Mrejesho: Sijui huyu mzungu atanikubali?

Mrejesho: Sijui huyu mzungu atanikubali?

jean phillipe beyun

Senior Member
Joined
May 18, 2015
Posts
142
Reaction score
167
Wakuu nawasalim wote,

Takribani miezi miwili kasoro niliwaeleza kuhusu mwanamke wa ki Mexico alieletwa na kampuni yetu kwa mkataba maalum kuongoza idara niliyopo
Na nikawaeleza kuwa tumekua tukitoka outing na kufanya vitu vingi kama wapenzi, kiasi kuwa kazini watu wakadhan nimeshamlamba mmexico
Naomba mrejee habari hiyo

Wengi wenu mlinishauri nisithubutu kumtaka kimapenzi kwamba wazungu wengi ni social sana, nikifanya hivyo naweza haribu kazi ukizingatia ni bosi wangu kazini

Mrejesho wenyewe:-

Nilitii maelekezo yenu sikumtamkia neno lolote kuhusu mapenzi hadi siku moja jumamosi aliponituma nikamchukulie zile burger za bonjour morocco zilizoamia leaders club huwa anazipenda sana.

Niliporudi kwake na burger nilimkuta na taulo tu akijiandaa kwenda kuoga, nilishindwa kujizuia, uchu mkali sana uliniingia, shetani akanishawishi nijilipue, bahati nzuri nilipojilipua akanipokea kwa mikono miwili tukawa tumejuana kimwili.

Nilifurahi sana nikajua nimeshaukata, tuliendelea wiki yote iliyofuata maana alisema alikua na kiu sana siku nyingi hajafanya hivyo

Hata hivyo furaha yangu imekua short lived, siku moja nastukia ananiambia twende airport tukampokee boyfriend wake anakuja kutoka America nilipigwa na butwaa, maana nilijua mm ndio nimeshakua boyfriend wake,

Wana Jf kwa kifupi hilo jitu lake kutoka amerika tangu limekuja sina raha, linakuja kazini kwetu wanabusiana hapo, yule Dada kalitambulisha hilo zungu kazini kwetu, sasa watu wananitazama wanachekea pembeni nimegeuka laughing stock

Juzi jumapili yule bosi wangu ameniita nyumbani kwake nikawakuta kwenye kochi wakiwa wanakumbatiana, surprisingly lile jitu eti linaniambia niwapeleke wakapaone Zanzibar weekend ijayo, dharau kiasi gani hii?

Nashindwa kuleta chokochoko kwa kuwa yule Dada ni bosi wangu, nilitegemea yy ndie awe na busara azuie huyo jamaa asije kwa kuwa tayari yupo tayari na mm lakini ni kama amenipotezea.

Wakati Mara zote tulipokutana alidai mm ndie Fundi kuzidi wengine wote, nashindwa hata kumwelewa.Huu si uhuni kabisa ndugu zangu!!!

Yaani hata kwenda kazini ikifika asubuhi najiuliza Mara mbili mbili, nampenda sana huyu mmexico kumbe nae hajatulia.Na wanawake wa kiswahili nao nashindwa hata kuwaelewa Jumamosi nimeenda kwa yule demu wangu wa kiswahili ili tuweze Ku reconcile maana kwa karibu miezi miwili hatukua pamoja, cha kushangaza anadai eti amesha move on, yaani mtu miezi 2 umeshapata mpenzi Mpya?
Na wakati alikua ananililia kila siku nisimwache

Nimechanganyikiwa sana kwa kweli, nianze tu mchakato wa kutafuta kampuni nyingine nihame pale

Ina maana huyu mzungu hawezi kuona ni jinsi gani ameniumiza? Ina maana hilo jitu lake likiondoka ataendelea tena na mimi au?

Mtu kwa karibu miezi minne tangu kuja kwake nimeacha shughuli zangu zote na kumzungusha yeye na kuwa karibu nae kwa kila hali na hadi kufikia kuwa wapenzi, nimeacha kwenda kwenye shuguli za kijamii, misiba, harusi na kadhalika kwa ajili yake, Leo limekuja hilo jamaa lake hata kunibembeleza tu hamna, hata kunieleza kuhusu hatma yetu hamna.

Can someone help
What should i do?
 
We mwenyewe umesha sema wazungu ni watu social sana sasa unalalamika nini?
We usha wekwa kwenye ile social side kwahiyo huna chako mpaka hapo.
 
Kwanza, wa-Mexicano nao ni wazungu? Oh wait...kibongo bongo hata Waarabu ni wazungu. I get it.

Pili, we bana hebu endelea na maisha yako. Kubali tu matokeo kuwa umetumika kama mchepuko, basi.

Hilo nalo ni jambo la kuja kuomba ushauri humu? Mbona liko dhahiri kabisa...
 
Mzigo kakupa kidogo umezama moja kwa moja, bora asingekuonjesha aisee cha msingi piga moyo konde usihame omba likizo kwa huyo mmexico atakuruhusu upishe upepo then lijamaa likiondoka tuu kurudi kwao unarudi kujipigia kama kawaida tuu
 
Wewe jamaa before ya kusema hawa wetback wazungu soma history kwanza ----- wewe
 
Kwanza, wa-Mexicano nao ni wazungu? Oh wait...kibongo bongo hata Waarabu ni wazungu. I get it.

Pili, we bana hebu endelea na maisha yako. Kubali tu matokeo kuwa umetumika kama mchepuko, basi.

Hilo nalo ni jambo la kuja kuomba ushauri humu? Mbona liko dhahiri kabisa...

Sasa mngejuaje kuwa na yeye kasha date 'mzungu'??
 
Dawa yake ndogo, mzungu akiondoka halafu akataka umpe mambo, mwambie akununulie ghorofa kariakoo lasivyo umesha move on yeye aendelee tu na lizungu lake
 
jean phillipe beyun

mkuu kwa muda huo ulioweka bandiko, ushauri wangu nenda muhimbili ulizia uwanja wa mpira ulipo, hapo kuna ka wodi kana vidirisha vidogo vya chuma omba nafasi hapo, maana dodoma mbali.
 
Last edited by a moderator:
kama unakumbuka nilikuushaur kuwa hawa ni wataalam xn wa one night stand luv...au kibongobongo tunawaitaga hit and run,sasa ww ndio umejenga kibanda! yaani hapo alishasahau hata km ameshawah date na ww,kwa ushaur zaid achana nae subir msela wake asepe utagegeda tena...ukimbana xn utakosa kaz na yy pia
 
Nenda kawashawshi mfanye 3some kiroho saf kabsa
 
Back
Top Bottom