hayo mambo yanaongeleka kabisa hapo,mngeazia hata kanisani kama ni wakristo, naona hakuna nguvu kubwa iliyotumika kutatua mzozo badala yake nguvu kubwa inatumika kugombania nyumba,wewe ukishapewa hiyo nyumba au ikiuzwa mkagawana hela utakuwa na raha gani, unajua ni jinsi gani mtu anajibana mpaka anasimamisha kibanda kwa maisha haya ya mtanzania wa kawaida, na je kama mna watoto mumeshazungumzia mustakabadhi wa watoto, usiangalie upande mmoja tu maamuzi yako yanaweza kuvuruga kabisa familia, mambo ya wanaume kudanganya hawajaoa mbona ndio habari ya mjini kwa sasa, mpaka mumeo anahamia kwa mchepuko ujue kulikuwa na uzembe hapa katikati, haiwezekani tu from no where mwanaume anaondoka ghafla nyumbani, nakushauri ufikirie vizuri kabla ya maamuzi hayo unayoendelea kuchukua.