Msaada haraka

Msaada haraka

DIKACY

Member
Joined
Oct 7, 2013
Posts
23
Reaction score
7
Nimeolewa nina mtoto,

Mume wangu kachepuka kampa mchepuko mimba,sasa kachanganyikiwa aishi na nani,kaanza kufunga na kusali ili Mungu amuonyeshe nani mke wake,kaenda Malawi kwa mchungaji Mmoja anaitwa Bushiri akamtabiria aachane na mke wa ndoa aende kwa mchepuko,

Sasa hivi hapashikiki, jamaa anataka kunipa talaka ili aoe mchepuko.

Ushauri jamani.
 
Ondoka tu kwa kuachwa sio mwisho wa maisha
 
Nimeolewa nina mtoto,mume wangu kachepuka kampa mchepuko mimba,sasa kachanganyikiwa aishi na nani,kaanza kufunga na kusali ili Mungu amuonyeshe nani mke wake,kaenda Malawi kwa mchungaji Mmoja anaitwa Bushiri akamtabiria aachane na mke wa ndoa aende kwa mchepuko, salsa hivi hapashikiki, jamaa anataka kunipa talaka ili aoe mchepuko,ushauri jamani.
wewe ni mke wa Ndoa?na ndoa gani?hebu tujibu haya maswali tukupe ushauri
 
Wewe hujaolewa ili ulipingwa mimba na ukawa promised kuwa utaolewa. Katika mizunguko yake jamaa amepata kifaa zaidi yako ndio maana anaweka hiyo mikakati ya kukumwaga kimtindo ili awe huru na usimsumbue sumbue.

USHAURI:

Ndoa hailazimishwi...kaa pembeni, muache aoe amtakaye. Wewe aliyekupangia Mungu kuolewa naye yupo...njiani anakuja wala usikate tamaa dada yangu. Pia huwezi jua mungu anakuepusha na nini hapo..kaa pembeni bidada usilazimishe.
 
  • Thanks
Reactions: Luv
Huyo ni mchungaji au anti baraka?

Mbona uchungajini nako kumekuwa na sanaa kama bongo movie aisee?
 
Nimeolewa nina mtoto,mume wangu kachepuka kampa mchepuko mimba,sasa kachanganyikiwa aishi na nani,kaanza kufunga na kusali ili Mungu amuonyeshe nani mke wake,kaenda Malawi kwa mchungaji Mmoja anaitwa Bushiri akamtabiria aachane na mke wa ndoa aende kwa mchepuko, salsa hivi hapashikiki, jamaa anataka kunipa talaka ili aoe mchepuko,ushauri jamani.
Unauhakika na jina la huyo mchungaji? jina lake halianzii na herufi G kweli?
Anaendesha gari la kimarekani?
 
Nimeolewa nina mtoto,mume wangu kachepuka kampa mchepuko mimba,sasa kachanganyikiwa aishi na nani,kaanza kufunga na kusali ili Mungu amuonyeshe nani mke wake,kaenda Malawi kwa mchungaji Mmoja anaitwa Bushiri akamtabiria aachane na mke wa ndoa aende kwa mchepuko, salsa hivi hapashikiki, jamaa anataka kunipa talaka ili aoe mchepuko,ushauri jamani.
Haya makanisa huwa yana wapotosha sana.
Kwanza kwa ulivyo andika inaelekea hilo kanisa swala la kuchepuka ni ruksa.

Hakika mna mambo nyie wana makanisa na kwa ulicho kiandika kila kanisa lina Mungu wake.
Hivi kwanini huyo Mungu wake akumuonesha ili hasikuoe?Hivi kwa nini huyo Mungu wake hakumuonesha huo Mchepuko kabla yako ili auoe?

Usijali hapo hakuna talaka atasumbuka sana kama mlifunga ndoa kwenye makanisa haya ya kawaida.

Hakuna kanisa lililo tayari kuvunja ndoa bali kuirejesha,kama anadhani alikuoa kimakosa basi ni kosa ambalo atalijutia sana.

Pole sana,Mumeo hakupendi.
 
mchungaji anakushauri uache njia kuu upite kwa mchepuko!
huyo c mchungaji wa kondoo wa bwana, huyo atakuwa mchungaj wa mbuzi.
 
Mpe kheri, aendelee. Subiria divorce mkubaliane kulea watoto.

ndoa haishikiliwi na plasta
 
Kubaliana na anachotaka. Usilazimishe mapenzi. Atakukumbuka.
 
hakuna kuachwa mtu hapa km una ndoa kamili kanisani na cheti kasain mke moja hiyo imekula kwake km vip akutunze na mtt wako mpk mwisho wa safar
 
Ndoa ya kanisani Roman Catholic

kama ni ndoa ya kanisani hawez kukupa talaka, atakupa kwa vigezo vipi? mchungaji gani huyo atakayetabiri amuache mke wake wa ndoa?huyo hawez kuwa mchungaji labda unadanganywa na mumeo au huyo ni mganga wa kienyeji.
Lakini dada kama una kazi yako ni jukumu lako kuondoka na kuanza maisha yako wewe mwenyewe na mwanao, maana akufukuzaye sio lazima akuambie TOKA... angalia maisha yako na ya mwanao, yeye muache aendeleze michepuko yake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom