kwa mujibu wa imani yangu kwamba yeyote atakaeishi hapa duniani kwa kutenda mema,kuepuka maovu na kufuata maelekezo yote ya Mungu muumbaji basi mtu huyo ujira wake ni kuingizwa peponi siku hiyo ya kiama.Huko peponi inategemea na kiwango chako cha uchamungu ulicokitenda hapa Duniani.Suala la kuabudu huko halitokuwepo,huko ni starehe mwanzo mwisho.Na ili kukabiliana na starehe hizo Mungu muumbaji atakurudisha/kukupandisha kuwa na umri wa miaka 20 mpk 25 hivi hakuna kuzeeka wala KUFA ni maisha ya milele. Na kubwa kuliko zote wewe kama ni wa kiume kwa idadi ya chini kabisa utaozeshwa warembo mabikra maalum 70 wanawake ambao uzuri wao ni Mungu pekee anaejua....kiufupi ni kwamba uzuri wao hauelezeki na hawazoeleki pia "TWAHARA" yan wako safi muda wote na huko wewe utatumikiwa kama mfalme lakini pia Mungu atakupa uwezo wa pekee kuwakabili hao wanawake.Starehe zitakuwa nyingi mno ila kwa upande wa kuoa kiufupi ndo hivyo.Hii ni kwa mujibu wa dini yangu ya kiislamu...........kama huyaamini haya hulazimishwi kuyaamini ila USISAHAU TU KWAMBA MOJA YA SHARTI LA KUINGIA PEPONI NI LAZIMA UAMINI...uamini aliyokuja nayo Adam mpk mtume wa mwisho ambaye ni Muhammad s.a.w.