 21. Inamaana sikukuu zote nazilia hapa uzuri tumetenganishwa na maji. Kuna kipindi nilishajifunza kutoamini malalamiko ya mwanamke. Na nishagundua mwanamke huwa anataka hata mumewe atembee uchi ilimladi tu anapewa kila anachokitaka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza shkamoo dada, pili pole kwa masahibu yanayokupata nafikiri labda swala hili ungelipeleka ustawi wa jamii wangeweza kukusaidia zaidi kimawazo na kisheria kulingana na uzoefu wao...
Nadhani hii itasaidia kwa sababu watawaita wote na kuwasikiliza wote na watajua tatizo liko wapi kama ni ushauri watawapa kama ni ni kutengana haya pia hutapoteza haki zako. Ni hayo tu
 
Pole sana

Ila wanawake mmezidi kulalamika mambo ambayo hayana msingi, sasa hapo ueleweki unataka nini?

Kuanza kusema wewe ni mlemavu sio kigezo na sio sahihi, na ndio maana umepata madegree yote hayo

Tatizo lako wewe ndio ulilolitengeneza mwanzoni kwa kujipa majukumu ambayo hayakuwa yako sasa yamekushinda ndio unaanza kulahumu
Mume wako anaonyesha tabia za kiume na kibaba kukukabili wewe uliyeanza kufanya mambo yako kibinafsi (uo ndio ukweli)

Solution;- Kama mpo kwenye ndoa halali washirikisheni watu wazima mnaowaheshimu kila mtu afunguke yake

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom