Msaada kimawazo nataka nihame civil niende computer engeneering

Msaada kimawazo nataka nihame civil niende computer engeneering

Joined
Mar 15, 2016
Posts
8
Reaction score
6
jamani wakubwa heshima zenu... Mimi nimechaguliwa diploma in civil ila nataka niamie computer engeneering kwasabab naipenda computer kutoka moyoni lakini watu wananikatisha tamaa wanasema nafanya kitu cha ajabu... Naombeni msaada kimawazo
 
jamani wakubwa heshima zenu... Mimi nimechaguliwa diploma in civil ila nataka niamie computer engeneering kwasabab naipenda computer kutoka moyoni lakini watu wananikatisha tamaa wanasema nafanya kitu cha ajabu... Naombeni msaada kimawazo
naona unataka kupishana na gari la mshahara wewe.... shauri yako nenda.... lakini utanikumbuka comment yangu ukifika mwaka watatu..... hata mm nilikuwaga na mawazo kama yako nilipochaguliwa Electrical Engineering..... leo hii nafurahia sana sana sekta ya umeme inavonipa ulaji.

Civil bonge la dili. lakini nenda kwa wajivuni ufurahishe moyo wako
 
mkuu kam unaipenda kweli na ni chaguo lako waweza kwenda,kam hujali masuala ya ajira mana mi naona weng wanaona kama utakosa ajira au sehemu ya kujiegesha so do whats in your heart and mind.
 
Agana na Nyonga mkuu!
Mie Nilipenda Beekeeping,ila kwa kukosa ushauri nikaenda teaching!dah,nafanya basi tu!ila 2017 narudi polini kukimbizana na nyuki,nimechoka kukimbizana na wanafunzi!
Mkuu Narudia Tena:Agana na Nyonga!
 
Kama unataka kufa njaa nenda computer engineering. Ukimaliza kozi ya civli hakya nan hukosi kazi. Labda uamue mwenyewe. Pia ukiwa na uwezo unaweza kujiajiri mwenyewe na kuwa contractor unajenga nyumba za watu unapiga pesa. Baki huko huko civil ndio kuna maisha mdogo wangu...
 
DO WHAT YOU LIKE, THE MONEY WILL FOLLOW.. usipoteze muda kutakakujua sijui ipi ipo hot you just remember what your doin is for you, ww na maisha yako. Sasa kama utasubiri wakushauri ss hv ufate usichopenda then tegemea kutegemea mawazo yao mpaka utakapo jitambua...
 
Ushauri wangu kwako kijana mwenzangu. USIHAME CiVIL ENGINEERING. Hayo maneno nimeandika kwa herufi kubwa maksudi. Iko siku utakuja na thread hapa at engineering hailipi akati ulisha ambiwa toka mwanzo. Narudia tena kama kaka yako. Usihame civil engineering
 
jamani wakubwa heshima zenu... Mimi nimechaguliwa diploma in civil ila nataka niamie computer engeneering kwasabab naipenda computer kutoka moyoni lakini watu wananikatisha tamaa wanasema nafanya kitu cha ajabu... Naombeni msaada kimawazo
Kijana unapotea niia,tulia huko huko CIVIL
 
Follow your dreams,live your dream.
Moja kati ya vitu wengi hatufanikiwi ni kutamani kuwa fulani na mwisho wa siku hauiwi, kuna sababu nyingi zinazopelekea hilo kutoke, Mazingira, ushawishi wa ndugu/jamaa marafiki lakini pia Mategemeo yetu kwa baadaye. Miongoni mwa mambo ambayo huwa ninayaogopa ni kuangalia jambo huku ukilenga/au kutarajia mafanikio ya kiuchumi/kipato kupitia fani husika. Hilo limewapoteza wengi baada ya kuwa na matarajio afu wakakuta ndivyo sivyo, Hilo linatokana na ukweli kwamba dunia inapitia mabadiliko katika kila sekunde ya uhai wake. Binafsi niliipenda Civil nilipokuwa darasa la tatu, Ni katika akili ya utoto nilidhamiria kuwa Civil Engineer, Kilichonisukuma ni Passion ya ukarabati wa Mabanda ya mifugo kama Ng'ombe, Mbwa, utengenezaji wa mabomba ya Nyumbani nk. Ni vitu nilivyokuwa nikivipenda sana hata leo. Nilipoanza kuwa mkubwa tamaa iliongezeka siku hadi siku huku nikiona magorofa na mimi nikitamani kuyajenga actually katika kuchezea maudongo nilijenga sana, Maisha yangu hadi sasa yametawaliwa na ukarabati,ujenzi na ufundi ufundi tu. Japo sikuwahi kuwa smart sana darasani ila ndicho nilichokipenda na Mungu alinisaidia hadi sasa niko katika hatua za Mwisho za kutimiza ndoto yangu, Ni kweli Civil Engineering Kwa case ya opportunity ni kweli zipo za kutosha hii inatokana na maendeleo hafifu ya nchi yetu, na fani husika kuwa moja ya hitaji la msingi kabisa la mwanadamu malazi(shelter) hivyo inapelekea kuwa ni fani endelevu yenye fursa zisizoisha sababu binadamu wanazaliana na mahitaji yao yanaendelea kuwa yasio na ukomo.

Follow your dream, Moja kati ya vitu vinavyoweza kuongeza tija na ufanisi katika utendaji wa jambo lolote lile ni pamoja na upendo/dhamira ya ndani ya moyo ya kweli ya muhusika katika kutenda jambo fulani. Kuna uwezekano mkubwa sana tija ya mtu asiyependa jambo fulani katika moyo kuwa hafifu ikilinganishwa na yule anayelipenda bila ya kuzingatia vipato wanavyoviingiza. Nafasi ya kuwa na ubunifu wenye tija na hali ya kujifunza vitu vipya katika fani husika ni kubwa sana kwa mtu anayependa kile anachofanya kuliko yule anayefanya ili apate fedha. Ndivyo ilivyo, Mapenzi katika vitu hutafanya tuvifanye kwa umakini na umaridadi bila ya kuzingatia kile ambacho tutaingiza, kufanya kazi iliyo maridadi na yenye kuleta faida kwa wengi huwa ndio farijiko la moyo.

Kwa mitazamo mingi ya watanzania utaambiwa nenda Civil, Kwa sababu wengi tumelenga tutapata nini na sio tutafanya nini ili tupate hicho tunachokitaka na wengi huwa hatujali kabisa kujifikirisha negative side za uamuzi tunaochukua, kwa mtazamo wa wenzetu, Industry ya Communication na Science ya kompyuta kwa ujumla inakua siku hadi siku, Shida ni pale ambapo tunasoma ili mradi tuhitimu na cheti na sio tuwe competent at world level, Wengi tunasoma tukijifunga kuzitumia taaluma zetu hapa hapa nyumbani, brother nachoweza kukwambia ukiwa smart utafanya kazi duniani mahali popote tu, Ukiona unang'ang'ania hapa hapa kwetu basi jiweke katika kundi lile ambao elimu zao zinatoa tija ya kawaida sana na ni zile zinazoogopa challenge, Nzito sana kujifunza vitu vipya na zipo ili kujaza nafasi na sio kutatua changamoto. Kama unakuwa granted na Muumba akupe uishi Miaka 40 ijayo Kozi unayoitamani haitakuwa kama unavyofikiria ndani ya miaka 10 ijayo mark my Word samahani kwa kuandika Marefu
 
Baki civil ndugu kama kwenu ni tia maji tia maji ila kama mkwanja upo fata moyo unachopenda
 
Naona wengi mnamkatisha tamaa, mimi binafsi nimesoma Bachelor's Degree ya Computer Engineering (hapa nchini) na Master's Degree ya Software Engineering (nje ya nchi).

Hii fani kama unaipenda na ukiwa na bidii ya kusoma zaidi ya yale unayofundishwa darasani basi inalipa possibly kuliko fani nyingine zozote unazoweza kufikiria, wakati ninaanza kusoma watu wengi walinikatisha tamaa na kuniambia nitaishia kuburn cd mtaani na kuua virus kwenye computer za ndugu zangu lakini kutokana na juhudi zangu binafsi nilianza kutengeneza hela wakati bado nipo chuoni, binafsi niliacha kutegemea boom (mkopo) nilipofika mwaka wa 2 chuo.

Nakushauri kama ulianza kujifunza programming kabla hata ya chuo una mwelekeo mzuri na unaweza kufanikiwa sana katika fani hii ukiendelea na juhudi zako.

Wengi unaowaona wababaishaji katika sekta hii ni wale ambao walikimbilia fani bila kujua ni nini hasa wanatakiwa kufanya ili kufanikiwa.
8ToBeGreat_Poster_Black.jpg
 
Naona wengi mnamkatisha tamaa, mimi binafsi nimesoma Bachelor's Degree ya Computer Engineering (hapa nchini) na Master's Degree ya Software Engineering (nje ya nchi).

Hii fani kama unaipenda na ukiwa na bidii ya kusoma zaidi ya yale unayofundishwa darasani basi inalipa possibly kuliko fani nyingine zozote unazoweza kufikiria, wakati ninaanza kusoma watu wengi walinikatisha tamaa na kuniambia nitaishia kuburn cd mtaani na kuua virus kwenye computer za ndugu zangu lakini kutokana na juhudi zangu binafsi nilianza kutengeneza hela wakati bado nipo chuoni, binafsi niliacha kutegemea boom (mkopo) nilipofika mwaka wa 2 chuo.

Nakushauri kama ulianza kujifunza programming kabla hata ya chuo una mwelekeo mzuri na unaweza kufanikiwa sana katika fani hii ukiendelea na juhudi zako.

Wengi unaowaona wababaishaji katika sekta hii ni wale ambao walikimbilia fani bila kujua ni nini hasa wanatakiwa kufanya ili kufanikiwa.
View attachment 430114
bro computer science nayo imekaaje
 
Back
Top Bottom