Nililipiaga Bastola Tsh. 2,700,000 pale Tanganyika Arms mwaka 2015 mwanzoni ,process zinakaanza mpaka kwenye Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Kinondoni kipindi kile DC Alli Happi na RC Makonda mwaka 2016 huo nikahojiwa vizuri tu, ghafla nikatakiwa kwenda kusoma nje kwa miaka 4 PhD duuuh!!!
Nikajiuliza sasa itakuwaje hii Silaha?? Nikafunga safari mpaka dukani Tanganyika Arms pale Stesheni nikamkuta Meneja wa Duka nikamsomesha,uzuri ni mchanga hakuwa na noma, akaniuliza tu utaniachaje, nikamwambia nipe ml.2 hiyo Laki Saba pata ya Chai, akachukua ile Risiti yangu akaniambia baada ya saa moja muamala utasoma nikasema poa, ndani ya Nusu saa tu akawa amenitumia 2ml, nikamshukuru mambo yakawa yameisha hivyo