Msaada: Aliyewahi kufikia hatua hii- Alitokaje?

Msaada: Aliyewahi kufikia hatua hii- Alitokaje?

the-need

Member
Joined
Jan 2, 2014
Posts
56
Reaction score
29
Ndugu wanajf....nimejaribu kila mbinu za kupambana na maisha kasoro kuiba mpaka sasa sijafanikiwa...ndio kwanza naona maisha yanazidi kua magumu sana.


Anything u mention, nimejaribu bila mafanikio. Is like upo kwenye ulingo wa ngumi na unapigana na Mohamed Ally au Cheka. Kila ukirusha ngumi moja...unamiminiwa 30 za haraka haraka tena zenye maumivu mpaka unaanguka huku damu zikikutoka.


Sasa nimeamua kumuomba Mungu tu...naenda kwenye maombezi mbalimbali. Sometimes nafunga na kuomba...

Nimekua mtu wa kushinda ndani tu. Naona giza tu mbele yangu. Nipo lonely sana. Sina kazi wala kitu chochote cha kuniingizia kipato.


Kazi nimetafuta sana bila mafanikio. Biashara nimefanya pia.



Mpaka sasa sijakata tamaa kuomba ajira na kufikiria mbinu za kupata pesa. But nimekua wa kukaa tu sina uelekeo.


Kwa yeyote aliyewahi kua na hali hii...ilikuaje akajikuta anaanza kupata neema?
 
Mkuu nimepitia hicho kipindi, kuna wakati nikashawishiwa na mama mmoja ambaye ni marehemu
kwa sasa niende nchi fulani kufuata mzigo (unga) kwa ahadi ya kitita cha tsh milioni 11, nilikuwa
nakaribia kukubali lakini wakati nikitafakari yule mama akakumbwa na umauti.

Nilitamani kuuza maji barabarani lakini aibu kilikuwa kikwazo kwangu, hatimaye nikapata mbinu
ambayo namshukuru Mungu ilinitoa sana, tena sana. Nilirudi kijijini nikaonana na wataalamu wa
tiba za asili..... naomba unielewe hapa ili kuweka mambo sawa sio waganga wa kienyeji ni wataalamu
wa tiba za asili. Ndiyo.... nikajikuta mpango wangu huo ukiniwezesha kununua kiwanja hapa Dar.. hadi
kufanikiwa kujenga.
Utumie vizuri muda wa asubuhi kwa kutafakari nini cha kufanya..... usichoke kila kitu kinaanzia
kwenye fikra hata ukiiona ghorofa kubwa vipi lazima itakuwa imetoka kwenye fikra za mtu mmoja kwanza
hata kama ni ghorofa ya serikali, jumuiya n.k.
 
Ni jambo jema kumwomba Mungu ila wakati huo huo fikiria biashara ambayo unaweza kuifanya hata kama ni kidogo kiasi gani, usijali Mungu ni mwema
 
pole sana ndugu. kama mchangiaji alivyo comment hapo juu, ni vyema ungeongeza details kama gender ,age, elimu yako na ujuzi ulionao, why uko lonely? je huna ndugu au rafiki wa karibu? ushauri wangu kwa kuanzia unatakiwa ujitoe katika kifungo cha kisaikolojia . naona hata jina umejipa 'the need' ku reflect jinsi akili yako inavyojiona. unaweza kufikiri una shida kuliko watu wote unaowajua kumbe si sahihi. kuna watu wana shida lakini wanajipa moyfo kua ipo siku mambo yatakua ok,hiyo inawapa nguvu ya kupigana na hakika mambo hubadilika. kuna watu wanajiita young millionare, au next billionnare wakati hawana kitu, ila akili yao inawatuma ipo siku itakua kweli. pili jaribu kutumia network uliyonayo ( rafiki, ndugu na majirani) kutafuta msaada. hao wanakujua vizuri zaidi na wanaweza kukutoa
 
Halafu watu wa aina yako wanakujaga kupata mafanikio makubwa sana! kwanza kabisa weka imani yako kwa mungu, pili jaribu kuchunguza back ground yenu kwa maana ya ukoo wenu ki ujumla, maana watu wengi kwenye maisha wanataabika kutokana na mambo ya ukoo km mila, mizimu, visasi na mambo yanayofanana na hayo so background inahusika pia ktk maisha au future ya mtu!
 
Mkuu fursa bado unayo labda iwe hauna kisehemu hata ka nusu eka.
Kama upo town na ulitokea kijijini rudi kijijin weka aibu pemben fursa zipo haswa kwenye kilimo kidogo kidogo kitakupa kick ya kuanzia life ila kama upo town na una kisehemu hata cha robo eka ungana na wengi kwenye kilimo na jembe huwa halimtup mtu.
 
Sijakuelewa we unaesema kuwa ulienda kwa mganga wa tiba za asili, je uliwnda kujifunza kutibu? Fafanua mkuu.
 
Nashukuru kwa majibu yenu. Kuna mmoja kanipa ushauri wa tiba asili. Kiukweli kabisa...siamini upande huo kabisa though niliwahi kwenda kwa wataalam kama 30 hivi tofauti bila mafanikio. Nikaamua kurudi kwa Mungu upya na kutubu. Na nilichukua mwaka mzima kujihusisha na tiba hizo na nilivyoona hazina tija nikaamua kurudi kwa Mungu.


Umri na elimu ni Degree...umri 35years.


Sina kibanda...kiwanja wala pesa ya kusema nitaanzisha biashara.


Kuhusu ndugu....ndugu zangu ni type ile ambayo ikimuona mtu yupo kwenye problems ndio wanafurahia. Ukiwa kwenye furaha wanapretend unafki.
 
Pole sana Mkuu hasa hapo kwenye suala la ndugu kushangilia problems zako. Nakushauri uongee na Headmasters wa shule za private unaweza pata dili ndogo ya kupiga chaki (kufundisha) huku ukiangalia ustaarabu mwingine kuliko kuendelea kujifungia ndani. Hiyo itakukeep bize maana ukikaa sehemu moja lonely halafu una mawazo ya maisha magumu unaweza fika hatua ya kuchukua maamuzi magumu.
 
Ndugu wanajf....nimejaribu kila mbinu za kupambana na maisha kasoro kuiba mpaka sasa sijafanikiwa...ndio kwanza naona maisha yanazidi kua magumu sana.


Anything u mention, nimejaribu bila mafanikio. Is like upo kwenye ulingo wa ngumi na unapigana na Mohamed Ally au Cheka. Kila ukirusha ngumi moja...unamiminiwa 30 za haraka haraka tena zenye maumivu mpaka unaanguka huku damu zikikutoka.


Sasa nimeamua kumuomba Mungu tu...naenda kwenye maombezi mbalimbali. Sometimes nafunga na kuomba...

Nimekua mtu wa kushinda ndani tu. Naona giza tu mbele yangu. Nipo lonely sana. Sina kazi wala kitu chochote cha kuniingizia kipato.


Kazi nimetafuta sana bila mafanikio. Biashara nimefanya pia.



Mpaka sasa sijakata tamaa kuomba ajira na kufikiria mbinu za kupata pesa. But nimekua wa kukaa tu sina uelekeo.


Kwa yeyote aliyewahi kua na hali hii...ilikuaje akajikuta anaanza kupata neema?

pole mkuu!nakufuata kwa PM tuzungumze mawili matatu!
 
Mkuu Pole Saana, Sasa Ni Rahisi, Kwanza Muombe Mungu Kwa Bidii Kwa Imani Yako. Sasa Tembelea Jukwaa La Biashara Na Uchumi. Anza Na Ujasiliamali, Utaonana Na Watu Wanao Fikiri Sawasawa. Kunashuhuda Za Watu Wengi Walio Fanikiwa Kupitia Jukwaa Lile, Hata Mimi Kunabiashara Waga Na Zifanya Kupitia Jukwaa Lile, Pale Utajifunza Kumiliki Biashara Kuuubwa Sana Kwa Mtaji Mdogo Tu! Na Ni Wengi Wamenufaika. Ukimaliza Jukwaa Lile Hamia Jukwaa La Kawaida La Biashara Na Uchumi Kuna Watu Wanao Fikiri Sawasawa Pale, Ningekushauri Upumzike Kwanza Na Utenge Muda Usiku Wa Manane Usome Thread Mbalimbali Katika Majukwaa Haya Nafikiri Utapata Mwanga. Mkumbuke Mungu Kwanza!
 
Dah pole sana ndugu ukizingatia umri ndio unaenda hivo lakini usikate tamaa.Usijifungie ndani jaribu ku share matatizo na watu wenye upeo walio karibu na wewe ipo siku Mungu atakuona.Usijaribu kuiba utaishia mikononi mwa wananchi wenye hasira.
 
Shemeji yangu ni mchungaji. Ni pm ili nikuelekeze jinsi gani uongee naye maana wengi wamefanikiwa kwa huduma yake na Mungu amewapandisha kwa viwango vingine. Amini utashinda
 
Nashukuru kwa majibu yenu. Kuna mmoja kanipa ushauri wa tiba asili. Kiukweli kabisa...siamini upande huo kabisa though niliwahi kwenda kwa wataalam kama 30 hivi tofauti bila mafanikio. Nikaamua kurudi kwa Mungu upya na kutubu. Na nilichukua mwaka mzima kujihusisha na tiba hizo na nilivyoona hazina tija nikaamua kurudi kwa Mungu.


Umri na elimu ni Degree...umri 35years.


Sina kibanda...kiwanja wala pesa ya kusema nitaanzisha biashara.


Kuhusu ndugu....ndugu zangu ni type ile ambayo ikimuona mtu yupo kwenye problems ndio wanafurahia. Ukiwa kwenye furaha wanapretend unafki.

Bado haujakishughulisha vizuri kichwa!
 
Nashukuru kwa majibu yenu. Kuna mmoja kanipa ushauri wa tiba asili. Kiukweli kabisa...siamini upande huo kabisa though niliwahi kwenda kwa wataalam kama 30 hivi tofauti bila mafanikio. Nikaamua kurudi kwa Mungu upya na kutubu. Na nilichukua mwaka mzima kujihusisha na tiba hizo na nilivyoona hazina tija nikaamua kurudi kwa Mungu.


Umri na elimu ni Degree...umri 35years.


Sina kibanda...kiwanja wala pesa ya kusema nitaanzisha biashara.


Kuhusu ndugu....ndugu zangu ni type ile ambayo ikimuona mtu yupo kwenye problems ndio wanafurahia. Ukiwa kwenye furaha wanapretend unafki.


Mkuu pole sn kwa Hali ulo nayo!

Mi niseme machache juu ya hoja yako!
Dunia ni Mahali penye shida sn Hasa ukizaliwa ktk familia maskini na ukakosa Urithi wowote ule Yani Elimu na Mali au ardhi au nyumba! Na Hasa Ukiwa mwanaume! Mengi sn yatakukuta Ukiwa masikini Sifa mbaya na kutengwa na Jamii na kutokuthaminiwa na Jamii au ndugu! Yote haya yatakukuta!

Niseme tu kidogo wewe una nafuu ata ya hiyo shahada. Kiasi uko na mwanga Wa kuweza kupambana!

Ningependa tu kujua uko mkoa gani ili niweze kutoa maoni yng ya nini waweza kufanya!

Asante!
 
Nashukuru kwa majibu yenu. Kuna mmoja kanipa ushauri wa tiba asili. Kiukweli kabisa...siamini upande huo kabisa though niliwahi kwenda kwa wataalam kama 30 hivi tofauti bila mafanikio. Nikaamua kurudi kwa Mungu upya na kutubu. Na nilichukua mwaka mzima kujihusisha na tiba hizo na nilivyoona hazina tija nikaamua kurudi kwa Mungu.

Umri na elimu ni Degree...umri 35years.


Sina kibanda...kiwanja wala pesa ya kusema nitaanzisha biashara.


Kuhusu ndugu....ndugu zangu ni type ile ambayo ikimuona mtu yupo kwenye problems ndio wanafurahia. Ukiwa kwenye furaha wanapretend unafki.

pole sana kamanda, hata mimi nilipitia kipindi cha mpito kigumu sana kabla ya ajira, kumbuka kusali kila siku asubuhi na kumweleza Mungu shida zako. ULIHITIMU DEGREE GANI?
 
Back
Top Bottom