Ni sahihi ndugu kugombania mirathi ya ndugu yake aliyemjengea nyumba mzazi wake na kuandika jina la mzazi wake kwenye umiliki?

Mohamedex121

JF-Expert Member
Jan 27, 2022
1,688
3,142
Habarini wakuu. Naimani humu nyote ni wazima wa afya. Nilikuwa naomba msaada ya kisheria.

Kuna hili suala la migogoro ya wanafamilia hasa kwenye mirathi ambayo huathiri jamii kwa namna moja ama nyingine na sijui suluhisho ni lipi?

Familia nyingi hasa hizi kwenye jamii zetu unakuta ni familia kubwa zenye ndugu wengi. Ni jambo la kawaida kukuta familia moja kuwa na watoto kumi au zaidi.

Mbali na hayo familia nyingi huwa ni masikini na ni ngumu sana kukuta watoto wengi wa familia moja kuwa na maisha mazuri, unaweza kuta ni mtoto mmoja ama wawili ndio wenye maisha mazuri

Na hili suala la kuwajengea nyumba wazazi kipindi ambacho Mungu amekubariki huwa haliepukiki kwa mtoto mwenye kuwapenda wazazi wake, hii inakuwa kama shukurani kuwapa wazazi na pia kuwapa hifadhi .

Swali langu linakuja apa, hivi ikitokea mtoto akamjengea nyumba mzazi wake na kwenye hati kuandika jina la mzazi wake, je pindi mzazi anapokufa mali zinarudi kwa mtoto aliyemjengea au zinakuwa za familia na kugawana mirathi??

Natanguliza shukurani wakuu.
 
Marekebisho kwenye kichwa cha habari.

Je, ni sahihi ndugu kugombania mirathi ya Ndugu mwenzie aliyemjengea nyumba mzazi wake na kuandikisha jina la mzazi wake kwenye hati miliki.
 
Ukimjengea kwenye kiwanja cha familia automatically hio itakua mali ya wote kwenye urithi.

ukitaka mali isihesabike kama ya familia ,mjengee bi mkubwa nyumba kwenye kiwanja chenye jina lako alafu muache akae,otherwise ukijenga kwenye kiwanja cha familia ndugu wanaweza kudai endapo siku huyo mzazi asipokuwepo na kisheria mtagawana sababu ipo kwenye kiwanja cha familia na wana hio haki .
 
Swali langu linakuja apa, hivi ikitokea mtoto akamjengea nyumba mzazi wake na kwenye hati kuandika jina la mzazi wake, je pindi mzazi anapokufa mali zinarudi kwa mtoto aliyemjengea au zinakuwa za familia na kugawana mirathi??
Kinachogawiwa ni mali ya marehemu... kama mtoto mmoja aliamua ampe mali mzazi, maana yake hata wenzake watarithi.

Tena kama ni kwenye kiwanja cha familia, ndio ishakuwa mali ya familia. Labda kama ni sehemu nyingine, mzazi kwa busara anaweza kuandika wosia wa kukupa hiyo nyumba.

Ukimpa mzazi umeipa familia... kama lengo lingekuwa kubaki nayo, tafuta eneo private, jenga, bakiza umiliki kwako. Akifa hakuna wa kuulizia.
 
Ukimjengea kwenye kiwanja cha familia automatically hio itakua mali ya wote kwenye urithi.

ukitaka mali isihesabike kama ya familia ,mjengee bi mkubwa nyumba kwenye kiwanja chenye jina lako alafu muache akae,otherwise ukijenga kwenye kiwanja cha familia ndugu wanaweza kudai endapo siku huyo mzazi asipokuwepo na kisheria mtagawana sababu ipo kwenye kiwanja cha familia na wana hio haki .
Na kama kiwanja ulinunua ila ukaandika jina la mzazi kwenye hati miliki nayo pia inakuwa mali ya familia??
 
Kinachogawiwa ni mali ya marehemu... kama mtoto mmoja aliamua ampe mali mzazi, maana yake hata wenzake watarithi.

Tena kama ni kwenye kiwanja cha familia, ndio ishakuwa mali ya familia. Labda kama ni sehemu nyingine, mzazi kwa busara anaweza kuandika wosia wa kukupa hiyo nyumba.

Ukimpa mzazi umeipa familia... kama lengo lingekuwa kubaki nayo, tafuta eneo private, jenga, bakiza umiliki kwako. Akifa hakuna wa kuulizia.
Hapana kiwanja si cha familia bali kimenunuliwa na mtoto kisha kumuandikisha jina la mzazi je apo kutakuwa na mgawanyo wa mali au mpaka marehemu atoe wosia mali zirudi kwa mwanae??
 
Kumuandika mzazi ndio kaipa familia. Kosa lilikuwa kuandika jina la mzazi. Walau mzazi angesema kwenye wosia.
Inasikitisha sana, je kuna njia ya namna kusitisha jina la mirathi kutoka kwa mzazi hadi kwa mtoto?? Bila kuathiri undugu?
 
Habarini wakuu. Naimani humu nyote ni wazima wa afya. Nilikuwa naomba msaada ya kisheria.

Kuna hili suala la migogoro ya wanafamilia hasa kwenye mirathi ambayo huathiri jamii kwa namna moja ama nyingine na sijui suluhisho ni lipi?

Familia nyingi hasa hizi kwenye jamii zetu unakuta ni familia kubwa zenye ndugu wengi. Ni jambo la kawaida kukuta familia moja kuwa na watoto kumi au zaidi.

Mbali na hayo familia nyingi huwa ni masikini na ni ngumu sana kukuta watoto wengi wa familia moja kuwa na maisha mazuri, unaweza kuta ni mtoto mmoja ama wawili ndio wenye maisha mazuri

Na hili suala la kuwajengea nyumba wazazi kipindi ambacho Mungu amekubariki huwa haliepukiki kwa mtoto mwenye kuwapenda wazazi wake, hii inakuwa kama shukurani kuwapa wazazi na pia kuwapa hifadhi .

Swali langu linakuja apa, hivi ikitokea mtoto akamjengea nyumba mzazi wake na kwenye hati kuandika jina la mzazi wake, je pindi mzazi anapokufa mali zinarudi kwa mtoto aliyemjengea au zinakuwa za familia na kugawana mirathi??

Natanguliza shukurani wakuu.
Pole mkuu sheria ya Tanzania na duniani kote.
Mwenye jina kwenye hati ndio mmiliki wa nyumba.
Kama ulikuwa ujui hilo pole hio nyumba ni mgao wa familia mzima.

Jamani kama mtu unataka kumjengea wazee wako nunua kiwanja chako Jenga nyumba kwa jina lako ndipo waweke wazee.
Usiandike jina la mzazi wako. Hio nyumba ni ya familia.
 
Duh! Unaweza kukata rufaa mali zikarudi kwa mtoto aliyemjengea badala ya huyo aliyerithishwa mali ambayo hajaitolea jasho
Kurudisha mpaka mzazi aamue kukurudishia .
Mpaka hapo hio nyumba kama umejenga sio ya kwako kwa 100%.
Ni ya mzazi maana ndio jina lake limeandikwa kwenye kiwanja.

Kurudisha mpk yeye aamue ndivyo sheria inavyosema mkuu.
Sijui kama kutakuwa na namana yoyote labda tafuta mwanasheria akushauri.
 
Back
Top Bottom