Mrejesho: Uso kwa uso na shemeji gesti

Mrejesho: Uso kwa uso na shemeji gesti

Mkuu kama unaamini mkeo ni mwaminifu kwako basi tambua humtendei haki hata kidogo, wewe ni zaidi ya katili kwake, na ulimuoa ili umkatili. Hivi unajisikiaje unapokuwa na mchepuko wako faragha? mnafanya tendo la ndoa wakati si mwanandoa mwenzio??? hata mkeo huwa humkumbuki? fikiria ungekuwa wewe ndio mke!

Pia tambua huyo mchepuko yupo na wewe lakini huko Arusha ana michepuko mingine zaidi, we jisifie tu kuwa anakupenda na hana haja ya wanaume wengine??, imekula kwako, yeye akiwa Arusha akae tu bila ya kukutana na mwanaume eti kisa wewe upo, na hali anajua wewe upo na mkeo huku, hakuna ana michepuko mingine ya kutosha. Usipoangalia utakuja kumletea mkeo magonjwa na kumuumiza moyo wake.

Pia kuhusu msaada wa kimahitaji, unaona sifa kwa jinsi unavyosaidiwa, je asingekuwepo huyo mwanamke usingeihudumia familia mwenyewe? acha kubweteka akili kwa kuwa yupo mtu anakusaidia malezi ya familia, tafuta njia mbadala ya kupata kipato, na njia moja wapo ni kama ulivyoshauriwa hapo juu mfungulie mkeo biashara yoyote afanye. Sio kuchukua hela za watu tu ipo siku hizo hela zitakugharimu sana.

Pia acha kumsema mkeo vibaya, eti mama wa nyumbani, ulishindwa nini kumfungulia hata genge auze matunda tangu umemuoa, leo ndo umuone mama wa nyumbani?. Acha bwana huyo mchepuko atakufikisha pabaya japo leo unamuona mwema. Kuhusu ndugu chukua hatua ya busara tu wewe si ndio kichwa cha family.
 
hivi kuna wanaume ambao hawana mchepuko? labda ni 15% tu!
Jamaa akomae na mchepuko wake bhana aache kujing'atang'ata bure; mchepuko unaokutia hasara na kukuegemea ndio shida, kwanza huyo mkewe amekaa kimchepukochepuko tabia gani hizo za kulala na mikombati
 
Nimepapenda unakofanya kazi maana kumbe makato ya kodi mbalimbali na bima za afya hayakuhusu wewe! Yaani kutoka katika mshahara unakatwa madeni tu uliyokopa kwa hiari..

Tuelekezane, tafadhali maana wengine tumechoshwa na makato ya lazimaa
 
Umenigusa, Umenigusa, Umenigusa, Umenigusa, Kwa Ufupi Piga Chini Mke Oa Mchepuko Kaka. Hawezileta Watu Home Kiasi Hcho, Kaka, Unijulishe Kama Umefanikisha
 
duu wanaume kama mabinti.

eti laki tano tuu kweli uko serious mkuu ishi kulingana na mshahara wako hao ndungu walojaa hapo kama kuna msiba wale utachopata wakitaka mboga tatu wanunue looo
lazima wew na mkeo muwe na maamuz ya life style ya maisha yakipato chenu.

unaonaje mkeo naye atafute mchepuko wenye hela maana hela yako haitoshi ?

Hajasema anampenda mchepuko kwa ajili ya hela.. Kasema walipendana tangu chuo.. Lakn akaleteww mke amwoe
 
Nina wasiwasi hata mke wa rafiki yako ulimtafuna japo humu umedai hujamgusa.
 
Tukisema idadi ya wanaume imepungua hamuelewi.... ndio kama hivi

Wife usiingizwe mkenge... fuatilia threads zake za nyumba utagundua hili jamaa ni jiongo balaa. FYI lenyewe limeshasema kikojoleo chake si rizki...

Mijitu kama hii inaniudhi sana. Shwain!!
 
Back
Top Bottom