Msaada: Jinsi ya kuvunja ndoa ya kikristo

Joined
Mar 22, 2023
Posts
23
Reaction score
21
Habari ndugu zangu, naishi Kigoma, nina lafiki yangu wa kike alifunga ndoa na mwanaume mmoja hivi toka wameona mwanaume hajawahi kushiriki tendo la ndoa na hana uwezo kabisa.

Wameishi miezi 3, hali hiyo imefanya binti arudi kwao. Kwa sasa anamiezi 2 na amepata mchumba mwingine, je, anawezaje kuvunja ndoa?

Naomba ushauri wapendwa.
 
Mwambie asilimu kwanza atumie kigezo cha kusilimu kumuacha.
 
Walifunga ndoa kanisani? Aende kwa mchungaji atoe lalamiko lake,ndoa inavunjwa fasta ,kama kweli jamaa jogoo hawiki, bila jogoo kuwika hakuna ndoa hapo
 
Ndoa ya kikristu ni balaa wakifuata utaratibu awatafute watu wote waliohudhuria siku ya ndoa wote waje kama walivyokuwa wamevaa kama walikuwa wajawazito waje na mimba zao.
 
Baada ya kufuga ndoa kanisani basi ndoa hukamilishwa kwa tendo la ndoa, bila tendo la ndoa hiyo sio ndoa. Moja kwa moja hicho ni kizuizi cha ndoa, ndio maana mnaambiwa muonjane kabla ya ndoa japo si vizuri.
 
Urongo ulio tukuka
Ndoa ya kikristu ni balaa wakifuata utaratibu awatafute watu wote waliohudhuria siku ya ndoa wote waje kama walivyokuwa wamevaa kama walikuwa wajawazito waje na mimba zao.
 
Hiyo ndoa kuivunja ni rahisi sana

Ndoa bila tendo la ndoa ni ndoa batili.

Kama hataki mzunguko mrefu Asiende kanisani.

Aende baraza la kata. Watawasikiliza wote wawili kisha watapewa cheti cha kata. Ambacho watapeleka mahakamani na kuivunja hiyo ndoa kisheria. Ndani ya mwezi mmoja tu kila kitu kinakamilika

Kanisani watawazungusha zungusha sana
 
Shida mwanaume hataki kuja kila tunapo ongea nae wala kanisan
 
Sheria ya ndoa ya Kikristo inasema hivi, “without consummation, marriage is invalid” wao wanasema “ratum sed non consummatum” yaani ndoa huwa ni batili au tuseme hakuna ndoa kabisa iwapo tendo la ndoa halikufanyika baada ya kiapo cha ndoa, yaani zile process na mbwembwe zote za kanisani.
Hapo hakuna ndoa mkuu, kama ni Mkatoliki huyo binti aende aongee na Baba Paroko atamsaidia kwa kutumia sheria ya ndoa ndani ya sheria ya kanisa yaani “code of canon law no; 1983. Hiyo ni rahisi sana ndugu, au wewe ndo unataka ukamate chuma!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…