Msaada: Kimehamishiwa wapi chuo cha IIT ( Institute of Information Technology )

Msaada: Kimehamishiwa wapi chuo cha IIT ( Institute of Information Technology )

Kama ni mitihani ya NCC Education ya UK unaweza kufanyia kwenye vyuo vingine vinavyofundisha hayo masomo na kusimamia mitihani hiyo.

Mojawapo ya chuo ni Learn IT, kipo mtaa wa Lumumba.
 
Mkuu hicho chuo hakipo tena,baada ya mwenye Chuo mzee Salemwala kufariki,vijana walishindwa kukiendeleza.vipi kuna mtihani ulitaka kufanya hapo?


Oh!! nashukuru sana kwa taarifa Mkuu, hapana kuna ndugu yangu alitaka kwenda kusoma hapo, sijui mbadala wake inaweza kuwa chuo gani kwa sasa
 
Kama ni mitihani ya NCC Education ya UK unaweza kufanyia kwenye vyuo vingine vinavyofundisha hayo masomo na kusimamia mitihani hiyo.

Mojawapo ya chuo ni Learn IT, kipo mtaa wa Lumumba.


Sawa Mkuu, nashukuru sana, yeye anataka kusoma nadhani mambo ya IT anasema aliona courseware zao kwa rafiki yake hivyo akavutiwa kwenda kusoma hapo
 
Mfano mzuri mimi mwenyewe kuna baadhi ya vi assets ninavyo ila hamna hata ndugu yangu mmoja anayejua


Hahahaaa, umenichekesha sana, ni nadra sana mtu kujitolea mfano kwenye mapungufu yake
 
Kama ni mitihani ya NCC Education ya UK unaweza kufanyia kwenye vyuo vingine vinavyofundisha hayo masomo na kusimamia mitihani hiyo.

Mojawapo ya chuo ni Learn IT, kipo mtaa wa Lumumba.
Huo mtaa ni tatizo!
 
Inawezekana yeye ndio alikuwa kila kitu, familia yake hakuihusisha sana kwenye uendeshaji wa chuo.
Na hii inatokea mara nyingi sana kwa sisi Waswahili, tunafanya vitu kwa kujificha sana.
Mfano mzuri mimi mwenyewe kuna baadhi ya vi assets ninavyo ila hamna hata ndugu yangu mmoja anayejua.
Mkuu kuwa makini na hizi mambo. Baba wa Binamu yangu, dk chache kabla ya kukata roho, alikuwa anawatajia wanawe Mali zake, kuna point alifika akawa anataja shamba alilokata viwanja, kabla hajamaliza kusema akafariki.

Mpk sasa mwaka wa pili, haijulikani kama viwanja vipo Mbezi Shamba, Chanika, Mabwepande ama....!
 
Hivi tatizo linakuwa ni nini? Baada ya mwanzilishi kufariki shughuli inaishia hapo. Hii huwezi kukuta kwa wenzetu waHindi au waArab ni kwetu sisi waTz waBantu
Hata mali zako mkuu, ukiondoka, taratibu nazo zitaanza kupotea, sababu wewe ndiyo ulikuwa na uchungu nazo, kuzitunza, uliowaachia hawataweza kuziangalia kama wewe, ni ukweli na tukubaliane na hili..
 
Hawakuwa wabantu mkuu,ni wahindi ila wana uraia wa Tanzania.
Nilisoma pale, ila wakati chuo kipo Mabibo, karibu na NIT, office zao mjini, walikuwa na basi lao hivi, jipya zuri matata sana la kututoa mjini mpaka chuo na kuturudisha, na pale Mabibo chuo kilikuwa fittings and settings mpya kabisa, kila kitu kilikuwapo, projectors, PCs za kumwaga, Library, haki ya nani kilikuwa kizuri mno, kama cha ulaya kabisa..
 
Hivi tatizo linakuwa ni nini? Baada ya mwanzilishi kufariki shughuli inaishia hapo. Hii huwezi kukuta kwa wenzetu waHindi au waArab ni kwetu sisi waTz waBantu
Napenda sketch moja ya KIPANYA, alikuwa anamuuliza kigogo mmoja, "kwani babu yake alimuachia future gani"?, baada ya kigogo kuonekana analundika mahela na mali?!
Kama una watoto, wape elimu mkuu, ya kutosha kama wataweza...Waachie na boma moja ulilokuwa unaishi na vigari vyako..
Zaidi ya hapo kula mali yako tu..Iponde vilivyo..
 
Icho chuo kilikuwa kizuri sana ila niliona wanekifutia usajili sijui kwann, me ni mmojawapo ya watu niliosoma apo walikuwa wanaenda vizuri sana
 
Back
Top Bottom