Msaada;gari yangu ina shida ya spidi

Msaada;gari yangu ina shida ya spidi

Linatumia Petrol


Mkuu

Mleta mada akija kujibu haya uliyouliza tutapata pia kuanzia pia kwasasa huwezi sema gari hilo ni mbovu maana unapopanda mlima kuna mambo

Kadhaa ya kuangalia hasa aina ya njia pia km ni
Auto hujibadili yenyewe sasa huenda labda kwa
kutokujua magari yanapokupita unahisi ni tatizo
 
Pamoja na majibu mazuri na mengine ya ovyo ovyo, naona swali hilo hapa hutapata ufumbuzi. Kuna msemo unaosema "miluzi mingi hupoteza mbwa", na wewe utapotezwa nawachangiaji. Nakushauri peleka gari lako gereji, ulizia gereji inayoaminika watachunguza tatizo na kukupa ushauri ikiwa ni pamoja na gharama.

Au umeleta fumbo kwamba umepata demu/buzi halafu jongoo halipandi mtungi??
 

Attachments

  • 1390299235843.jpg
    1390299235843.jpg
    99 KB · Views: 179
Weka wazi....kama mlima ni mkali na gari ni auto unataka ibadili gia isiyoendana nayo? Hata Manual ukiweka 3 itakugomea...weka wazi size ya mlima na aina ya gari kama wanavyouliza wadau

Mlima kasema ni ule kutoka njia panda ya Kitunda unapopanda kuelekea gereza la Ukonga. Kwa kweli ule mlima ni mdogo, kama nilivyokuelewa, kajaribu kubadilisha Hydraulic fluid. Lakini tafuta wataalam wa magari. Hiyo niliyokuambia ni preliminary test tu.
 
Habari za kwenu,katika mihangaiko ya hapa na pale,Mungu kanijalia kupata gari.lakini kuna tatizo limeanza jitokeza ambapo ukiwa katika mlima kuupanda inatembelea spidi 40 na hapo umekanyaga mafuta hadi mwisho.naombeni mwenye ufahamu na tatizo hilo anisaidie.
Gari ni auto,na ni suzuki escudo.mlima wa kawaida tu kama wa airport dar kuelekea magereza(ukonga).nakanyaga hadi spidi ya mwisho mafuta lakini spidi ni 40 tena kwa shida sana.ni petrol

Mkuu wamekuuzia kimeo, niliona tangazo lako ukihitaji gari, ipeleke gereji mkuu.. By the way mtoto na mama yake hawajambo??
 
Minadhani tatizo unalipata kwenye speed tu hivyo inaashiria kwamba engine inafanya kazi vema kabisa. Kwa maoni yangu tatizo ni umeme wa gari (kwenye gearbox only): Labda: (1) Control unit ya gear box hapo vizuri na kama ndivyo suluhisho ni kubadilishwa, (2) circuit ya umeme esp switches zilizoko ndani ya gearbox labda kuna iliyo kufa hivyo hupati higher gears, (3) Fuses etc

Mtihani ulionao kama ubashiri wangu upo sahihi ni kwamba mafundi waliowengi ni vibaka tu hawajui umeme wa magari, hasa kariakoo/uhuru/sharimoyo, wanagusagusa kubahatisha wala hawaelewi lolote ila talalila ni nyingi mno. Jaribu kutafuta fundi aliye makini na pia mtaaluma wa umeme wa magari
 
gari kuwa na speed ndogo= kukosa nguvu
1. cooling system- angalia kama inakimbia muda mrefu joto la injini ninapanda? kama linapanda sana then ina maana injini ina mushkeli haiwezi kuwa na nguvu hasa milimani
2. Feul syatem- hasa carburation - wakati mwingine kuna baadhi ya jet zimeziba kwa hiyo kama inatakiwa ifunguke yote kuioa injini nguvu hewa ama mafuta yabakuwa hayaensi yote , kwa hiyo gari haiwezi kuwa na nguvu
3. je mlimani moshhi unaotoka ni rangi gani? maana inawezekana tayari piston rings zimeanza kuisha ( wear) kwa hiyo compression inakuwa ndogo sana hivyo kuikosesha nguvu gari.
4. angalia hata fuel pump na fule filter sometimes zinakuwa na uchafu hivyo kutoruhusu mafuta kwenda mengi na hivyo injini kuwa na nguvu kidogo
5. angalia hata breaking syatem wakati mwingine kuna kujam ikaonekana gari haina nguvu,

Sasa nini cha kkufanya
nenda kwa fundi mwenye vipimo vya diagnosis apime compression pressure kudetermine kama ni issue ya pistion ringa am kitu kingine
Lakini la msingi fanyia gari lako service kwelikweli, clean and check kila kitu.

Ubarikiwe sana
 
Ukitoka Isoko pale hosiptali unakwenda Ktengele kuna mlima unaitwa kashima ni mlima una akili sana gia sahihi pale ni 0.6

ule mlima pale katengele ukishuka nao unaiona kabisa gari ilivyo inama aisee....... Mwambieni yule mkandarasi wenu aupunguze ye kazi yake ni kupaki magreda yake na vibrator roller sijui yamekufa? Wakati bado ujenzi unaendelea
 
Mkuu GREAT VISIONAIRE nakushauri badili gear box. kwani tatizo liko hapo mkuu.Ukiwapa mafundi wataichokonoa na bado haitarudi nguvu. Hilo ni tatizo la kawaida kwa automatic gear. Na kwa ufumbuzi zaidi nunua manual, zile huwa hazizingui hovyo na pia zinachokonyoleka na mafundi wetu wa kibongo ,na pia bei ni cheap sana ukilinganisha na hiyo uliyo nayo. Yaani auto gearbox ya escudo inauzwa laki 9 wakati manual inauzwa laki 3- 4 kariakoo.
 
milima niliyopita;
K9-ngara kama unakwenda burundi
nyaishozi kama unakwenda karagwe
lukumburu songea
mlima wa kwa binti Ndembo kutoka Utwango kwenda Litola
mlima nyoka Mtera Iringa
ludewa ndo balaa
sekenke ya zamani
mlima kolo
CHIWETA --MALAWI... HAPA INABIDI USALI KWANZA THEN UENDE TOILET......
 
Unataka speed hii nenda autobahn, sorry just joking
 

Attachments

  • 1390643113879.jpg
    1390643113879.jpg
    27.6 KB · Views: 102
hahahahahaaaa....... We Mwanyasi hujatulia lol!
nimetulia tulii hapa Barabara ya 13.
Tatizo vijana wanataka speed ya Boeing 777x wakati nguvu ya gari lake ni horsepower 5... lol!

ule mlima pale katengele ukishuka nao unaiona kabisa gari ilivyo inama aisee....... Mwambieni yule mkandarasi wenu aupunguze ye kazi yake ni kupaki magreda yake na vibrator roller sijui yamekufa? Wakati bado ujenzi unaendelea

Kwataarifa yako watu wanatembea kutoka Ikuti mpaka Isoko/Katengele kwa mguu
 
Back
Top Bottom