Msaada gari imegoma kuwaka ghafla

chilubi

JF-Expert Member
Sep 21, 2011
8,182
6,216
Habari zenu,

Nipo na project yangu kufanya engine conversion ila sasa nimekwama njiani. Nimeweka engine ya 2jzge non vvti kwenye gari, siku za mwanzo, mafundi walifanya wiring na wakajaribu kuiwasha ikakubali fresh.

Kwa vile ilikuwa kuna vitu vyengine kama exhaust nlikuwa sijamaliza modification, nikapanga na mafundi next day waje waendelee ikiwa nimemaliza kuweka exhaust. Walikuja wakapiga moto, mnyama kawaka fresh tu, kapigwa race bila matatizo.

Sasa mafundi wakapanga waje next day kwa ajili ya kumaliza wiring ya kwenye dashboard na mambo mengine ili kila kitu kifanye kazi kama kawaida. Hapa ndio mtihani ukaanza, wakawasha, mnyama ame race kama kwa sekunde 5 ivi, akazima kama vile mtu kazima kwa funguo. Tukajaribu kuwasha tena haikuwaka kabisa na spark zikapotea.

Tukachomoa betri na kurudisha, mnyama akawaka tena, aka rev sekunde zake 5 akazima tena, ukiwasha tena haiwaki mpaka uchomoe betri na inajirudia ivo ivo.

Mafundi wa umeme wakapima pale wakaona CODE 12, inasema ni RPM signal, lakini wamepima wameona RPM signal inapatikana kwenda kwa ECU haina tatizo, wakaanza kuishutumu Distributor.

Nikawaambia nnavojua mie distriutor kama mbovu, gari haiwaki kabisa, iweje hii inawaka kila ukichomoa betri na kurudisha halafu inakata moto? Wao wakashikilia distributor. Nikanunua nyengine used na kuifunga, Afadhali ile ya mwanzo, hii ndio ilikuwa gari haiwaki kabisa ata ufanye nini. Nikairudisha na sikutaka nyengine.

Kila nlipoenda kwenye spare, jamaa nikiwaeleza gari inavofanya wanasema hio sio distributor ila kuna jengine. Nikakumbuka ECU ilikuwa imeunganishwa na immobiliser (lakini mwanzoni iliwaka bila immobiliser na race ikawa inapiga fresh tu) nikasema tuifunge immobiliser labda ECU ime reset na kudai Immo. Kawaida nnavojua mie, kama gari inadai Immobiliser basi itakuja code 99, lakini haikutokea hii code, lakini mimi na watu wa umeme tukaamua kuifunga, ngoma iko pale pale hamna liwalo.

Sasa apa nimekwama. Mwenye ujuzi wa hili suala anisaidie mawazo. CODE 12 Rpm signal circuit
 
1. Angalia kama timing belt ipo kwenye right tooth. Baadhi ya engine zipo very sensitive.

2. Angalia pia Crankshaft position sensor. Sijajua kama hiyo engine mliyoweka inaweza kuwa inatumia hall effect au magnetic(inductive) type sensor. Kwa maana hizo dalili ulizotaja zinafanana 100% na hiyo sensor.
 
1. Angalia kama timing belt ipo kwenye right tooth. Baadhi ya engine zipo very sensitive.
Hili nitacheki na fundi aje acheki timing kama imekaa sawa
2. Angalia pia Crankshaft position sensor. Sijajua kama hiyo engine mliyoweka inaweza kuwa inatumia hall effect au magnetic(inductive) type sensor. Kwa maana hizo dalili ulizotaja zinafanana 100% na hiyo sensor.
Engine ni 2jzge non vvti, nimejaribu kugoogle hizi hazina crankshaft sensor wanasema distributor ndio inafanya kazi ya hio sensor.

Huko google nimekutana na mixed results, wengine wanasema Distributor ibadilishwe, wengine ECU, wengine wamebadilisha vyote ila bado hamna kitu.

Nasubiri fundi apate mda aje tu anichekie hio timing.

Kama kuna vtu vyengine vya kucheki nijuilishe.
Check engine Code nnayopata ni CODE 12 ambayo inasema RPM signal circuit
 
Hili nitacheki na fundi aje acheki timing kama imekaa sawa

Engine ni 2jzge non vvti, nimejaribu kugoogle hizi hazina crankshaft sensor wanasema distributor ndio inafanya kazi ya hio sensor...

Me ninachojua Distributor inafanya kazi ya Camshaft Position Sensor.

2JZGE inakuwa na Crankshaft position sensor ambayo ipo mounted kwenye housing la oil pump. Wameificha kishenzi...
 
Me ninachojua Distributor inafanya kazi ya Camshaft Position Sensor.

2JZGE inakuwa na Crankshaft position sensor ambayo ipo mounted kwenye housing la oil pump. Wameificha kishenzi...
wacha niitafute mana mara hio ndio mzizi wa fitna
 
1. Angalia kama timing belt ipo kwenye right tooth. Baadhi ya engine zipo very sensitive.

2. Angalia pia Crankshaft position sensor. Sijajua kama hiyo engine mliyoweka inaweza kuwa inatumia hall effect au magnetic(inductive) type sensor. Kwa maana hizo dalili ulizotaja zinafanana 100% na hiyo sensor.
Wazo la huyo mdau linaweza kuwa suluhisho
 
Daah! kwanza umenifurahisha sana.. hata mimi nina car project yangu nataka kuianza mwezi ujao.... nimenunua body moja ya pickup single cab.. ila ina engine ya RWD, L18nataka kufumua kila kitu niisuke.. niweke FWD... nafikiria 5A ya toyota.. anyways turudi kwako.. hio ni purely issue ya wiring.. mfano.. anza na huo ufunguo unaotumia kuwasha gari.

Niliwahi kuwa na gari ambalo funguo zake zina sensor. Ukitumia funguo tofauti.. litawaka.. ila baada ya sekunde kadhaa linazima, baada ya kufanya wiring zote ndo tatizo lako limeanza which probably means fundi kaunganisha na ile sensor pia.

Jaribu kufanya basic wiring ile inayohitaji tu gari kuwaka halafu uone.
 
1. Angalia kama timing belt ipo kwenye right tooth. Baadhi ya engine zipo very sensitive.

2. Angalia pia Crankshaft position sensor. Sijajua kama hiyo engine mliyoweka inaweza kuwa inatumia hall effect au magnetic(inductive) type sensor. Kwa maana hizo dalili ulizotaja zinafanana 100% na hiyo sensor.
Timing belt ikiwa kwenye jino tofauti gari inakua inapiga tu ila haiwaki...

... huyu kasema anapiga inawaka kabisa na resi anakanyaga then inazima baada ya sekunde chache.. timing ingekua mbaya.. asingefika huko kwenye kukanyaga resi.
 
Kichuguu aje kutupa mawili matatu.
Kwa vile haya ni matokeo ya modification, P0012 inaweza kuwa na maana kuwa wafungaji wa injini hiyo ya modification hawakukaza baadhi ya bolts sawasawa. Kwenye Injini kila bolt ina torque inayotakiwa ndiyo maana wakati wa ufungaji lazima uhakikishe unatumia Torque wrench pamoja na kujua namba za kila bolt.

Sasa makosa hayo yanaweza kuwa yamesababisha camshaft timing gear haikukazwa sawasawa na sasa inehama au inepanua key way. Hilo ndilo kosa kubwa ninalooana, ila pia inawezekana crank position sensor imelegea kwa hivyo haisomi sawasawa.

P0012 ina mambo mengi sana ila kwa namna kosa lilivyotokea, mimi ninadhani ni kulegea kwa timing gear kwenye camshaft tu. Unapoanza inakuwa na timing sawasawa, ila ukiachia mafuta, ile backlash inahamisha hiyo timing na kuzimisha injini kabisa
 
Daah... kwanza umenifurahisha sana.. hata mimi nina car project yangu nataka kuianza mwezi ujao.... nimenunua body moja ya pickup single cab.. ila ina engine ya RWD, L18nataka kufumua kila kitu niisuke.. niweke FWD... nafikiria 5A ya toyota.. anyways turudi kwako.. hio ni purely issue ya wiring.. mfano.. anza na huo ufunguo unaotumia kuwasha gari...
Kila la kheri kwenye project yako Mkuu

Hata mimi nina wasi wasi mzima na hii sensor ya funguo. Huenda ndo chanzo cha engine kukata moto. Kwa sababu ukichomoa betri na kurudisha ukipiga nawaka halafu inakata baada ya sekunde ata 5 hazifiki naona tena inakata kama vile mtu amezima kwenye switch.

Nimeitisha fundi aje atizame kwanza Timing, ikiwa kila kitu sawa naurdi hapo kwenye sensor.
 
Kwa vile haya ni matokeo ya modification, P0012 inaweza kuwa na maana kuwa wafungaji wa injini hiyo ya modification hawakukaza baadhi ya bolts sawasawa. Kwenye Injini kila bolt ina torque inayotakiwa ndiyo maana wakati wa ufungaji lazima uhakikishe unatumia Torque wrench pamoja na kujua namba za kila bolt...
Hii engine nimeitoa kwenye gari, na humo ilikuwa inatembea fresh tu, only one time niliivutia ikakata moto hafla ila nlipowasha ikakubali apo apo. So engine kama engine yenyewe haijafunguliwa kitu zaidi ya kuondolewa Air intake, disconnected from gearbox, na kutiwa kwenye bodi nyengine tu na kurudishiwa.

Hapo mwanzoni, iliwashwa ilikuwa fresh tu. Baada ya siku chache ndio haya yakajitokeza.

p0012 ni mambo za vvti io, hii 2jzge sio VVTi ni kavu. na code inayokuja ni 12 (obd1 hii ECU) ambayo inasema RPM signal Circuit.

Nimejaribu kuuliza camshaft sensor, kazi hio inafanywa na distributor.
 
Hii engine nimeitoa kwenye gari, na humo ilikuwa inatembea fresh tu, only one time niliivutia ikakata moto hafla ila nlipowasha ikakubali apo apo. So engine kama engine yenyewe haijafunguliwa kitu zaidi ya kuondolewa Air intake, disconnected from gearbox, na kutiwa kwenye bodi nyengine tu na kurudishiwa....
Kama hawaku-temper na timing, na unasema injini yako siyo VVT-i, nadhani ni engine ya kabla ya mwaka 1995. Ndani ya distributor kuna kitu kinahesabu mizunguko ya distributor kwa dakika. Kila design zinatofautiana, na design rahisi sana ni switch ya kawaida tu ambapo kila distributor ikizuzunguka mara moja inawasha na kuzima ile switch.

Huenda switch hiyo ina masizi mengi kiasi kuwa haiunganishi umeme tena sawasawa. Distributor nyingine zina pickup coil kama ya kwenye radio cassete ambayo pia inakuwa inagenerate pulses kwa kila mzunguko mmoja wa distributor; inawezekana waya za pickup coil hiyo zimelegea kwa kutu.
 
Kama hawaku-temper na timing, na unasema injini yako siyo VVT-i, nadhani ni engine ya kabla ya mwaka 1995. Ndani ya distributor kuna kitu kinahesabu mizunguko ya distributor kwa dakika. Kila designe zinatofautiana, na design rahisi sana ni switch ya kawaida tui ambpo kila distributor izkuzunguka mara moja inawasha na kuzima ile switch.

Huenda switchi hiyo ina masizi mengi kiasi kuwa haiunganishi umeme tena sawasawa. Distributor nyingine zina pickup coild kama ya kwenye radio cassete ambyo pia inakuwa inagenerate pusles kwa kila mzunguko mmoja wa distributor; inawezekana waya za pickup coil hiyo zimelegea kwa kutu.

JITU LA MIRABA MINNE

hivi ndivo inavofanya
 

Mkuu mimi bado nastick kwenye CPK/CPS sensor... Na kama haipo basi inatakiwa tujue ni kifaa gani kinachopeleka signal ya RPM kwenye ECU halafu baada ya hapo ikaguliwe signal line, ground na power supply(kama ipo) ya hicho kifaa.

Maana kwa ile code unayopata it seems like ECU haipokei signal yoyote ya RPM.

Next week nakuja Dar kama utakuwa hujapata ufumbuzi naweza kupita niangalie.
 
Mkuu mimi bado nastick kwenye CPK/CPS sensor... Na kama haipo basi inatakiwa tujue ni kifaa gani kinachopeleka signal ya RPM kwenye ECU halafu baada ya hapo ikaguliwe signal line, ground na power supply(kama ipo) ya hicho kifaa.

Maana kwa ile code unayopata it seems like ECU haipokei signal yoyote ya RPM.

Next week nakuja Dar kama utakuwa hujapata ufumbuzi naweza kupita niangalie.
CPS sensor hamna, distributor ndio inafanya kazi ya cps na ndio inapeleka signal ya RPM. Waya zimechekiwa kutpka distributor kwenda kwenye ECU zinaonekana zinapeleka signal.

Kwa jinsi inavowaka halafu kuzima, inaonekana ECU inapokea signal kwa muda mfupi halafu inakata.

Next step hapa natafuta wiring ya 1G kavu na control yake, iungwe na mashine halafu itizamwe, ikiwa haikati moto basi manake ECU yangu itakuwa mbovu nitafute nyengine, ikiwa bado inakata basi Distributor mbovu.
 
CPS sensor hamna, distributor ndio inafanya kazi ya cps na ndio inapeleka signal ya RPM. Waya zimechekiwa kutpka distributor kwenda kwenye ECU zinaonekana zinapeleka signal.

Kwa jinsi inavowaka halafu kuzima, inaonekana ECU inapokea signal kwa muda mfupi halafu inakata.

Next step hapa natafuta wiring ya 1G kavu na control yake, iungwe na mashine halafu itizamwe, ikiwa haikati moto basi manake ECU yangu itakuwa mbovu nitafute nyengine, ikiwa bado inakata basi Distributor mbovu.

Okay mkuu. Nimejaribu kupitia hapa wanasema Distributor ambazo zipo advanced zinakuwa na hall pick up au zinakuwa na magnetic swicht kwa ajili ya masuala ya ignition timing. Ni mechanism hiyohiyo ndo inatumika kwenye CPK sensor na speed sensor zingine.

Kwa ninachokiona kama unafikiria kutest Control nyingine na Distributor nyingine basi anzia kwenye distributor.
 

Ngoja baada ya kazi nitkuandikia orodha ya suspects wengine katika injini hiyo, ila inaonekana kama kuna mambo mawili makubwa . (1) Ninaona kama hiyo timing belt yako hata kama haikuguswa ilikuwa tayari imeshapanuka kwa hiyo inapoteza timining ikianza kuwa loaded, au (2) Connectors zako kutoka kwenye ECM kwenye sehemu mbalimbali za gari, mojawapo ina kutu kwa hiyo haiunganishi vizuri waya mmoja;hasa ile ya kutoka kwenye distributor. Jaribu kusafisha ile plug inayotoka kwenye disributor kutumia mafuta yake haya

1594058266451.png
 
Ngoja baada ya kazi nitkuandikia orodha ya suspects wengine katika injini hiyo, ila inaonekana kama kuna mambo mawili makubwa . (1) Ninaona kama hiyo timing belt yako hata kama haikuguswa ilikuwa tayari imeshapanuka kwa hiyo inapoteza timining ikianza kuwa loaded, au (2) Connectors zako kutoka kwenye ECM kwenye sehemu mbalimbali za gari, mojawapo ina kutu kwa hiyo haiunganishi vizuri waya mmoja;hasa ile ya kutoka kwenye distributor. Jaribu kusafisha ile plug inayotoka kwenye disributor kutumia mafuta yake haya

View attachment 1499390
Nasubiri unipe suspects nyingine katika engine mana sasa hii project imeanza kunichukiza

1) timing belt imechekiwa iko powa
2) Fundi umeme amepima kwa tester yake plug ya distributor kwenda kwa ECU ameona kuwa signal ipo na haina interruption yoyote ile (ikiwa engine off apo)

Kwenye hio video nloiweka, baada ya kuzima, tukijaribu kuiwasha tena ndio inagoma mpaka tuchomoe betri, lakini tukijaribu na akipima, anakuta spark na injectors hamna kitu ndio mpaka achomoe betri arudishe.

Hapa tumekuwa na suspect ya ECU, tuliifungua ndani tukakuta resistor moja iliungua, tukaipeleka kwa fundi ikatolewa ikawekwa nyengine, ambayo nayo pia nna wasiwasi ilikuwa mbovu mana ilikuwa na alama za kuungua, lakini pia hatuna uhakika kama ameweka resistor iliokuwa sawa na alioitoa, iliotoka iliunguwa ilifutika namba zake kabisa, sasa sijui kama jamaa kwa vile aliona blue akaweka blue yoyote tu ile.
 
Nasubiri unipe suspects nyingine katika engine mana sasa hii project imeanza kunichukiza

1) timing belt imechekiwa iko powa
2) Fundi umeme amepima kwa tester yake plug ya distributor kwenda kwa ECU ameona kuwa signal ipo na haina interruption yoyote ile (ikiwa engine off apo)

Kwenye hio video nloiweka, baada ya kuzima, tukijaribu kuiwasha tena ndio inagoma mpaka tuchomoe betri, lakini tukijaribu na akipima, anakuta spark na injectors hamna kitu ndio mpaka achomoe betri arudishe.

Hapa tumekuwa na suspect ya ECU, tuliifungua ndani tukakuta resistor moja iliungua, tukaipeleka kwa fundi ikatolewa ikawekwa nyengine, ambayo nayo pia nna wasiwasi ilikuwa mbovu mana ilikuwa na alama za kuungua, lakini pia hatuna uhakika kama ameweka resistor iliokuwa sawa na alioitoa, iliotoka iliunguwa ilifutika namba zake kabisa, sasa sijui kama jamaa kwa vile aliona blue akaweka blue yoyote tu ile.
ECU huwa hazifi kirahis vile; ila kama mlikuta kuna resistor imeungua, halafu mkaibadilisha hiyo tu, bado itakuwa haifanyi kazi tena kwa vile hamjatafuta sababu iliyofanya hiyo kuungua. Electronic components zina tatizo moja kuwa zinaweza kufa bila kukuonyesha dalili; kwa hiyo kubadilisha resistor moja hakuna maana kuwa components nyingine zote ni nzima. Ningekushauri ubadilisha engine control unit yote kwa zile, kama ilivyo motherboard ya computer, huwa hasifanyiwi matengezo kabisa.

Kwa sasa usitafute ushauri wowote kabla hujabadilisha hiyo ECU. Kama gari yako inatumia OBDI basi itakuwa na computer moja tu, na zinuzwa zinauzwa bei ghali kidogo kuliko zile za OBD II sijui kwa nini
 
Back
Top Bottom