Msaada kuhusu Kununua Trekta

Msaada kuhusu Kununua Trekta

Shakir

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2012
Posts
1,692
Reaction score
2,098
Wadau,

Nataka kununua Trekta either kwa kuagiza Nje, au kununulia hapa hapa bongo, kuna mwenye kujua taratibu za importation?
Ni kweli Niki-import hakuna kodi bandarini (exempted) ??
Ni kodi zipi zipo exempted?
Na ni aina gani nzuri ya matrekta inayofaa?

Na kama nikiamua kununulia hapa bongo, wapi nitalipata kwa unafuu?
Kuna jamaa yangu kaniambia kua matrekta ya KILIMO KWANZA yaliyopo pale Mwenge Jeshini mengi ni feki.
 
Mkuu,
Uki-import itakugharimu zaidi ni heri ununuwe hapa hapa tz, ni kweli vifaa hivyo vimeondolewa kodi lakini urasimu na usumbufu bado haujaondolewa, unaweza kuagiza trekra toka nje leo na ukaipata mwakani wakati kuna maduka mengi wanauza hapa hapa.

Matrekta mi ninayoyakubali zaidi ni ya aina ya FIAT na NEWHOLLAND, mara zote bei nafuu kwa tz ni DSM tu. Ukiweza njoo PM nitakupa maelezo zaidi.
 
Jaribubkuwasiliana na epza uone kama unawezakunufaika na lolote. Hata kama watakuzungusha miezi na ikaweza kuokoa milioni kadhaa sioni tatizo. Google namba yao kwa website.
 
John Deer ni matrekta mazuri ,Morroco Dar es salaam,mtaa wa ursino na bei ni kulingana horse power ya tractor utakalo.Kwa mawasiliano na aina za hayo matrekta google john deer Tanzania
 
Jaribubkuwasiliana na epza uone kama unawezakunufaika na lolote. Hata kama watakuzungusha miezi na ikaweza kuokoa milioni kadhaa sioni tatizo. Google namba yao kwa website.
Poa best, ngoja nijaribu, yaani nina Mzuka sana na Tractor this time.
 
John Deer ni matrekta mazuri ,Morroco Dar es salaam,mtaa wa ursino na bei ni kulingana horse power ya tractor utakalo.Kwa mawasiliano na aina za hayo matrekta google john deer Tanzania
Poa,
Nikishindwa ku-import nitawaona hao, hopping hawana bei za kutisha!!
 
Poa,
Nikishindwa ku-import nitawaona hao, hopping hawana bei za kutisha!!
bei ni za kawaida,matractor wanauza mapaya kabisa na wanazo spea parts za kutosha,mafundi wao ambao ni john deer certified.kabla ya kuamua kuagiza nje waone hawa sababu kuagiza yaweza kuwa gharama zaidi
 
Mkuu Shakir umetoa maelezo mafupi sana kuhusu Ombi lako la msaada wa kununua trekta....labda ningekuuliza maswali kadhaa ili twende sawa...
1: Unataka trekta ya HP ngapi? Au ukubwa gani?
2: Unaenda kulimia wapi? Au unabebea makontena? Udongo wa sehemu huwa unadetermine HP ngapi itakuwa suitable..upatikanaji wa vifaa sehemu husika,mafundi n.k n.k
3: bajeti yako yk inarange bei gani? Hii itadetermine aina ya trekta inayakufaa coz aina tofauti zina bei tofauti...
Mwisho; nakushauri ucheki na trekta za swaraj nazo ni mkataba.
 
Wadau humu ndani habari zenu, hili suala limenigusa nahitaji kwa ajili ya kusombea mbao msituni huku njombe kwetu. majibu ya SHAKIR yatanipa mwanga. kabajeti kangu mil 5 tu !
 
Wadau,

Nataka kununua Trekta either kwa kuagiza Nje, au kununulia hapa hapa bongo, kuna mwenye kujua taratibu za importation?
Ni kweli Niki-import hakuna kodi bandarini (exempted) ??
Ni kodi zipi zipo exempted?
Na ni aina gani nzuri ya matrekta inayofaa?

Na kama nikiamua kununulia hapa bongo, wapi nitalipata kwa unafuu?
Kuna jamaa yangu kaniambia kua matrekta ya KILIMO KWANZA yaliyopo pale Mwenge Jeshini mengi ni feki.
massay 265 au 285. Ford au john deer
 
Wadau humu ndani habari zenu, hili suala limenigusa nahitaji kwa ajili ya kusombea mbao msituni huku njombe kwetu. majibu ya SHAKIR yatanipa mwanga. kabajeti kangu mil 5 tu !

makasi be! mkuu hiyo hela ni ya kununulia power tiler,tena haitoshi. trekta andaa kuanzi mil 25 to 45 sana sana 30-45m ndio utapata trekta angalau la maana
 
Mkuu kwa milioni 5 huwezi kupata trekta popote pale inayoeleweka..sema kuna wakulima huwa wanataka kubadilisha trekta na kuchukua mpya huwa wanayauza ya zamani.Unaweza kubahatisha huko?
 
Hayo ya kilimo kwanza Farm track usilogwe kuchukua, ni vimeo af spare parts zake hazipatikani. Jaribu na matrekta ya Swaraj ni mazuri sana. Kwa bajeti yako hiyo ya 5Ml utaishia kununua 3 disc plough hata used hauwezi kupata kwa pesa hiyo.
 
mkuu Shakiri Leta mrejesho wa mahali ulipofikia watu wengi wanasubiri mrejesho Nao wajue pa kuanzia..je umewasaliana na Epza? wamekupa jibu gani? mkuu lyokopokomayoko inaonekana kuna mengi unayafahamu kuhusu tractors uweza ukayamwaga humu jukwaani kwa faida ya wengi? .na kama kuna mawakala wa Matrekta humu wajitokeze watupe maelekezo na bei zao watu tujue pa kuanzia
 
Mkuu kwa milioni 5 huwezi kupata trekta popote pale inayoeleweka..sema kuna wakulima huwa wanataka kubadilisha trekta na kuchukua mpya huwa wanayauza ya zamani.Unaweza kubahatisha huko?

Mkuu una data recently za bei ya Swaraji FE 855 na FE 744 mpya? Hizi trekta za swaraj ni ngumu sana na ni mkataba...binafsi nazikubali sana.
 
Hayo ya kilimo kwanza Farm track usilogwe kuchukua, ni vimeo af spare parts zake hazipatikani. Jaribu na matrekta ya Swaraj ni mazuri sana. Kwa bajeti yako hiyo ya 5Ml utaishia kununua 3 disc plough hata used hauwezi kupata kwa pesa hiyo.

Mkuu +255 una data za karibuni za bei ya swaraj FE 855 au FE 744 mpya?
 
unamaanisha hiyo hela ndio ununulie tractor!!!?

Hata zile SWARAJ hupati

old-tractors-for-sal-cc98f.jpg
 
Brand nzuri ni Massey Ferguson na John deer sema kwa hiyo hela labda umpate mtu kaichoka ila ebay kuna za kuanzia £1000 sema process sasa af ni mnada..
 
Back
Top Bottom