Mrejesho: nashukuru nimepata mpenzi

Mrejesho: nashukuru nimepata mpenzi

wepson

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2014
Posts
831
Reaction score
219
Habari wana MMU bila shaka mmesherekea sikukuu ya Chrismass na Mwaka mpya vizuri na kwa amani,ingawa jana kundi la Panya Road limetikisa Mji maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar Es Salaam kama Sinza ,Mwananyamala, Kinondoni ,Temeke na Kinyerezi na kusababisha baadhi ya maduka kufungwa mapema.

Nirudi kwenye maada ya msingi kwa kweli napenda kurudisha shukrani zangu za dhati hapa jukwaani kwani nilitangaza kutafuta Rafiki wa Kike awe aliyekomaa kiakili/Kifikra (matured) ,kwa kweli nashukuru nimekutana na mwanajamvi mmoja hapa ambaye ni so serioous na kwa kweli tunaelewana vizuri sana.

Na tumepanga mambo mengi mazuri kwa mwaka
huu bilka shaka napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa wajamvi wote walio jitokeza ingawa wengine walikua si jinsia husika na huku wengine wakiwa na umri uliopita vigezo .

Pia napenda kupeleka shukrani zangu za dhati kwa Moderator na mmiliki wa jamii forum kwa kutuwekea Jukwaa hili kwani limekua msaada kwetu kimawazo na kimaendeleo pale linapotumika kama lilivyopangwa na mwanzilishi. Asante sana wenu Wepson
 
haya mkuu kila la kheri... Mm nakutakien maisha mema na mjenge familia iliyobora
 
Labda kuna sehem ulikosea mkuu

Sidhani ila ndo sitokaa kufikiri tena wala si lazima kuoa au kuwa na mwenza

Mambo ya kufanya majiribio na maisha Mimi siwezi kwa kweli acha niwe mshamba
 
Mbwaroad wamerudi huko??naulizia michepuko??
 
Sidhani ila ndo sitokaa kufikiri tena wala si lazima kuoa au kuwa na mwenza

Mambo ya kufanya majiribio na maisha Mimi siwezi kwa kweli acha niwe mshamba

Hawa watu bwana wana mambo sana ukimtukuza sana jeuri zinaanza ukiwa careless vilio so weka plan nzuri kama hivi kaa tu kimya atakuja na kujikomba mwenyeweee
 
Back
Top Bottom