- Thread starter
- #21
umeshafikia maamuzi yoyote?
kumpenda nampenda ila yeye nitatizo sasa! Maamuzi bado kwa kweli...
umeshafikia maamuzi yoyote?
Kuna kipindi aliniambia naomba ubadilishe muonekano wako, kwanza kwa kuacha kuvaa tshat na jins na badala yake uvae suruali za kitambaa na mashati.. Nilikubali nikaanza kushona suruali za vitambaa na mashati nikawa smati sana, hata sasa navaa sana na kuwa smati, lakini ndo hivyo hataki hataki!
Ni mtazamo wangu; alikupenda kwasababu ya pesa zako sasa zimepotea anaona humfai tena jipange upya usimtegemee sanaMimi nina mke na mtoto mmoja, kwa bahati mbaya mke wangu anaishi mbali na mimi mikoa tofauti, tunaishi hivyo kwa kuwa yeye ni mwajiriwa wa serikali na mimi ni mfanyabiashara, hivyo bado hajapata uhamisho wa kunifata mimi. Tumefunga ndoa na ndoa yetu ina mwaka na miezi 6 huwa tunatembeleana kila panapopatikana nafasi... Lakini cha kushangaza ni kwamba ninapomtembelea mke wangu huyo huwa hapendi kabisa kutembea na mimi! Kwa mfano siku za jumapili ukimwambia twende kanisani haendi!. Lakini nikiwa sipo anaenda ukimuuliza hana sababu. Hata pengine anaenda sehemu hawezi kamwe kukubali muende pamoja, katika mazungumzo yetu sametime ananiambia sijui kusalimia, mara hawezi kwenda na mimi popote! Tena anaapia! Kwa kweli kimshiko mimi kabla ya kufunga nae ndoa nilikuwa vizuri kwani hata nnyumba nimejenga, lakini kutokana na mambo fulani biashara imekata sana, hivyo sametime hunipiga tafu hasa upande wa familia... TATIZO LINGINE ALILONALO NI MTU ANAENUNA KWA JAMBO DOGO SANA! Tukiwa pamoja haipiti siku 3 utamkuta kanuna kwa kitu cha kijinga tu..! Ila hakuwa hivyo awali... NIKO KWENYE MAJUTO NAOBENI MSAADA WA MAWAZO NINI CHANZO! Kumpenda nampenda kupitiliza ila tatizo ni hayo.
kaka, una jambo lolote umeamua kulifanya? ​
Mh! miezi 6 ya ndoa keshajuta kuolewa? Basi labda alikuwa anataka ndoa na si wewe kwa hiyo mawazo yake yalikuwa kwenye ndoa bila kujali nani anamuoa; sasa matarajio yake yameenda kinyume baada ya kuanza kuishi uhalisia. Dalili ndo kama hizo za kukuambia ubadili mitindo ya nguo n.k. Ukiona mwaka wa kwanza kwenye ndoa unakuwa mgumu basi ujue hiyo ndoa ilijengwa kwenye msingi mbovu, vinginevyo mwaka wa kwanza unatarajiwa kuwa wa asali kama mlijenga ndoa yenu kwenye msingi imara. Mapenzi peke yake hata yawe yale ya kuonana kwenye glasi hayatoshi kujenga uhusiano imara. Mahusiano mengi tu yanavunjika watu wakiwa bado wanapendana. Sasa kwenu kuna moja kati ya haya mawili: 1). Umechagua mke sahihi na mkeo kachagua mume sahihi ila hampendani kiusahihi kwa maana kwamba jinsi yenu ya kuwasiliana haiko sawa, wote hamjui namna ya kuwekana karibu au mmoja anajua, mwingine hataki, hamsemi wazi mnachokitaka matokeo yake mnahisi hamtakani, mmoja wenu, hasa mkeo haupi uhusiano uzito unaotakiwa. 2) Uko na mtu asiye sahihi kwako:-jinsi yenu ya kupenda na mtindo wa maisha havifanani, itikadi zenu haziendani kwa kiasi kikubwa n.k.
Umbali mara nyingi unaleta matatizo pale wahusika wanapokuwa mbali mbali halafu wakaja kuoana na kuishi pamoja. Hapa kila mmoja anaanza kuzijua rangi za mwenzie maana zamani walikuwa wakitemebeleana wanaonyeshana mazuri tu, lakini kwa hawa waliotengana baada ya ndoa tena kidogo tu maana simu zipo na wanatembeleana umbali ulitarajiwa uwe kiungo cha mahaba. Kumisiana kutamu jameni. Sasa si vizuri kukimbilia kuhisi anachepuka ingawa uwezekano upo. Nenda mdogo mdogo baba ujue tatizo nini. Ukishalijua lipime, kama linarekebishika hewala, kama halirekebishiki basi kila mmoja akae mkoa wake kivyake vyake atafute wa kufanana nae. Hukufunga ndoa na wakati, ulifunga na mtu. Yale mambo ya milele mimi nayaheshimu sana lakini huwa tunatamka kwa imani bila kujua kesho italeta nini.
siyo miezi 6 ni mwaka na miezi 6, mwanzo wa ndoa nilidhani ni mimba lakini baada ya kujifungua bado yuko hivyo hivyo..! Kununa umekuwa ni ugonjwa wake, hata liwe jambo la utani tu!!
Lkn awe na kifua, usijemsababishia stroke akaacha wenzake wanafaidiMkuuu kaa macho ndoa yako iko njia panda hzo ni dalili za mwanamke kukuchoka cha msingi,FANYA UCHUNGUZI BILA YEYE KUJUA,NENDA MTAANI UNAPOISHI PIGA STORI NA WANA WATAKUPA UMBEA 2,PENDA KWENDA KWAKE BILA TAARIFA KWA KUSITUKIZA UCKU MIDA YA SAA 2 LAZM UTAJUA MBIVU NA MBICHI.
kuna wakati pia huniambia anajuta kuolewa!
ha ha mkuu bora ukathibitisha na kujua kuwa unasalitiwa,na kuchukua hatua KULIKO kuhisi unamegewa,utakonda bila ugonjwa mwilin.MAPENZI NI UGONJWA HATARI TENA HAUNA TIBA WALA DAKTARI.Lkn awe na kifua, usijemsababishia stroke akaacha wenzake wanafaidi
ha ha mkuu bora ukathibitisha na kujua kuwa unasalitiwa,na kuchukua hatua KULIKO kuhisi unamegewa,utakonda bila ugonjwa mwilin.MAPENZI NI UGONJWA HATARI TENA HAUNA TIBA WALA DAKTARI.
Nina wasiwasi huko aliko katangaza hajaolewa
kuna wakati pia huniambia anajuta kuolewa!
kumpenda nampenda ila yeye nitatizo sasa! Maamuzi bado kwa kweli...
siyo miezi 6 ni mwaka na miezi 6, mwanzo wa ndoa nilidhani ni mimba lakini baada ya kujifungua bado yuko hivyo hivyo..! Kununa umekuwa ni ugonjwa wake, hata liwe jambo la utani tu!!