Hako kazee kamepauka. Maoni yake hayawezi kuwa habari. Mimi niliacha kukasikiliza muda mrefu sana.
twambieni kama jamii sasa ni mali ya washabiki wa chadema maana naona imekuwa web ya kumponda kila aliyetofauti na mawazo ya chadema why? this is no longer a home of great thinkers my friends it is too much.
twambieni kama jamii sasa ni mali ya washabiki wa chadema maana naona imekuwa web ya kumponda kila aliyetofauti na mawazo ya chadema why? this is no longer a home of great thinkers my friends it is too much.
twambieni kama jamii sasa ni mali ya washabiki wa chadema maana naona imekuwa web ya kumponda kila aliyetofauti na mawazo ya chadema why? this is no longer a home of great thinkers my friends it is too much.
katika fukua fukua yangu nimeikuta hii pahala.....
Huyu usanii kaanza zamani sana Lyatonga!
Nimecheka weee, mpaka mbavu zangu zinauma.
Huwezi kuamini kwamba nimeona sinema ya vichekesho ambayo naweza kabisa kuipa nafasi ya kwanza kwa kunichekesha vyema mwaka huu.
Kitu kilichozoeleka ni kwamba sinema nyingi za namna hiyo tunaziona kutoka kwa waigizaji wa nje, lakini huyo wa safari hii ni Mtanzania mwenzetu. Sielewi kwanini anakaa akipigizana kelele na serikali badala ya kuingia kwenye usanii na akala mahela yake kiulaiiini, kwani hawaoni wasanii wa sasa wa Bongo, wimbo mmoja tu (wao wanaita single) ananunua gari na hata nyumba.
Huyu msanii siyo mwingine, bali ni Augustino Lyatonga Mrema, mzee wa Kiraracha kule Moshi aisee.
Basi bwana, yeye jana wakati ameshachukua fomu kutoka kwa wakubwa wa usimamizi wa uchaguzi, akapanda baiskeli akiwa na mgombea mwenza wake, mwanamama kutoka Zanzibar. Wakazungushwa mji mzima wa Dar es Salaam wakiwa na wafuasi wao huku bendera za chama chao cha TLP zikitawala.
Ilikuwa ni burudani ya aina yake kwa kweli. hakuna aliyenuna baada ya kumuona Mrema akiwa juu ya baiskeli ya miguu mitatu akiwapungia wananchi kwa ishara ya kuwaambia kwamba anaingia kwenye kinyang'anyiro hivyo anaomba kura zao aweze kula tu kama wenzake wanavyofanya. Hakuna tofauti kamwe miongoni mwa hawa wenzetu.
Naomba kumpa ushauri wa bure, ikiwa atashindwa (jamba ambalo ninalo uhakika), basi aanze uigizaji katika vituo vya trelevisheni vya hapa kwetu na hata nje, kwani hata kama hajui malugha ya wengine anaweza kabisa kuwa mchekeshaji wa ishara tu kama Roward Atkinson (Mr. Bean). Akifanya hivyo hatakuwa mwenzetu tena, atakuwa ni bilionea mkubwa.
ANGALIZO LA DK AUGUSTINO MREMA KWA CHADEMA NA UHAMASISHAJI WA MAANDAMANO - Global Publishers
Mbunge wa Jimbo la Vunjo, mwenyekiti wa Chama cha TLP na mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Fedha za Serikali za Mitaa Dk. Augustino Lyatonga Mrema akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo wakati alipotoa angalizo kwa chama cha CHADEMA kutokana na mikutano yake inayohamasisha maandamano akisema kuhamasisha maandamano kunaweza kuleta uvunjifu wa amani kama ilivyotokea kwa nchi za Madagascar, Misri, Tunisia na sasa Libya.
Dk. Mrema ameongeza kwamba kwa kawaida mkiiangusha serikali bila kufuata utaratibu wa kikatiba upo uwezekano mkubwa wa kuleta vurugu katika nchi kama ilivyotokea kwa nchi hizo za kiafrika ambazo hata walipoondolewa watawala ambao walikuwa hawatakiwa bado hakuna utulivu na mahali pengine jeshi limepata mianya ya kuchukua madaraka kwa lengo la kuhakikisha usalama wa nchi zao kama ilivyotokea kwa Misri ambayo kwa sasa inaongozwa na Jeshi.
Mbunge wa Jimbo la Vunjo, mwenyekiti wa Chama cha TLP na mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Fedha za Serikali za Mitaa Dk. Augustino Lyatonga Mrema akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo wakati alipotoa angalizo kwa chama cha CHADEMA kutokana na mikutano yake inayohamasisha maandamano akisema kuhamasisha maandamano kunaweza kuleta uvunjifu wa amani kama ilivyotokea kwa nchi za Madagascar, Misri, Tunisia na sasa Libya.
Dk. Mrema ameongeza kwamba kwa kawaida mkiiangusha serikali bila kufuata utaratibu wa kikatiba upo uwezekano mkubwa wa kuleta vurugu katika nchi kama ilivyotokea kwa nchi hizo za kiafrika ambazo hata walipoondolewa watawala ambao walikuwa hawatakiwa bado hakuna utulivu na mahali pengine jeshi limepata mianya ya kuchukua madaraka kwa lengo la kuhakikisha usalama wa nchi zao kama ilivyotokea kwa Misri ambayo kwa sasa inaongozwa na Jeshi, katika picha kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho Mh. Hamad Tao.