Mimi si mwanasheria wala mtaalamu, lakini nimekwishasimamia mirathi kama mara mbili. Kwa uzoefu wangu huo mdogo,
Iwapo una maana kuna ndugu yenu amefariki na suala ni kushughulikia/kugawanya mali zake:
(a)Fanyeni kikao cha ndugu za marehemu mchague/kupendekeza msimamizi wa mirathi. Kikao hiki pia kinaweza kusaidia kuorodhesha mali na madeni ya marehemu na pia kutoa mwongozo wa ugawaji wa mali na kushughulikia madeni;
(c) Ni muhimu kufuatilia na kupata cheti cha kifo (RITA) mapema, kwani kitahitajika sana mahakamani na kufuatilia mali za marehemu sehemu kama benki, mashirika ya mafao ya jamii, kwa mwajiri, nk
(d)Shauri la mirathi lifunguliwe mahakama ya mwanzo - ambako kumbukumbu ya kikao cha wanandugu itahitajika, pamoja na cheti cha kifo na uthibitisho wa serikali za mitaa kuhusu kifo, makazi ya marehemu, nk; Iwapo marehemu alikuwa na ukwasi mkubwa shauri litahamishiwa mahakama ya juu zaidi.
(e) Mahakama itamthibitisha msimamizi wa mirathi iwapo itamwona anafaa (baada ya kufuata taratibu zake);
(f) Baada ya kupata hati ya mahakama ya usimamizi wa mirathi, msimamizi afanye kazi ya kukusanya/kuorothesha mali zote za marehemu, ashughulikie madeni na kugawa mali inayobaki kwa warithi halali kulingana na wosia halali wa marehemu (kama upo), mwongozo wa vikao vya wanandugu, desturi, dini, sheria, nk.
(g) Mahakama husimamia ugawaji mali za marehemu na inapobidi kutoa miongozo - na mara nyingi taarifa ya ugawaji wa mali inabidi ipelekwe mahakamani zoezi linapokamilika.
NB - Sio lazima msimamizi wa mirathi awe miongoni mwa warithi - bali awe mtu anayekubalika/kuaminiwa na wanandugu/warithi watarajiwa.
Aksante kwa maelezo yako mkuu hapo nimekupata....pia napenda kukkliza ni taratibu gani hutumika kupokea fetha za malipo toka ktk mifuko ya jamii,ni kupitia katika akaunti ya msimamizi au?huja kwa mfumo wa cheki na hiyo cheki mnaenda nayo benki,au ni vip?ushauli haraka....
endapo mahakama inapofanya kitendo cha ugawaji bila ya cheki ni makosa au?ni lwamba fedha imelipwa lakini hawajatuonesha cheki ila wanaonesha barua tu....hapo kunaharufu ya uchakachuaji au?Kwangu ilivyokuwa ni kwamba mafao yalilipwa mahakama - ndivyo mahakama ilivyowaelekeza benki na NSSF, na mahakama baada ya kupokea malipo ndiyo iliandika cheki mbalimbali kwa warithi kulingana na mgawo uliopangwa. Ni process iliyochukua muda kiasi.
endapo mahakama inapofanya kitendo cha ugawaji bila ya cheki ni makosa au?ni lwamba fedha imelipwa lakini hawajatuonesha cheki ila wanaonesha barua tu....hapo kunaharufu ya uchakachuaji au?