Yimakatso
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 7,829
- 11,420
Habari za muda huu wakuu.Blackberry yangu z3 tangu jana inaniandikia 'SIM NOT DETECTED' sijui tatizo nini?Ilikuwa hivi jana nilipokuwa naingia kiwanda cha cement dangote mtwara simu iliniandikia emergency calls only baadae sim not detected.Wenyeji wa eneo hilo wakaniambia kuna tatizo la network hapo hivyo nikaamini nikitoka eneo hilo network itarudi.Cha kushangaza hata nilipofika Mtwara mjini network haikurudi na hadi sasahivi nipo Dar bado inaniandika SIM NOT DETECTED.Nimebadilisha chip tofauti tofauti hakuna inayosoma.Naombeni msaada wataalamu wa blackberry na smartphone kwa ujumla.NB:Simu ni original.