Mrejesho: MwanaJF aliyeomba mtaji

Ukiona hivyo ujue...ushapigwa wewe... ndio maana anakuzungusha
Kesha pigwa vp yy hakumkopesha bali alimpatia mtaji na kutaka kumuongezea kama kweli alikuwa ameanza biashara lkn kwa ujinga wake ni kama alikula hiyo pesa ss hapo nn maana yake kajipiga mwenyewe kwa upumbavu wake ni tapeli huyo hana tofauti na muhongo.
 
Pole sana na hongera kwa moyo ulionao wa kupenda kujali wengine na kutaka kuwainua
 
Itakuwa si vizuri mkuu, lengo sio kumdhalilisha bali kumpa funzo ajirekebishe na wengine wajifunze kutokana na kisa hiki.

Hapana mtaje. Ataendelea kutapeli. Wee ulicho kipata ni somo ambalo wengine wanatakiwa kujifunza. Atatapeli na wengine. Muweke waz hapa tumfahamu. Tena kwenye post ya kwanza kabisa.
 
Itakuwa si vizuri mkuu, lengo sio kumdhalilisha bali kumpa funzo ajirekebishe na wengine wajifunze kutokana na kisa hiki.
Atakuja kutapeli wengine aisee, wengi sana wanakuja pm kuomba msaada tunashindwa kuwasaidia kwa kuogopa kutapeliwa.
 
Jamani!!!!!!. Naombeni.
 
Mkuu sisi wengine hatukuiona hiyo post uliyoituma mwanzo
Tubainishie mtu huyo ni Nani? Tuchukue Tahadhari tusije ingizwa Mkenge!!!
 

MKUU una huruma kama mimi naomba ujifunze mimi najifunza ka njia ngumu sn ingaa deep inside nashindwa kuacha kusaidia,hongera sn kwa hiko MUNGU AKUBARIKI
 
kuna matapeli wa aina nyingi, ingawa na wewe uli risk sana
Amewaponza na wenye shida kweli
 
Kitu ambacho ni kibaya na kinajijenga katika jamii ya kibongo ni tabia ya upigaji. Yaani sio wafanyakazi wa supermarket au kiwandani au maofisini wengi nimeona wanamawazo ya kipigaji tu, yaani wasilate mwanya. Ni muhimu kuwa na utamaduni wa kuwa na uadilifu kama nchi.
 
watu kama hao ndio wanaossababisha wenzao walio serious kukosa misaada.
 
Yaani sijui tuna fikra za namna gani, kuna siku niliagiza kitu flani kutoka china, kwa watu nisiowajua na hata wangenipiga nisingeweza hata kuwafuatilia licha ya kuwapata, lakini cha ajabu niliwatumia hela kwa western union walikiri kupokea na muda mfupi baadae walinitumia mzigo wangu na mpaka unafika airport dar, jamaaa wananiambia mzigo uko hapo airport wahi ukauchukue usije ukarudi, nikachukua mzigo wangu na nikakuta uko vile vile kama tulivyo kubaliana.

Nilishangaa sana kwa kweli huo uaminifu, maana ingekuwa bongo, ungeshangaa tu simu haipatikani tena.
 
mkuu, kuajiriwa sio lazima serikalini au mgodini, vijana waajiriwe hata kuuza duka, kukata kucha salon kuendesha bodaboda, ili mradi jioni anapeleka hesabu na mwisho wa mwezi anapewa jasho lake, huyu kijana angeambiwa aende kuajiriwa kufuta vumbi supermarket ungeshangaa alivyo na bidii ya kazi,
 
Hahahaha, ila huko dukani nako wengi wao wanapenda kudokoa kweli, wewe fikiria wengine mpaka pale airport wanadokoa licha ya makamera yote yale
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…