Msaada: Hivi kibox cheusi ni cha nini katika ndege

Msaada: Hivi kibox cheusi ni cha nini katika ndege

Kama hakina nafasi waambie wakuchongee chako, abiria mfalme bwana ala!

Haaaahhhh unanifanya nicheke maana black box ni kidogo sana kina urefu ucozidi robo mita(0.25m) isitoshe kinakaa mkiani mwa ndege na si ndani wanapokaa abiria kwa hiyo uwezekano wa wewe kuishi ni mdogo pia
 
Picha yake
 

Attachments

  • 1420664865587.jpg
    1420664865587.jpg
    8.1 KB · Views: 273
  • 1420664883338.jpg
    1420664883338.jpg
    8.6 KB · Views: 244
  • 1420664892710.jpg
    1420664892710.jpg
    14.9 KB · Views: 242
Wakuu katika kitu kinacho nichanganyaga na kunifanya niwe na maswali mengi ni kuhusu hiki kidude kitwacho box nyeusi
Kwakweli mawazo yangu huenda mbali na kuanza kuwaza mambo ya kishirikina kuwa labda ni hirizi za wazungu au kinakuwa na roho za watu maana pindi ndege ikipinduka watu wapo maradhi kupoteza ma milioni ya fedha za madafu mpaka kipatikane
Je hiki ni kidude cha nini na kwanini watu wasitafute mabaki ya watu bali hukitafuta hiki kitu ...


scatter

Ndege huwa haipinduki mkuu. Kama wewe ni rafiki wa ushirikina basi hata uelezwe vipi scientifically huwezi kuelewa. Nenda kwenye YouTube katafute clips za wataalam utaelewa ingawaje sina uhakika kama utaelewa kama sio kulewa!
 
Mungai.... -> Mulugo -> Kawambwa

Elimu na Maarifa ya kizazi hiki vimeshuka sana...!

hahaha mkuu..baba enock anafikiria hirizi ya mzungu n.k..sasa unadhani enoki atakua na utandawazi na fikra gani kama baba upewo wake upo hapo
 
Nami naomba niulize maswali ya nyongeza, baada ya majibu yote hayo, mosi je chaweza fanyiwa hujuma? Pili kinapopotea ni njia gani zinatumika kukipata?, tatu je taarifa uchukuliwa hata kama hajali haijatokea? Nne imewahi tokea wanashindwa kukipata? Ni hayo tu naomba wataalamu mnijibu.
 
Priority ya kwanza kabisa ni kuokoa maisha!
Mda ukipita kiasi cha wataalam kuamini kuwa uwezekano wa kuokoa maisha haupo tena bali ni kutafuta na kuokota maiti tu, hapo ndipo wanagawana majukumu na kuanza kutafuta mabaki ya ndege na hizo visanduku vyeusi.

Hizo "black boxes" ziko mbili.
Moja ina record mitambo, na hali ya kiufundi ya ndege, na jinsi ilivyo endeshwa. (DFDR)
Cha pili hurekodi sauti na mawasiliano kati yamarubani na controllers, na sauti zozote za chumbani mwa kuendeshe (cockpit), Inaitwa Cockpit Voice Recorder (CVR).
Vimetengenezwa kwa kutumia chuma cha pua, hivyo vinaweza kuhimili moto mkali, kuvunjika na maji baharini.

Mwonekano wa kiifaa kiitwacho "Black Box" .
Nadhani sasa hapo tupo pamoja abandugu kwani tulio wengi pich yake hatuijui au hata hatujawahi kuiona.
 

Attachments

  • BALCK2.jpg
    BALCK2.jpg
    23.1 KB · Views: 115
  • BLACK3.jpg
    BLACK3.jpg
    8.7 KB · Views: 109
  • black-box-cutaway.gif
    black-box-cutaway.gif
    27.6 KB · Views: 147
  • ENGQ33.JPG
    ENGQ33.JPG
    38.3 KB · Views: 112
  • images2.jpg
    images2.jpg
    10.4 KB · Views: 109
Nami naomba niulize maswali ya nyongeza, baada ya majibu yote hayo, mosi je chaweza fanyiwa hujuma? Pili kinapopotea ni njia gani zinatumika kukipata?, tatu je taarifa uchukuliwa hata kama hajali haijatokea? Nne imewahi tokea wanashindwa kukipata? Ni hayo tu naomba wataalamu mnijibu.

Mosi:Ndio chaweza fanyiwa hujuma hasa kama kuna mambo ya uhasama hasa umafia kwa mamlaka husika "mfano nchi husika na nchi nyingine " mfano mzuri kuna ndege kadhaa za viongozi wakubwa wa nchi au watu maalufu zisha anguka na hicho kibox kinachotegemewa kiwe na taarifa husika juu ya mwendo wa ajali husika huwekwa kapuni na wahusika ili kukidhi matakwa yao kwa kisingizio cha mambo ya usalam wa Taifa, n.k hasa kwa zile ndege za kimataifa, na pia kama wahusika wanataka kuficha taarifa flani flani kuhusu chanzo halisi cha ndege husika.

Pili:Utafutaji wa hicho kibox cheusi ni kwa kutumia "signals" maalumu ambazo huonesha maala kilipo angukia . Yaani kina "signal detectors" kama ambavyo askari au wanajeshi wanavyoweza kwenda msituni au maala flani kusaka bomuau mlipuko uliotokea sehemu flani ulikuwa ni wa kitu gani , utakuta hapo ni lazima kuwe kuna vifaa vinavyoweza ku detect uwepo wa kitu husika kinachotafutwa.

Tatu: Ndio , taarifa huanza kuchukuliwa punde ndege inapoanza maandalizi ya safari husika mpaka ilipo pata ajali husika.

Nne: Ndio wanaweza shindwa kukipata kama muda mrefu umepita toka ndege husika ipate ajali , mfano miezi 3 au zaidi tokea ajali itokee, kwani na chenyewe huweza kuishiwa chaji yake iliyowekwa kukitunza, mfano ndege ya malaysia ilivyopotea mazima hapo juzi kati au zile ndege ambazo huanguka maeneo ya "Bermuda Triangle" n.k au maeneo ya uhasama mfano katika uwanja wa vita.
 
Ajali ya ndege Air Asia iliyotokea karibu wiki tatu zilizopita, viboksi vyeusi vyote viwili vimepatikana.
Iliyobaki ni wataalamu kuvisoma na kutafsiri kilichorekodiwa.
Ulimwengu utajua nini chanzo hasa cha ajali hii. Data nyingi na mawasiliano yote huwemo humu.
Picha kamili karibu itapatikana sasa.

Na pia wataalam watajifunza mengi ili wafanye marekebisho yapasayo kuhakikisha usafiri wa anga unabaki kuwa ndio wa usalama zaidi kuliko wowote duniani.
 
kiboksi chenyewe ni cha orange...black box zamani. kazi yake ni kuhifadhi mwenendo mzima wa ndege ikiwemo maongezi baina ya marubani, kwahio ajali ilkitokea wakikipata hiki ni rahisi kujua chanzo cha ajali....pia kinawekewa kifaa[transponder] ambacho kinatoa signal kuashiria kipo wapi ili iwe rahisi kukipata.

Ingekua hivyo basi Wamalaysia wasingehangaika mwaka Mzima wanatafuta ndege hawaioni
 
Ingekua hivyo basi Wamalaysia wasingehangaika mwaka Mzima wanatafuta ndege hawaioni

Ndugu, hiyo signal yake siyo powerful kama signal ya minara ya simu au mawimbi ya radio, kwa hiyo ni muhimu pia eneo ilipongukia ndege lifahamike kwanza ndipo kiweze kutafutwa!

Kumbuka kuwa kujulikana kwa eneo ndege ilipoangukia ndio huweza kufnikisha kupatikana kwake na sio kinyume chake.
 
Duuuh! mleta mada ameonyesha a very low profile ya ku-reason....! PLZ KADI YAKO YA CLINIC IPO?
 
Mosi:Ndio chaweza fanyiwa hujuma hasa kama kuna mambo ya uhasama hasa umafia kwa mamlaka husika "mfano nchi husika na nchi nyingine " mfano mzuri kuna ndege kadhaa za viongozi wakubwa wa nchi au watu maalufu zisha anguka na hicho kibox kinachotegemewa kiwe na taarifa husika juu ya mwendo wa ajali husika huwekwa kapuni na wahusika ili kukidhi matakwa yao kwa kisingizio cha mambo ya usalam wa Taifa, n.k hasa kwa zile ndege za kimataifa, na pia kama wahusika wanataka kuficha taarifa flani flani kuhusu chanzo halisi cha ndege husika.

Pili:Utafutaji wa hicho kibox cheusi ni kwa kutumia "signals" maalumu ambazo huonesha maala kilipo angukia . Yaani kina "signal detectors" kama ambavyo askari au wanajeshi wanavyoweza kwenda msituni au maala flani kusaka bomuau mlipuko uliotokea sehemu flani ulikuwa ni wa kitu gani , utakuta hapo ni lazima kuwe kuna vifaa vinavyoweza ku detect uwepo wa kitu husika kinachotafutwa.

Tatu: Ndio , taarifa huanza kuchukuliwa punde ndege inapoanza maandalizi ya safari husika mpaka ilipo pata ajali husika.

Nne: Ndio wanaweza shindwa kukipata kama muda mrefu umepita toka ndege husika ipate ajali , mfano miezi 3 au zaidi tokea ajali itokee, kwani na chenyewe huweza kuishiwa chaji yake iliyowekwa kukitunza, mfano ndege ya malaysia ilivyopotea mazima hapo juzi kati au zile ndege ambazo huanguka maeneo ya "Bermuda Triangle" n.k au maeneo ya uhasama mfano katika uwanja wa vita.

Ahsante sana mkuu kwa majibu yako muruwa.
 
Nahisi ndegezetu fastjet na presitio hazina hicho kifaa.
 
Fikie sasa watengeneze ndege kama blackbox ili ikipata ajali isiharibike watu wapone.
 
Nahisi ndegezetu fastjet na presitio hazina hicho kifaa.

Unachokusema hakina ukweli hata wa 0.001%. Ili upate kibali cha kutengeneza ndege mamlaka husika za dunia, uingereza au za marekani lazima wahakikishe kuwa unakidhi vigezo vinavgotakiwa ikiwemo black box na vitu vingine vingi. Pia mamlaka husika ya nchi unakofanyia biashara ya kusafirisha abiria au mizigo haitaweza kukupatia kibali kama ndege yako haina vitu vinavyotakiwa ikiwemi black box. Mpaka unafanya biashara ya kusafirisha watu hupati kibali kirahisi rahisi na kila baada ya muda flani mamlaka husika ya nchi unakofanyia biashara yako inakutembelea na kukukagua kama ndege zako bado zinavigezo vya kusafiri angani. Pia mamlaka husika kwa tanzania TCAA hawakupatiikibali kama hauna ndege zaidi ya moja. Na vigezo vingine vingi, tupendelee kutembelea mitandao ya taasisi zetu ili tujue hata wanafanyaje kazi
 
Back
Top Bottom