Msaada: Anataka kuolewa na kupata watoto ila hana bwana

Money Penny

JF-Expert Member
Jun 20, 2016
15,921
14,820
Niaaaaajeeeee!

NAOMBENI mumsaidie huyu mTz halisi mwenzenu ana mateso sana ya moyo

Anatamani KUOLEWA lakini hapati BWANA wa kumuwowaaa...

MTz: Money Penny nahisi kujiua.. marafiki zangu wote wameolewa... woooote wamezaaa. ..woooote wamefunga uzazi wanalea watoto kasoro mimi

Huu ni mwaka wa 14 sina na sijawahi kuwa na boyfriend nilikuwa buzy na shule mpaka PHD nimeipata

Kuja kushtuka nimezama sana kitabuni naambiwa nina ugonjwa wa Fibroids tena za kuondoa haraka na natakiwa kuzaa watoto haraka mana nikiondoa nikakaa bila kuzaa watoto zitarudi tenaaa

Sasa mtu wa kuzaa nae sina wanaume wote umri wangu na wakubwa wote walishaoa wanalea

Nikapita pita kwa marafiki kuuliza jinsi walivyowapata hao waume zao.. kiukweli njia walizotumia zote kwangu zitahitaji grisi la maana doh penny njia zao zote sitaweza

Marafiki zangu wote walipita shortcut njia zifuatazo

1. wengine waliozalishwa wakaolewa...

2. wengine waliolewa walishaikatikia sanaaa...

3. wengine waliolewa walishashusha engine mara 3....

4. wengine waliolewa kwa kwenda kwa waganga....

5. wengine waliolewa baada ya kutoa show zote za kimalaya

6. Wengine waliolewa kwa kuruka sana ukuta (sio ukuta Huu wa nyumba ule ukuta wet. .. kiru!)

7. Wengine walitumia nguvu kuvurga mahusiano ya muda mrefu wakakaa tu hapo na ndoa ilivyofungwa mambo yakawa hayaendi wakaamua kutengana. .. basi tu shogangu alitaka kutoa nuksi ya kuolewa na baada ya miaka 5 kupita kaolewa tena na mzunguuu

doh nikasema hapa Penny sio pangu nikijiangalia mimi michezo ya baba na mama niliiacha form 4 nahisi nipo sealed!

Nafanyaje Penny, nimesoma hadithi zako zooote nimefanya kama ulivyoshauri lakini waaap... Huu mwaka wa 2 natendea kazi ushauri wako lakini darasa nimeshalifeli

Sijui nina gundu maana kanisani Mchungaji ameniombea mpaka mdomo wake ushapindaaa. ..

nimetabiriwa na manabii weee mpaka natamani kuwapiga maweee wale manabii nikiwaona...mwaka 2017 ndio Huu ushaishaaa bado nipo singo

Miaka tu inakatika Penny sina hata wa kuniambia mambo nafanyaje penny nazidi kuchanganyikiwa 2018 naingia 35 gonjwa la fibroid linazidi kupandaaaa naogopa kutolewa kizazi nimeambiwa fibroids zimeota pabaya nisipotoa mwisho wa siku wataondoa kizaziii

Nataka nizae watoto wangu lakini nazaa na nani?

Tatizo langu lingine mimi huwa ni mwogaa... juzi kati hapa nilipewa bwashee wa kipare aniamshie dude nikakimbiaaa naogopaaa tulishapimwa kila kitu kwenda hotel nikakimbiaaa nasingizia tumbo la kuharaaa

Penny nakufa miee si bora tu Yesu achomoze tusepe, haya mateso yangu ni zaidi ya Jehanam ya moto wa milele

Yeleuwiiii wana JF mnamsaidiaje Mzalendo mwenzenuuu....

help me help her abeg abeg! Nahisi nimeishiwa na grisi ghaflaa

Hamna mwaka JF nae anataka kuoa hana beibe nimpe huyu dada

Ps:
Yupo vizuri kifedha jamaa fursa hii

 
Kwahiyo hakuna alomuomba Mungu hata mmoja!! Kweli marafiki zako kiboko.

Ngoja waoaji waje, huenda ukajipatia hitaji la moyo wako.
Una maana hitaji la moyo wake?

Si amekwambia kwa kanisa ameshakwenda kaombewa mpaka Pasta mdomo umepinda?
 
Back
Top Bottom