Msaada haraka

Msaada haraka

Mapenzi hayalazimishwi angekuwa anakupenda asingechepuka,wewe chukua chako mapema.
 
yaani ukishaona hvyo ujue huyo hana akili............achana nae huyo, hajielewi.......yaani mwanaume akikosa msimamo haafaai haaafai atakutia mashaka tu ya moyo. kwanza sitashangaa baada ya muda atakwambia kaambiwa tena amrejee mke wake wa ndoa.....kesho atakupa stori nyingine ya mchepuko mwingine.hana maana huyo
 
Yanini kumng'ang'ania mtu ambaye hana mapenzi tena na wewe mwache aende! mama lea watoto wako Mungu atakuwezesha .akipata fundisho huko ata rudi anatembelea magoti !
 
Mmmh ndiyo mana kuna mtu alisema hapa hawa wanaume wanalishwa vitu vichafu huko kwa michepuko hawasikii!!
 
Usiondoke kwenye ndoa yako kirahis, funga ,sali kwa iman yako na kuwa mvumilivu katika kipind hiki kigumu .katika maombi yako muombe mungu akionyeshe lipi jambo sahihi .kuachana na Mume wako au kuendelea na ndoa yako .usichukue maamuz kama wewe inawezekana mumeo kalogwa na hakuna wa kumuokoa zaid yako na njia ya kumuokoa ni kumuomba mungu.najua una wakat mgumu ila hutakiw kukurupuka katika maamuz .mwanamke mjinga anaivunja ndoa yake mwenyewe
 
DIKACY yaani wewendo mke? yaliyokukuta unasimulia kama hekaya hata uchungu huna
 
Last edited by a moderator:
DIKACY yaani wewendo mke? yaliyokukuta unasimulia kama hekaya hata uchungu huna

watu wengine au wengi wanaandika kwa style ya ku- hide identity yao, kumbuka mwingine unamuanzishia thread na yeye yupo humu humi. kwahiyo kuna trick namna ya uandishi wa true sensitive story.
 
Last edited by a moderator:
kweli hapa pagumu,ni vizuri kumuacha aendelee na mambo yake na wewe uende na maisha yako,hata akiwa tayari kumgharamikia mtoto,vipi kuhusu tendo la ndoa kwako?yeye atakuwa na mchepuko wake,wewe utakuwa na nani coz ukilala na mwanaume mwingine utakuwa unazini maana huyo ni mumeo hadi kifo kitakapo watenganisha
 
Kama ulivyoambiwa mrahisishie maamuzi kubali talaka sepa kaanze maisha mapya kuachika sio mwisho wa maisha kama amelogwa mwache akalogwe zaidi bt kabla hujaachana nae anzia kanisani kwa paroko ili usije ukabeba lawama baadae huwezi jua kesho ikoje,kikubwa tambua unaweza ukaforce ndoa lakini sio furaha ya kweli ambayo inatokana na mapenzi ya dhati
 
Ndoa ya kanisani Roman Catholic

Muombe nawe Mungu wako huko shetani alikomuiba amrudishe,mkumbushe Mungu mema uliyomtendea,mkumbushe Mungu ahadi na agano mlilowekeana na mume wako,lia na Mungu wako,usishindane naye kimwili wala huna haja ya kupigana naye makelele shindana naye kiroho,pigana na shetani aliyemuiba mume wako,hakika Mungu ni mwaminifu atarudi tu.
 
Umeanza kwa kusema, '..umeolewa na una mtoto...' kisha 'ndoa ni ya kikatoliki'.. kisha. 'mume kaenda kwenye maombi ili afunuliwe kati yako na mchepuko nani mke wa kuishi nae'..

Naona kama kuna mkanganyiko fulani. Nyote ni waumini wakatoliki (kama ni kweli ndoa yenu ya kikatoliki). Kwa imani hiyo kuna nukuu wakati wa ndoa 'mume atawaacha baba na mama yake na kuambatana na mkewe.. nao watakuwa mwili mmoja...' kisha kuna nukuu... 'alichofunga Mungu mwanadamu asikitenganishe'. Pia kuna kiapo cha ndoa cha kuvumiliana kwa shida na raha mpaka kifo kiwatenganishe.

Kwa nukuu za torati mtu hatamwacha mkewe isipokuwa kwa zinaa/uzinzi, etc.etc. Na hata inapothibitika kuwa mwenzi ni Mzinzi huchukua muda mrefu sana kwa kanisa katoliki kuridhia ndoa kuvunjwa.

kwa mapokeo ya mafundisho ya kikatoliki ukioa au kuolewa nyie hamtenganishwi. Kutengua ndoa ya kikatoliki ni process ndefu sana sana. Rejea mafundisho ya ndoa.

Bottom line: usiwe chanzo cha kuleta ufarakano katika ndoa, jichunguze kwa nini imefikia mumeo kuwa na mchepuko, jitihada gani umefanya kumrudisha mumeo katika mstari wa ndoa. Kama una uhakika wa zinaa/uzinzi na hauko tayari kujadili/suluhisha. We all err. Hata wewe katika hali yako ya udhaifu wa kibinadamu unaweza kuteleza.

Fikiria maisha ya mwanao pia. Kama unaweza kurudisha imani ya mmeo katika ndoa, ningeshauri ufanye kila liwezekanalo katika imani uokoe pia furaha ya mwanenu.

All the best, my sister.

PP
 
Nimeolewa nina mtoto,

Mume wangu kachepuka kampa mchepuko mimba,sasa kachanganyikiwa aishi na nani,kaanza kufunga na kusali ili Mungu amuonyeshe nani mke wake,kaenda Malawi kwa mchungaji Mmoja anaitwa Bushiri akamtabiria aachane na mke wa ndoa aende kwa mchepuko,

Sasa hivi hapashikiki, jamaa anataka kunipa talaka ili aoe mchepuko.

Ushauri jamani.

Ushauri gan hapo upewe? Hapo huyo mwanaume hakupendi, ndo maana anatafuta na msaada wa kuambiwa yupi mke bora kwake wakati chaguo ni lake,Wewe Ondoka achana nae na huyo anayeona ndo alistahili kuwa mke wake.,My dear maisha ni mafupi sana na hamna mengine zaidi ya haya so ishi kwa furaha, pigania maisha yako na mwanao muishi vizuri, yaan hapo hamna Mwanaume kabisaaaa, hata akijiweka kwako tayar anaonekana hajielewi flani na atakupa matatizo mengne bure hata kulogwa na huyo mchepuko ukafa ukaacha mwanao, Be happy huwezi jua Mungu kakuepushia nini kwa huyo mume..
 
ndoa hupangwa na mungu

,jiweke tayari kwa lolote,

ulipaswa kabla ya kuzaa nae mfunge ndoa,

ila huwezi jua mungu kakuepushia nini.
wewe pia unaae Mungu,mwombe utafanikiwa tu.
 
ndoa hupangwa na mungu

,jiweke tayari kwa lolote,

ulipaswa kabla ya kuzaa nae mfunge ndoa,

ila huwezi jua mungu kakuepushia nini.
wewe pia unaae Mungu,mwombe utafanikiwa tu.
Asanteni sana kwa ushauri wenu,naomba wengine msome mada muielewe vizuri kabla ya kujibu chochote.
 
Huyo mwanaume hana akili.....

Ila hakuna cha mchungaji wala nini hakutaki tu na umalaya wake

Swali la nyongeza huyo ni mumeo wa ndoa???
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom