Msaada Kuhusu pete ya uchumba.

Msaada Kuhusu pete ya uchumba.

Yes zinafanyika. Kilakitu kinafanyika kama harusi. Usichelewe mkuu, ni jambo jema mbele za Mungu na wanadamu kuishi katika ndoa takatifu. Cha msingi waambie wazee wako mpeleke mahari kwao binti. Hata kwao binti watafurahi na kujisikia vizuri kua unaenda rasmi na kwa heshima ukienda na wazee wako
Nashukuru mkuu[emoji120]
 
lengo la harusi ni nini wakati nyie ni wanandoa na mna mtoto tayari
Sasa mkuu mtu akishapata Mtoto haruhusiwi kufunha ndoa???[emoji15][emoji15][emoji15][emoji15] Kwani hizo si sherehee tu au za kuhidhinishaa.
 
kama ulivyoshauriwa na mchangiaji mmoja kuwa kama hayo mambo ambayo yapo ya msingi kabisa (too basic need) na hata kijana mdogo tu wa form two anaweza kukuelezea kutokana na taratibu za koo zake wewe unaanzisha jukwaa ni bora ukasubiria hata mwaka mmoja kwanza kabla ya kufanya maamuzi ya kubariki au kufunga ndoa.
Pia kuhusu mtoto pia umeshajiridhisha kuwa ni wako??? Jiridhishe kwanza ili usije kuleta mada nyingine siku za usoni
Mtoto ni wangu mkuu... tunafanana na wife wangu hana mambo mengi kabisaa..
 
Unaishi na huyo mama mtoto au mlipeana tuu ujauzito? maana kuna tofauti hapo. Kama utafunga ndoa na mama mtoto hiyo itaitwa kubariki ndoa na kama utafunga ndoa na mwanamke mwingine hiyo ni mnafunga ndoa harusi fresh.
Nilizaa nae ila sikuishi nae nabado tupo pa1
 
Nadhani hii inafall katika category ya kubariki ndoa, process ni zilezile za kuanza na mahari
Kwahiyo naweza kutoa mahari nakumvisha Pete yauchumba, je nilazima nimvishe mbele yawazazi wake nandugu zake?
 
Hapana, hua naona marafiki na ndugu wanaovalishana siku ya mahari na wengine wanavalishana popote na kwa walokole wanavalishana kanisani mbele ya kanisa zima. Hapo utachagua wewe ila kusave cost bora umvalishe siku ya mahari. Ukimvalisha sehemu nyingine kama utahitaji kuwaalika marafiki na ndugu si itakucost misosi na vinywaji. So mi naonaga ni heri kumvalisha siku ya mahari au kanisani
Aha Sawa mkuu naona siku ya mahari ndio imekaa poa kwaamaana hiyo itakuwa mbele yawazazi wake ndugu zake
 
Yaan bora utengwe na uongozwe sala ya toba tena, bila kufanya hivyo hiyo roho itakurudia tena, mtakuja kuzini tena na hiyo roho itakusumbua katika ndoa yako. Dhambi ni lazima itubiwe, fanya kumuona mchungaji tena mwambie akutenge
Doh!! Mkuu mbona hivyo tena, yaani nikaombe kutengwa ni sawa na jambazi kaingia kwako anataka kukuua lakini akakuacha halafu wewe unamfuata na kumwambia akuue tu.

Mkuu nishatubu hiyo dhambi na ninauhakika mwenyezi Mungu kanisamehe so haina haja tena kuomba kutengwa.

Nachotaka kujua tu labda mkuu ni kwamba si naruhusiwa kumuoa mzinifu mwenzangu na tukapata baraka za kanisa ama vipi?
 
Unasali kanisa gani? kwa sisi walokole hatunaga mambo ya kubariki ndoa yaan kama mmeshaishi au kuzini au kuzaa. Kama sio mpentekoste kuna kitu kinaitwa kubariki ndoa. Inakubaliwa. Cha kwanza nenda kwao binti ukatoe mahali then unamvika engagement siku ya mahali ( hii hata kama mmeshazaa), then ukimaliza mambo ya mahali nenda kanisa unalosali kwaajili ya process za kubariki ndoa.
Note: Anza kwenda kwao kwaajili ya kutoa mahali na kupewa fine za kumzalisha binti wa watu

MAHARI sio MAHALI
 
Back
Top Bottom