Msaada kuhusu hii BVM

Msaada kuhusu hii BVM

atkuwa amekosea kuandika may be alimaanisha Veterinary medicine na si veterani lakini hongera sana kwa kuelezea maana ya hilo lako: naamini aliye kosea kuandika atakuwa makini wakati mwingine.

VETERAN by definition;-
A person with long experience of a particular activity.
OR
A person who has served in the armed forces, especially an old soldier who has seen long service.

Sasa wewe unataka kusoma digrii yake.


Jamaa kaelezea kinoma yaan dah hadi nmecheka kwa sauti
 

Namaanisha unaweza kulinganish ugumu wa bvm na PCB au PCM kwa advance?
Aaamm mimi nilichukua ECA but naheshimu sana hizo comb but nahisi chuo ni pagumu zaidi ya Advance.Anyway tusubiri hiyo October/November tukajionee wenyewe inshallah!!
 
Namaanisha unaweza kulinganish ugumu wa bvm na PCB au PCM kwa advance?
Niseme tu ni zaidi ya Advance lakini watu wanamaliza hivyo isikutie shaka ingawa bidii na nidhamu ya hali ya juu inatakiwa kama unataka uwe na ufaulu mzuri.
 
Bro
wakuu nimejaribu kuchagua hii kozi ya BVM i mean bachelor of veteran medicine pale SUA.
Je hi kozi inakuaje hapa tz kwani nahtaji kuingia huko.
Na je ajira zake zipo za kueleweka ama unaweza kujiajiri mwenyewe katika maisha baadae au ni lazima uajiliwe??[/QUO bro Ni koz nzuri Sana Bt msuli wake co WA nchi hii
 
Aaamm mimi nilichukua ECA but naheshimu sana hizo comb but nahisi chuo ni pagumu zaidi ya Advance.Anyway tusubiri hiyo October/November tukajionee wenyewe inshallah!!
aisee BVM uslinganishe na msuli WA advance BVM Ni Atari haiuzwi chino ya umri weka mbali na watoto
 
BVM ndio kozi rahisi rahisi kuliko kozi zote pale sua. Tatizo lake ni muda tu wa kozi ambao ni mrefu.miaka mitano.
Ikifuatiwa na Bsc Agriculture general, Bsc Agric Engeneer, Biotechnology ,nutrition, informatics

Hizi ndio kozi rahisi sana kupita maelezo na zina future nzuri sana.
Ni very rare kusikia mtu wa kozi hizi ka-disco . Mara nyingi wanaishia ku-carry tu.


Ukilinganisha na kozi ngumu sana ambazo ni pamoja na Bachelor of Rural Dev, BTM, Extension, informatics, agribusiness, wildlife
Hakuna coz ngumu pale we ni kichwa chako ndo ngumu.
 
BVM ndio kozi rahisi rahisi kuliko kozi zote pale sua. Tatizo lake ni muda tu wa kozi ambao ni mrefu.miaka mitano.
Ikifuatiwa na Bsc Agriculture general, Bsc Agric Engeneer, Biotechnology ,nutrition, informatics

Hizi ndio kozi rahisi sana kupita maelezo na zina future nzuri sana.
Ni very rare kusikia mtu wa kozi hizi ka-disco . Mara nyingi wanaishia ku-carry tu.


Ukilinganisha na kozi ngumu sana ambazo ni pamoja na Bachelor of Rural Dev, BTM, Extension, informatics, agribusiness, wildlife
We ndo uko na kichwa ngumu, acha kuita coz za watu rahisi, we unafikir unajuaa kila kitu...
 
BVM ndio kozi rahisi rahisi kuliko kozi zote pale sua. Tatizo lake ni muda tu wa kozi ambao ni mrefu.miaka mitano.
Ikifuatiwa na Bsc Agriculture general, Bsc Agric Engeneer, Biotechnology ,nutrition, informatics

Hizi ndio kozi rahisi sana kupita maelezo na zina future nzuri sana.
Ni very rare kusikia mtu wa kozi hizi ka-disco . Mara nyingi wanaishia ku-carry tu.


Ukilinganisha na kozi ngumu sana ambazo ni pamoja na Bachelor of Rural Dev, BTM, Extension, informatics, agribusiness, wildlife

Mkuu sina hakika kama unatania au vipi. Naamini unapotosha hali halisi. Katika course za SUA BVM sio tu ni ndefu kuliko nyingine zote, BVM watu hawa-carry forward una repeat year au una-retake somo. Sitaki kusema ni ngumu lakini kukaza mgongo ni lazima na disco ni kawaida. Cha msingi kile kitu vijana mnaita bata-BVM kwa mwanafunzi wa kawaida atakuambia hakuna bata. Kuna kitu tunaita 0745-1930 ndio maisha ya wanafunzi wa vet darasani.
 
Hakuna coz ngumu pale we ni kichwa chako ndo ngumu.
Kwa sababu vichwa vya watu sio sawa, tukubaliane kuna watu wanaona course fulani ni course ngumu na hao watu wakiwa wengi course hiyo huitwa ngumu na huhitaji misuli ya hali ya juu zaidi ili mtu aweze kufaulu. Hapa naongelea kwa mfano umechukua PCB ukaenda course husika ya ki-PCB na bado course hiyo inahitaji misuli wa juu kwa wengi-course hiyo watu husema ni ngumu, haina maana ni ngumu kwa kila mtu.
 
Mkuu sina hakika kama unatania au vipi. Naamini unapotosha hali halisi. Katika course za SUA BVM sio tu ni ndefu kuliko nyingine zote, BVM watu hawa-carry forward una repeat year au una-retake somo. Sitaki kusema ni ngumu lakini kukaza mgongo ni lazima na disco ni kawaida. Cha msingi kile kitu vijana mnaita bata-BVM kwa mwanafunzi wa kawaida atakuambia hakuna bata. Kuna kitu tunaita 0745-1930 ndio maisha ya wanafunzi wa vet darasani.
Mkuu, sijui wewe umesoma lini?. Binafsi nina Miaka nane nyuma hata Huo Mkoa sijawahi kufika tena. Huu uzi una miaka kama miwili tangu ni comment hapa. Hata yule aliyeomba ushauriz kwa Muda wote huu, atakua ameshafanya maamuzi siku nyingi sana.

Sioni haja ya kuwatisha watu wanaotaka ku opt hii Course. Ukiwa na Backgrounds nzuri ya kujituma kimasomo, ni Guarantee tosha kua Unaweza kutoboa bila matatizo yoyote. Cha msingi mtu ajitathmini mwenyewe kwanza. Sio lazima uwe na background ya sayansi tokea advance. Mengi unaenda kuyajulia Darasani bila shida yoyote. Kwasababu yana involve zaidi Practical experience. Ambayo kwangu naiona ni The best teaching method ever.

Unlike Courses kama Agric general, Horti, ndio zinahitaji zaidi mwanafunzi awe na backgrounds za sayansi. Kwasababu ya chemistry

Pia Agribusiness inahitaji kichwa cha Hesabu. Lakini kozi hizi zinakua nyepesi kama darasani mpo wanafunzi wengi.

Nakumbuka BVM ya miaka ile unakuta msichana ni mmoja kozi nzima na mpo 10 tu darasa zima. Mambo yanakua magumu hasa kwenye kuweza kusaidiana baina ya wanafunzi. Na kuna kozi zinapita hakuna msichana Darasani.

Sikuhizi BVM zinajaza fuso. Hii Inasaidia sana Kozi kua nyepesi and With advent of technology na Internet.

Nakumbuka kuna watu waliwahi kututisha kuhusu somo la Biochemistry kwamba ni somo gumu Sana, lakini nililisoma sikuona tatizo lolote. BVM na Forestry ndio courses zisizo na enough leisure time. Vitu ni vingi vya kumeza kuliko Muda. Hivyo inakulazimu hata weekend, Likizo uwe bize sana kukesha na masomo. Ukilinganisha na courses nyingine pale SUA.
Na hii inafanya wengi Kukinai. Ila ndio course pekee yenye guarantee promising future. Hizo kozi nyingine watu wanamaliza wanaanza kua ombaomba na bahasha mkononi.

Kuhusu Disco. Disco ipo ilikuwepo, uliikuta, Utaicha,na itaendelea kuwepo. So long as ni University za Serikali, ambapo wao hawako kibiashara kama Vyuo Binafsi.
Disco ni part and percel ya University education.
 
Sioni haja ya kuwatisha watu wanaotaka ku opt hii Course. Ukiwa na Backgrounds nzuri ya kujituma kimasomo, ni Guarantee tosha kua Unaweza kutoboa bila matatizo yoyote. Cha msingi mtu ajitathmini mwenyewe kwanza. Sio lazima uwe na background ya sayansi tokea advance. Mengi unaenda kuyajulia Darasani bila shida yoyote. Kwasababu yana involve zaidi Practical experience. Ambayo kwangu naiona ni The best teaching method ever.
Kilicho nifanya kujibu mchango wako ni pale uliposema "BVM ndio kozi rahisi rahisi kuliko kozi zote pale sua". Mimi sina nia ya kuwatisha wengine, kama watu wameingia na kugraduate basi inawezekana nia yangu ni kutoa tahadhari ya kuwa BVM sio lele mama. Pia asikudanganye mtu kama huna background ya science BVM utaiona ni mlima kwako ndio maana wanahitaji ufaulu wa Chemistry na Biology. BVM ninayoifahamu mimi ina theoretical material nyingi tu hata huko kwenye practical sio tu ujue unafanya nini bali pia kwa nini unafanya unachofanya na unatakiwa ufaulu practical na theory kila kimoja kivyake.
Mengine uliyoweka ni sawa lakini hayaonyeshi kuwa BVM ni rahisi. By the way last intake walichukua zaidi ya 100 na sasa wako kama 80.
 
Yani ukipata iyo kozi jipange sana misuli mirefu yaukichaa.... Ajira usiulize ukishachaguliwa bcushaweza maisha kikubwa ukatoboe maana sua pagumu.... Iyo ni udaktari wamifugo
Washakuwa wengi hao kwa sasa, wapo mitaani wakisubiri ajira huku wakijiajiri kwa kututibia kuku wetu!!!!
 
Kaka ugumu wake unaweza kuwa kama advance ukisoma PCB/pcm au huko pagumu zaidi
Kwa taarifa yako ni kwamba hakuna hatua ngumu zaidi katika safari ya elimu kama A level. Ukiweza kufanikiwa A level hasa sayansi inabidi mtu afanye uzembe fulani ili ashindwe chuo!!!! Wengi wanazuzuka na maisha ya uhuru na kujiingiza kula bata na mademu hasa baada ya kupata boom!!! Mtu aliyefanya vizuri PCB A level hawezi kushindwa kozi yoyote ya chuo, isipokuwa kama akijisahau na kufanya uzembe!
 
Niseme tu ni zaidi ya Advance lakini watu wanamaliza hivyo isikutie shaka ingawa bidii na nidhamu ya hali ya juu inatakiwa kama unataka uwe na ufaulu mzuri.
Nashukuru sana mkuu,wewe ulisoma comb gani na kama ni PCB wanaweza kuchukua mwisho ngapi maana nasikia mostly ni wenye div 1
 
Back
Top Bottom