Msaada: HIV Non reactive

sundoka

JF-Expert Member
Oct 9, 2011
2,067
2,752
Habari za mida wadau,

Leo katika pitapita zangu huku kijijini nikakuta mahali AMREF wameweka mahema yao wanatoa huduma za kupima magonjwa kama HIV, TB, Cancer, tezi dume, n.k bure.

Kwa kuwa nlikiwa napanga several times kwenda mjini kupima ngoma nikaona bora nimalizie shida yangu ya kupima pale.

Sasa baada ya kutolewa damu nikaambiwa nisubiri nje kama dk. 5 then nitakuta majibu yako tayari.

Wakati nipo pale nje akatokea kijana mmoja mle ndani tayari amepima na kapewa kadi yake tayari na nikaona nyuma imeandikwa HIV neg na ameandikiwa tar ya kurud kupima tena. Nikamuuliza aliingia ndani pale muda gani akaniambia asa hivi tu na aliniona natoka mimi ndo akaingia.

Baada ya dakika 6 nikaenda tena ndani kwenye hema kufata majibu lakini hapo nishaanza kuwa na wasiwasi nikaanza kujiuliza kwa nini mimi nimeambiwa nisubiri dakika 5 wakati huyu bwa mdogo hakuchukua hata dk 3 katoka na majibu???

Nilipofika ndani yule mama mpimaji akaniambia majibu yangu ni mazuri sina maambukizi ya UKIMWI. Akanipa hii kadi
IMG_20170424_171238.jpg
IMG_20170424_171247.jpg
IMG_20170424_171247.jpg


Baada ya kuona hii kadi moyo wangu uliripuka kidogo. Kila nikipima sijawahi kuandikiwa hivi "Non Reactive" sasa iweje leo?? Nikatoka nikiwa na maswali mengi na nikiamini kuna kitu cha ziada hapa. Sababu zinazonifanya niwe na mashaka labda huyu mama ananificha kitu ni hizi:

1. Kitendo cha kunisubirisha mimi nje muda mrefu wakat kuna mwingine amewahishwa (nahisi alikuwa anapanga anitoke vipi)
2. Kitendo cha yule mama kutaka kuninyima ile kadi yenye majibu. Baada ya kuniambia sijaathirika nilinyoosha mkono kuchukua ile kadi akaniambia hata nisipoichukua ile kadi niende zangu tu home niendelee na ishu zangu akiniambia eti ile kadi anapewa aliyeathirika ili aendelee kupima TB. Nikamwambia nataka nipime na TB maana huwa nina tendency ya kubanja sana sana nikiamka usingizini akajaribu kunidiscourage lakini nikakaza hadi akanipa ndo nikaondoka zangu.

Wakuu naombeni mniondolee utata hapa. Neno HIV Non Reactive lina maana gani katika HIV testing??

Mbarikiwe zana
 
Non reactive maana yake wametumia kipimo chao kinacho react kama una virusi wa HIV, lakini kipimo chao hakiku react, kwa sababu huna HIV.

Ni kama uchukue litmus paper ambayo hubadilika kuwa yekundu kwenye tindikali na bluu kwenye alkali, ukiiweka kwenye maji yaliyo neutral haibadiliki, hai react.

Kuto react huko ndiyo kuwa "non-reactive", kunaonyesha kile kinachopimwa (tindikali/alkali) hakipo kwa sababu unapima maji neutral.
 
HONGERA SANA kwa kuchukua maamuzi sahihi ya kupima afya yako na ukawa mvumilivu kusubiri majibu
hapo ni kwamba tanzania tuna vipimo viwili tunavyo tumia ktk upimaji hivyo majibu ya kipimo cha bkwanza huwa ni REACTIVE/ NON REACTIVE kwa mtu ambae imeonesha reactive humaanisha ana maambukizi ndipo huwa tunachukua kipimo cha p[l[ ambacho ni CONFIRMATOLY TEST ambacho hicho tunatumia positive /negative .
hivyo wewe kama hukuchukuliwa kipimo kingine kweli hauna maambukizi.
Kuandikiwa hayo majibu kwenye karatasi sijaipenda kwa sababu jiulize ukimwandikia hivyo alie athirika na akakidondosha na watu wakiwa wamemuona inakuwaje. hapo hakuna usiri kwa mteja.
kwa hiyo kweli kaka una non reactive ynye maana hauna maambukizi
 
HIV Non Reactive kwa Maelezo haya nitakayotoa naomba uwe mpole na uyaelewe utaratibu na vizuri.

Tanzania kuhusu upimaji wa HIV huwa tunapima kitu kinaitwa Antibodies za HIV.Antibodies hizi huzalishwa taratibu sana Mara tu MTU anapopata maambukizi ya HIV.

Sasa Katika kipimo chetu cha HIV kama umeshazalisha antibodies za HIV then ukichukua damu ya mgonjwa ukaipima ita React na tunasema ime React Positive kwahiyo majibu huwa ni Reactive.

Sasa unaweza kuwa umepata HIV lakini mwili bado haujatengeneza antibodies za HIV yaani iko ktk kipindi cha Window Period..Hapa ukipima damu ya mgonjwa majibu yatakuwa Non Reactive lakini HIV unayo mpaka hapo utakapo tengeneza antibodies za HIV

Kwa wale ambao antibodies za HIV zimeshatengenezwa huyu akipimwa tu damu yake it's react na majibu yatakuwa Reactive.
 
HIV Non Reactive kwa Maelezo haya nitakayotoa naomba uwe mpole na uyaelewe utaratibu na vizuri.

Tanzania kuhusu upimaji wa HIV huwa tunapima kitu kinaitwa Antibodies za HIV.Antibodies hizi huzalishwa taratibu sana Mara tu MTU anapopata maambukizi ya HIV.

Sasa Katika kipimo chetu cha HIV kama umeshazalisha antibodies za HIV then ukichukua damu ya mgonjwa ukaipima ita React na tunasema ime React Positive kwahiyo majibu huwa ni Reactive.

Sasa unaweza kuwa umepata HIV lakini mwili bado haujatengeneza antibodies za HIV yaani iko ktk kipindi cha Window Period..Hapa ukipima damu ya mgonjwa majibu yatakuwa Non Reactive lakini HIV unayo mpaka hapo utakapo tengeneza antibodies za HIV

Kwa wale ambao antibodies za HIV zimeshatengenezwa huyu akipimwa tu damu yake it's react na majibu yatakuwa Reactive.

Antibodies- Kingamwili

Kwahiyo kuna kingamwili dhidi ya HIV pekee na kingamwili ya mwili mzima ?
 
Wakuu,ninaomba ufafanuzi wa hilo neno ANTIBODIES kwa Kiswahili maana ndiyo Lugha watumiao Watanzania wengi.
Je hii Antibodies kila mtu anayo kiasili kwenye mwili wake?

Mi sjui jina lake la kiswahili.Ila antibodies kila mtu anazo na zinatumika katika kukinga mwili.mfano wakiingia bacteria flani mwilini mwako, antibodies maalumu kwa hao bacteria wanatengenezwa na hizi seli zinaitwa plasma cells(au B cells).Hawa antibodies wanafanya kazi nyingi muhimu kwa mfano,waki bind,yani 'waki ungana' na hao bacteria,wanasababisha seli maalumu za kulinda mwili mfano phagocytes,kuja 'kumla' yule bacteria.
Kwa hiyo HIV virus na yy akiingia..kuna antibodies zitatengenezwa maalumu kwa ajili yake.Virus anaweza akawepo mwilini lakini bado hao antibodies hawajatengenezwa.Yaani huyu virus anaweza akasambaa mwilini bila mwili wako kujua(yani kuproduce antibodies).
Kwa hiyo hawa antibodies wa ukimwi wakija kutengenezwa,ukienda kupima,hao antibodies maalumu kwa ukimwi Wata react na hicho kipimo.Kwa hiyo utakuwa HIV positive.Non reactive itamaanisha hao Antibodies hawajatengenezwa.Kwa hiyo kuna mawili.HIV hayupo kabisa(HIV Negative) au bado mwili haujajua Kama yupo.Ndomaana inakubidi ukapime tena baada ya miezi kadhaa.

Ila ndo hivyo huyu virus Ana mechanism ambayo ataathiri seli zako muhimu za kinga Kama CD4 tcells.Hawa CD4 tcells ndo wanasaidia mwili kujua kama una ukimwi au magonjwa mengine.Hawa sasa ndo wanaathiriwa.Hivyo utakuwa immune compromised(kinga ndogo).Ndo Maana muathirika ataanza kuugua magonjwa mengi ambayo mwili ungeweza kupambana bila uhitaji wa dawa.
 
Back
Top Bottom