Uncle Jei Jei
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 1,684
- 2,157
Habari mwanaJF hasa wa jukwaa hili la wajasiria mali, nikiri kuwa limekuwa msaada mkubwa wa mawazo kwa watu mbalimbali. Back to the topic; kuna ndugu yangu mhitimu wa chuo kikuu katika fani ya Literature, huyu ndugu ni mbunifu wa stori na ukiachilia mbali elimu yake, lakini pia ana kipaji cha uandishi wa vitabu. Mpaka sasa anavitabu kadhaa ambavyo walim wake wa chuo kikuu walivipitia na kumpongeza kwa kazi nzuri inayoichora jamii ya Tanzania. Challenge imebaki jinsi ya kuviingiza sokoni ili afaidi matunda ya kazi yake! Hivi ili kitabu cha riwaya kikubarike na Taasisi ya Elimu Tanzania ni hatua gani hufuatwa?? Na malipo yake yanakuwaje??