Mrisho Gambo ajijue yeye sasa hivi ni Mbunge sio Mkuu wa Mkoa tena

Lazima utofautishe ziara za kiutendaji na ziara za kisiasa.

Gambo haya unayolialia uliyatengeneza ukiwa RC Arusha dhidi ya MP/Mbunge godbless_lema.

Leo yanakurejea wewe mwenyewe pole usilie lie,ila Mbunge nafasi yake ni kubwa kuwakilisha wananchi na kuisimamia Serikali (Kuanzia Rais, mawaziri ,manaibu n.k). Ziara zako hazihitaj wataalamu au watendaji wa Manispaa/Halmshauri au Jiji. Ww sikia shida za wananchi zibebe zifikishe sehemu husika.

Yaani Mbunge akifanya ziara yake yeye Kama Mbunge sio ziara za kiutendaji sababu hana mamlaka ya kutenda au kuagiza kitu fulani kifanywe. Ni tofauti na Waziri, Naibu waziri, Mkuu wa mkoa, Mkuu wa wilaya au Mkurugenzi hawa wanaweza kutembea na watendaji wa idara ktk ziara zao sababu wana mamlaka ya kuagiza (Power of ordering).

Ziara za Mbunge ni ziara za aidha kusikia changamoto za wananchi wake ,kuzibeba na kuzipeleka Sehemu husika (Serikalini) kushawishi Serikali izitatue na kuisimamia Serikali izitatue au ziara za kutembelea miradi mbalimbali iliyotekelezwa katika Jimbo lake kuona mafanikio na kasoro hivyo kuwasilisha sehemu husika kwa utatuzi zaidi.

Lazima Gambo ajiondoe ktk viatu vya nafasi ya ukuu wa mkoa nafasi aliyekuwepo, sababu sasa hivi yeye sio mkuu wa mkoa ,yeye ni Mbunge hana mamlaka yeye binafsi kutembea na watendaji wa idara au wataalamu wa Halmshauri, Manispaa au jiji katika ziara zake anapotaka yeye bila idhini ya viongozi wa Serikali aidha Mkurugenzi, mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa.

Sababu hao watendaji/wataalamu ni watu wa Serikali wapo chini ya Mkurugenzi, Kama Mkurugenzi hajaridhia wataalamu au watendaji kuambatana na Mbunge ktk ziara zake hilo huwezi lazimisha.Sababu hata wakihudhuria hawawezi pokea maagizo kutoka kwa Mbunge.

Mbili ,Mbunge mamlaka yake ni makubwa sana sio wa kugombana na Mkurugenzi,Mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa ,sababu Mbunge ana nafasi ya kuonana na waziri mkuu mtendaji mkuu wa shughuli za Serikali, Mbunge ana nafasi ya kuonana na waziri yeyote, Naibu waziri yeyote kuwasilisha changamoto za wananchi wake ktk Jimbo husika.

Lakini Mbunge na yeye ni mjumbe ktk kikao cha Baraza la madiwani hivyo ana nafasi kubwa ya kuwasilisha changamoto alizozisikia na kuzikusanya kutoka kwa wananchi.

Lakini pia Mbunge ni mwenyekiti wa kamati ya fedha za mfuko wa Jimbo ,hivyo ana nafasi ya kushawishi kamati fedha fulani iende Sehemu fulani kutokana na changamoto alizokusanya na kuzisikia ktk ziara zake ili kidogo zikatatue hizo changamoto.

Lakini pia Mbunge ana nafasi ya kupata mtandao mkubwa wa wafadhili kutoka nje au mashirika tofauti kupitia Manispaa au Halmshauri aliyopo na wakaja kutekeleza miradi mbalimbali. Hii njia alikuwa anaitumia saana Mh.@zittokabwe Kigoma mjini.

Zitto alitafuta wafadhili mwenyewe Bil 100 kutoka JICA (Japan) kwa maboresho ya Bandari ya Kigoma ila Serikali tuu ndio ilikwamisha ku saini, Mradi wa Bonde la mto luiche Serikali ya Kuwait (Kuwait Fund ),Bandari ya Ujiji, Barabara za Pavement blocks ufadhili wa Serikali ya Ubelgiji inayotoa Euros mil.65 Kigoma tu, Mradi wa mchikikichi kupitia wafadhili TradeMark East Africa.

Hii ni mifano dhahiri ya namna Mbunge anaweza tumia nafasi yake katika kutatua matatizo ya wananchi wake.Kulazimisha kufanya ziara pamoja na watendaji/wataalamu wa Halmshauri,Manispaa au Jiji haisaidii kitu sababu hawatafuata agizo la Mbunge ila agizo la Mkurugenzi ambaye ni boss wao,au mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa au kiongozi yeyote mkubwa wa Serikali ila sio Mbunge.

Mnavyozozana na kugombana waziwazi ikiwa nyinyi nyote ni wanachama wa chama kimoja alafu bado mnagombana tafsiri yake nini?, Sababu zamani wabunge wa vyama pinzani walikwamishwa kwa Serikali kutosaini miradi ya wafadhili sababu ni wabunge wa upinzani au Halmshauri/Manispaa ipo chini ya upinzani. Sasa hivi je?

Tutaona mengi ,usipotumia akili ktk kuwakilisha, kutetea na kuisimamia Serikali ktk kuletea wananchi maendeleo Mbunge utaishia kulalamika hatimaye na hutafanya lolote hadi miaka 5 inakwisha.

Rai yangu haina maana RCs, DCs ,DEDs kuingia migogoro isio na maana na Mbunge, Mbunge ajue nafasi yake na hawa viongozi wajue nafasi zao ubaya tunafanya kazi kwa kila mtu kutaka kuonekana kwa mkubwa kwamba anafanya kazi tatizo. Wajibikeni kwa ajili ya wananchi na kwa maslahi yao.


Abdul Nondo.
CCM msituchoshe bana ... mnajitekenya wenyewe mnacheka wenyewe ... mnalazimisha hamasa wala watu hawana time na nyinyi ... serekali yenu na watendaji wake haina mvuto sikwambii hao wabunge ndio kabisaaaaa!

Mnatengeneza malumbano ili ionekane kuna amsha-amsha ya kukimbiza maendeleo ndio mnazidi kuharibu kabisaaaaaa mnaonekana kabisa mnacheza sinema za mzee yombayomba

Mlituahidi Tanzania tutaishi kama ulaya na mkasema wapinzani ndio walikua wanachelewesha maendeleo haya sasa tunasubiri msituletee mapichapicha ya kutengeneza hapa hamna amsha-amsha yeyote Hovyooooo ... !!!
 
Uchawi una tabia moja. Mwanzoni huuwa majirani, lkn majirani wakiisha unaanza kuingia kwenye ukoo wa mchawi na hatimaye humuua mchawi mwenye.

Hiyo ndiyo CCM. Awali CCM ilishughulika na wapinzani. Sasa wapinzani hakuna inashughulikia wanaccm wenyewe.
 
Lazima utofautishe ziara za kiutendaji na ziara za kisiasa.

Gambo haya unayolialia uliyatengeneza ukiwa RC Arusha dhidi ya MP/Mbunge godbless_lema.

Leo yanakurejea wewe mwenyewe pole usilie lie,ila Mbunge nafasi yake ni kubwa kuwakilisha wananchi na kuisimamia Serikali (Kuanzia Rais, mawaziri ,manaibu n.k). Ziara zako hazihitaj wataalamu au watendaji wa Manispaa/Halmshauri au Jiji. Ww sikia shida za wananchi zibebe zifikishe sehemu husika.

Yaani Mbunge akifanya ziara yake yeye Kama Mbunge sio ziara za kiutendaji sababu hana mamlaka ya kutenda au kuagiza kitu fulani kifanywe. Ni tofauti na Waziri, Naibu waziri, Mkuu wa mkoa, Mkuu wa wilaya au Mkurugenzi hawa wanaweza kutembea na watendaji wa idara ktk ziara zao sababu wana mamlaka ya kuagiza (Power of ordering).

Ziara za Mbunge ni ziara za aidha kusikia changamoto za wananchi wake ,kuzibeba na kuzipeleka Sehemu husika (Serikalini) kushawishi Serikali izitatue na kuisimamia Serikali izitatue au ziara za kutembelea miradi mbalimbali iliyotekelezwa katika Jimbo lake kuona mafanikio na kasoro hivyo kuwasilisha sehemu husika kwa utatuzi zaidi.

Lazima Gambo ajiondoe ktk viatu vya nafasi ya ukuu wa mkoa nafasi aliyekuwepo, sababu sasa hivi yeye sio mkuu wa mkoa ,yeye ni Mbunge hana mamlaka yeye binafsi kutembea na watendaji wa idara au wataalamu wa Halmshauri, Manispaa au jiji katika ziara zake anapotaka yeye bila idhini ya viongozi wa Serikali aidha Mkurugenzi, mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa.

Sababu hao watendaji/wataalamu ni watu wa Serikali wapo chini ya Mkurugenzi, Kama Mkurugenzi hajaridhia wataalamu au watendaji kuambatana na Mbunge ktk ziara zake hilo huwezi lazimisha.Sababu hata wakihudhuria hawawezi pokea maagizo kutoka kwa Mbunge.

Mbili ,Mbunge mamlaka yake ni makubwa sana sio wa kugombana na Mkurugenzi,Mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa ,sababu Mbunge ana nafasi ya kuonana na waziri mkuu mtendaji mkuu wa shughuli za Serikali, Mbunge ana nafasi ya kuonana na waziri yeyote, Naibu waziri yeyote kuwasilisha changamoto za wananchi wake ktk Jimbo husika.

Lakini Mbunge na yeye ni mjumbe ktk kikao cha Baraza la madiwani hivyo ana nafasi kubwa ya kuwasilisha changamoto alizozisikia na kuzikusanya kutoka kwa wananchi.

Lakini pia Mbunge ni mwenyekiti wa kamati ya fedha za mfuko wa Jimbo ,hivyo ana nafasi ya kushawishi kamati fedha fulani iende Sehemu fulani kutokana na changamoto alizokusanya na kuzisikia ktk ziara zake ili kidogo zikatatue hizo changamoto.

Lakini pia Mbunge ana nafasi ya kupata mtandao mkubwa wa wafadhili kutoka nje au mashirika tofauti kupitia Manispaa au Halmshauri aliyopo na wakaja kutekeleza miradi mbalimbali. Hii njia alikuwa anaitumia saana Mh.@zittokabwe Kigoma mjini.

Zitto alitafuta wafadhili mwenyewe Bil 100 kutoka JICA (Japan) kwa maboresho ya Bandari ya Kigoma ila Serikali tuu ndio ilikwamisha ku saini, Mradi wa Bonde la mto luiche Serikali ya Kuwait (Kuwait Fund ),Bandari ya Ujiji, Barabara za Pavement blocks ufadhili wa Serikali ya Ubelgiji inayotoa Euros mil.65 Kigoma tu, Mradi wa mchikikichi kupitia wafadhili TradeMark East Africa.

Hii ni mifano dhahiri ya namna Mbunge anaweza tumia nafasi yake katika kutatua matatizo ya wananchi wake.Kulazimisha kufanya ziara pamoja na watendaji/wataalamu wa Halmshauri,Manispaa au Jiji haisaidii kitu sababu hawatafuata agizo la Mbunge ila agizo la Mkurugenzi ambaye ni boss wao,au mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa au kiongozi yeyote mkubwa wa Serikali ila sio Mbunge.

Mnavyozozana na kugombana waziwazi ikiwa nyinyi nyote ni wanachama wa chama kimoja alafu bado mnagombana tafsiri yake nini?, Sababu zamani wabunge wa vyama pinzani walikwamishwa kwa Serikali kutosaini miradi ya wafadhili sababu ni wabunge wa upinzani au Halmshauri/Manispaa ipo chini ya upinzani. Sasa hivi je?

Tutaona mengi ,usipotumia akili ktk kuwakilisha, kutetea na kuisimamia Serikali ktk kuletea wananchi maendeleo Mbunge utaishia kulalamika hatimaye na hutafanya lolote hadi miaka 5 inakwisha.

Rai yangu haina maana RCs, DCs ,DEDs kuingia migogoro isio na maana na Mbunge, Mbunge ajue nafasi yake na hawa viongozi wajue nafasi zao ubaya tunafanya kazi kwa kila mtu kutaka kuonekana kwa mkubwa kwamba anafanya kazi tatizo. Wajibikeni kwa ajili ya wananchi na kwa maslahi yao.


Abdul Nondo.
Nondo mbona una kichwa kibovu, huyu gambo nani kamchagua kuwa mbunge? Sema aliyeiba kura na kujipachika ubunge.....
 
Huyo dogo na limbukeni mwenzake Bashite walifikia mahali wakajisahau na kudhani kuwa wao ndiyo wenye nchi. Gumbo anavuna alichopanda. Alizoea kuwanyanyasa akina Lema asijue kutesa kwa zamu. Ashukuru Mungu amesaidiwa kuiba kura na kuwa mbunge. Hakupaswa kuwa hata mjumbe wa nyumba kumi. Ana bahati. Naomba Magufuli amuamishie Arusha mkuu wa mkoa wa sasa wa Mbeya ili ampe na kumtia adabu.
 
Back
Top Bottom