Nimesikitishwa sana na kilichonikuta.
Mnamo mwezi wa tano mwaka huu nilijikunjua nikalinunua godoro super banco 6x6 inch 6 kwa Tshs. 220,000/= na muuzaji akanishawishi kuwa super banco ndiyo bora kwa sasa, nikalichukua ila tangu mwanzo likawa linabonyea na kutengeneza mashimo nikajua ndiyo mtindo wake ila kadili siku zilivyosogea likawa mtumbwi katikati, baada ya miezi 6 nimerudi kutoa taarifa kwa muuzaji ananambia muda umepita sana ilibidi nitoe taarifa ndani ya miezi mitatu na sikutakiwa kuwa nimechana karatasi la juu wala nembo, mambo ambayo hakunieleza wakati nalinunua lile godoro, nikamwambia kuwa natambua kuwa sio kosa lake bali ni kosa la kiwanda hivyo wanisaidie mawasiliano ya moja kwa moja na kiwanda ila wamegoma wanadai wao watawasiliana nao ila dalili ni kwamba wananikwepa.
Kusema kweli inaniuma sana na tatizo sio pesa tu ila nasikitishwa na utapeli tunaofanyiwa na hivi viwanda vya magodoro kwa kushirikiana na shirika la viwango Tanzania tbs, inakuwaje watuaminishe kuwa bidhaa ni bora wakati zina matatizo!?
Mwanzo nilidhani labda kama ilivyo jambo la kawaida labda walikosea kwa baadhi ya magodoro katika kutengeneza na hivyo wanaweza kuchukua hatua ya kukufidia kwa mapungufu ambayo ni bahati mbaya ila baada ya kupitia maoni yenu inaonesha ndiyo ubora wa magodoro ya super banco hata nikifidiwa nitaletewa aina ileile.
Nilikuwa na mpango wa kukiandikia kiwanda kukilalamikia na nakala nitume kwa tbs ili wanipatie bidhaa iliyo bora.
Ikionekana hawawezi basi na mimi nitumie namna yoyote kuuhabarisha umma wa watanzania kuwa super banco sio magodoro ya kutoa pesa yako kununu.
Naomba ushauri nifanye nini?
Tanfoam mwisho wa matatizoHayo majuto ninayo mm pia, yn ukiamka asubui kama umepigwa na fimbo mwili mzima unauma, nataka kununua baba lao Tanfoam haya makampuni mengine uchwara tu
Yapo but uwe makini wanafake, jitahidi upate toka ArushaDar yapo haya?
Uko sahihiWala usibabaike....Jikamatie Tanfoam
Dodoma nalo ni uchafu, nunua Tanfoammwenzio anakwambia hilo ndo limemuamsha mifupa inauma saaasa una mrudisha hukohuko.
bora magodoro ya dodoma.
Inategemea kimo, ikiwa ana umbo la wanefili wala sio tatizoDuuh kg 95:95 au 100:90 si mchezo mzee zingatia mazoezi mkuu hiyo ni hatari kwa afya yako.
sipati picha wanajisikiaje wenye bidhaa kwa kauli hiyo.Dodoma nalo ni uchafu, nunua Tanfoam
Bora wajisikie vibaya, hili godoro ndani ya mwaka unalalia chagasipati picha wanajisikiaje wenye bidhaa kwa kauli hiyo.
TanfoamTan form
Nimenunua godoro si zaidi ya miezi minne iliyopita la banco , lile la size ya mwisho. Niliamini Super banco ni zuri na wametoa guarantee ya mwaka. Lakini, sasa hivi ni chanzo cha kuamka shingo au mwili unauma kwani , godoro linabonyea chini.
Naomba uzoefu wa magodoro mengine, au ni spring mattress tu??
Quality foam magodoro DodomaNimesikitishwa sana na kilichonikuta.
Mnamo mwezi wa tano mwaka huu nilijikunjua nikalinunua godoro super banco 6x6 inch 6 kwa Tshs. 220,000/= na muuzaji akanishawishi kuwa super banco ndiyo bora kwa sasa, nikalichukua ila tangu mwanzo likawa linabonyea na kutengeneza mashimo nikajua ndiyo mtindo wake ila kadili siku zilivyosogea likawa mtumbwi katikati, baada ya miezi 6 nimerudi kutoa taarifa kwa muuzaji ananambia muda umepita sana ilibidi nitoe taarifa ndani ya miezi mitatu na sikutakiwa kuwa nimechana karatasi la juu wala nembo, mambo ambayo hakunieleza wakati nalinunua lile godoro, nikamwambia kuwa natambua kuwa sio kosa lake bali ni kosa la kiwanda hivyo wanisaidie mawasiliano ya moja kwa moja na kiwanda ila wamegoma wanadai wao watawasiliana nao ila dalili ni kwamba wananikwepa.
Kusema kweli inaniuma sana na tatizo sio pesa tu ila nasikitishwa na utapeli tunaofanyiwa na hivi viwanda vya magodoro kwa kushirikiana na shirika la viwango Tanzania tbs, inakuwaje watuaminishe kuwa bidhaa ni bora wakati zina matatizo!?
Mwanzo nilidhani labda kama ilivyo jambo la kawaida labda walikosea kwa baadhi ya magodoro katika kutengeneza na hivyo wanaweza kuchukua hatua ya kukufidia kwa mapungufu ambayo ni bahati mbaya ila baada ya kupitia maoni yenu inaonesha ndiyo ubora wa magodoro ya super banco hata nikifidiwa nitaletewa aina ileile.
Nilikuwa na mpango wa kukiandikia kiwanda kukilalamikia na nakala nitume kwa tbs ili wanipatie bidhaa iliyo bora.
Ikionekana hawawezi basi na mimi nitumie namna yoyote kuuhabarisha umma wa watanzania kuwa super banco sio magodoro ya kutoa pesa yako kununu.
Naomba ushauri nifanye nini?
Duuh kg 95:95 au 100:90 si mchezo mzee zingatia mazoezi mkuu hiyo ni hatari kwa afya yako.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] hili nalo nenoMsiangalie upande mmoja,awaambie anakaa maeneo gani.
Huyu itakuwa siku ya kununua Wanga wa mtaani walimuona na mtaani kwao wanga wengi.
Sasa ikifka usiku wanamuwekea mkeka na waanga wao wanachukua Godoro wanalali kwa raha zao,ikifika asubuhi wanamrejeshea.Lazima mgongo uume