Msaada :Feni ya laptop yangu inapiga kelele

Msaada :Feni ya laptop yangu inapiga kelele

Socw

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2016
Posts
1,385
Reaction score
2,850
Wakuu
Natumia HP elite book 6930p inayotumia windows 8.1
Hivi karibuni nimekuwa nasikia kelele za feni iliyopo upande wa kushoto sawa au karibu na power button. Na kuna wakati nikichomoa ac power adapter kelele zinatoweka lakini nikichomeka tu zinaanza. Na sometimes hata kama sijachomeka power adopter inapiga kelele kwa muda kisha kutulia na inaweza kujirudia tena. Msaada Tafadhali msaada wa kusolve hilo tatizo
 
Embu tafuta blower ipige upepo then uone itakuwaje yawezekana inauchafu.
Ilisha wahi nitokea nikaisolve kwa njia hiyo. Kwa ushauri zaidi wataalam wanakuja.
 
hapo inawezekana ipo hivi.

-ukichomeka power adapter pc inaingia kwenye perfomance mode, clock za cpu zinaongezeka, perfomance inaongezeka, joto linaongezeka feni linawaka kupoza.

-ukitoa adapter pc inakuja kwenye power save au balance mode, clock zinapungua, perfomance inapungua, joto linapungua, feni linazima.

click start kisha search power mode halafu jaribu kuset.

alternative fungua task manager (right click kwenye taskbar kisha chagua task manager) halafu angalia ulaji wa cpu ukoje hilo feni likizunguruka.
 
Hizo ni dalili za feni kuwa na uchafu. Nenda kwa mafundi pc, waisafishe feni hutoamini uchafu utakaouona. Baada ya hapo feni itatulia.
 
Ila usiipige pige laptop makofi hilo eneo la feni kwa kudhani utaifanya isitoe jayo makelele. Kwakufanya hivyo basi, unaiongezea pc matatizo mengine mengi
 
Nmewahi kupata tazo hili mkuu nna tumia hp probook 6360b.
Solution fungua hyo fan then iwekee yale mafuta yake ya kulainisha imekauka so ikzunguka sana inatoa saut km mashine mkuu ilkuwa mwaka jana had leo tatzo ksha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo feni ni chafu mkuu inahitaji kusafishwa tu.

ANGALIZO: ni bora peleka kwa fundi akusafishie kuliko kujifanya unaweza.

[emoji252]You get what you work for not What you wish for [emoji252]
 
Back
Top Bottom