Msaada: Kuku wangu yupo hoi

thomas_360

JF-Expert Member
Oct 11, 2015
1,459
1,428
Mwenye kujua huu ugonjwa naomba msaada nimpatie tiba kuku wangu
IMG-20210203-WA0002.jpg
IMG-20210203-WA0000.jpg
IMG-20210203-WA0001.jpg
 
Iko kama infectious corayser. Ni aina ya mafua makali yanashambulia mfumo wa upumuaji, koo, na macho. Mpe chakula kizuri na vitamin. Kama wako wengi tafuta dawa
 
Iko kama infectious corayser. Ni aina ya mafua makali yanashambulia mfumo wa upumuaji, koo, na macho. Mpe chakula kizuri na vitamin. Kama wako wengi tafuta dawa
Yupo pekee yake...ingawa mdondo umewashambulia sana kuku wangu ndo napambana na madawa na kuwachinja wale wanaonesha dalili
 
Yupo pekee yake...ingawa mdondo umewashambulia sana kuku wangu ndo napambana na madawa na kuwachinja wale wanaonesha dalili
Siku nyingine bandua hiyo ngozi iliyo kauka hapo paka mafuta ya mgando,hiyo inaweza kuwa ni fowlpox au infectious coryza tumia broad spectrum antibiotics!au muone mtaalamu wa mifugo aliye karibu yako
 
Mpake mafuta ya alizeti ( au mafuta yoyote ya kula) eneo la kidonda na sehemu yote kichwani.Lakini mpake pia Antibiotics ya unga na unaweza kumpa Antibiotics ya kunywa. Ukifanya vyote kwa pamoja huwa inasaidia.
 
Nashukuruni kwa mawazo yenu hali halisi ni kwamba nilizembea kuwapa chanjo ya mdondo hivyo huu ugonjwa from no where umeibuka na kuku wangu huwa hawatoka nje ya fensi kukutana na mifugo mengine na nimekaa miaka mitatu sijashuhudia hii hali nimeshapoteza kuku kama 15 hivi....waswahili wanasema kuteleza sio kuanguka cha msingi nikuinuka na kuendelea na mwendo kwa tahadhari zaidi...
 
Huo ugonjwa hapo juu ni ndui hukumchanja huyo kuku chanjo ya ndui
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom