Mramba anasafishwa?


Post nimeisoma vizuri tu.

Sijui mimi,wewe au na wewe nani hajaielewa. na sijui nani anatafuta sympathy na kama aliomba kukumbatiwa

Any way sinacomment zaidi.
 
Last edited:
Mimi nataka nyie wote mnaopinga.

KAMA ANGEKUWA NI BABA YENU AU REFIKI YAKO WA KARIBU UNGEFANYAJE?

SEMA UKWELI.


Mkuu Kanda2x2

Mbona unakuwa huelewi; angekuwa ni baba yangu ningemwambia; usijali baba angalau tumeshasoma ulaya, nyumba tumejenga dar na kule rombo na bado wewe ni mbunge. Ukifungwa jela tutakuja kukutembelea...

Lazima ukumbuke kuwa familia yake wamekuwa hizo hela pamoja naye hivyo ni muhimu wampe sapoti; hao wabunge badala ya kumuona adui wa yale wanayoyapigania bungeni wao wanampa hug...hawana hata aibu.
 
Kwa wizi na ujambazi wa hawa wakina Mramba, kama angekuwa baba ningemsusia na si ajabu ningemzomea.
Baba mwizi au mama mwizi sina undugu wala urafiki naye.
Tena sikiliza wewe Kandambili, mwizi ni mwizi tu hata akiwa na kesi ambayo haijaamuliwa bado ni mwizi. Na hata wakimu aquit mahakamani bado haitaondoa wizi wake. Kama aliiba atabaki ni mwizi tuuuuuuuuuuuu.
Ebu soma hiyo signature yangu ndugu.
 

MKuu, najua wewe ni mpambanaji na mchukia fisadi kweli. Lakini naomba usije ukaingia katika mtego na ukawa kama waziri wetu mkuu Pinda, to be caught up emotionally and throwing law out of the window.
Everybody is assumed innocent until proven guilty, au siyo? Mpaka sasa hatujaona ushahidi dhidi ya Mramba ni upi na hivyo hatuna budi kusubiri kesi yake iendelee tupate kujua zaidi. Nadhani hata wabunge walioenda kumpa pole walikuwa wanafanya hivyo in collegial gesture. Na si kitu kibaya.
Kupambana na ufisadi kunahitaji hekima, cool minds and even temper, ili siku watakapokamatwa waweze pia kushtakiwa na hatimaye kufungwa. Na si kushabikia tu.
 
Friends,
I have just three observations;
1. Was it proper kwa Wabunge ku-express public sympathy kwa Mh. Mramba? My opinion is no- They were neither to express sympathy nor to ignore. In my opinion wangem-treat with the business as usual attitude kama ambavyo wamekuwa wakifanya kabla ya hili zahama, wasubiri outcome then wa-respond kufuatana na outcome! By and large walichokifanya kinaleta tafsiri nyingi, na nyingi si nzuri, unafiki ikiwa inaongoza, ama kuamini kuwa yanayomtokea yote ni chuki binafisi, etc.
2. The notion of innocent till proven guilty- what do I think? My opinion ni kwamba bado hatujui mahakama itafikia conclusion gani na kwa sababu zipi? ili nataka kuhoji kuwa hata akiwa declared innocent na mahakama, ni wangapi tunaamini kuwa haki itakuwa imetendeka na kuwa kweli Mh. Mramba ni innocent kwenye charge hizo na nyingine zinazofanana na hizo ambazo hajashitakiwa nazo? Kama kweli tupo ambao conclusion ya mahakama ikiwa ni mu-declare innocent tutakubali kuwa kumbe yote haya yalikuwa uongo tu na defamation ya mtu safi, basi Mungu aibariki Tanzania!
3. Kama angekuwa mtu wako wa karibu ungefanyaje? My answer to that, is under such circumstances personal attributes zibaki kuwa personal, watu wake wa karibu ambao ni wafaidika wa kwanza na waathirika wa kwanza kwa mambo yanamhusu ndio wajue wana-deal vipi na hili! Wengine tuli-jadili kwa national interest because hatuna personal interests kwenye affairs zake!
 

Je na baba yako au mama yako huyo huyo akikuambia kuwa mwanangu mi nimeanza wizi toka kabla hujazaliwa na fedha zote zilizokufikisha hapa kuanzia posa ya mama yako hadi malezi yako yote mpaka leo hii vyote vya wizi utafanyaje hapo?.
 

Kweli nitabaki na msimamo wa kuchukia ufisadi wao na wao sintawapenda maana siku wakiondoka mimi na watoto wangu na wajukuu wangu tutabaki katika kilio. Wizi wao utakuwa umenipa tiba ya muda kama vile wanavyofanya kwa uchaguzi maana hii hii miela wanaonga wapiga kura na wanawarudisha bungeni na wakirudi bungeni wanawabeza tena kuwa wale majani. Sioni faida yao kabisa.
Nina machungu mengi nikisimulia hapa utashangaa. Yote chanzo ufisadi huu huu. Ni hawa hawa walikuwa wakisema kwa majigambo kuwa tule majani tu wakati wao wanakula pesa yetu ndugu. Ndugu zangu wakikosa dawa hospitali. Haloooooooooooooooo.
Kama wanashabikiwa na wana wao, sawa lakini siku si nyiingi vizazi vya wana wao watalia tu. Hatutaruhusu wizi huu uendelee na tukae kimya tu. Iko siku tutawauliza hata wana wao.
 
Mimi nataka nyie wote mnaopinga.

KAMA ANGEKUWA NI BABA YENU AU REFIKI YAKO WA KARIBU UNGEFANYAJE?

SEMA UKWELI.

SASA KAMA NI BABA NINGEKUWA NIMESOMESHWA SHULE ZA ACADEMIA, NIMENUNULIWA GARI NIMEPELEKWA ULAYA NA NYUMBA KUPEWA SIKU YA HARUSI,LAZIMA NINGESIKITIKA...
KAMA NI RAFIKI NINGEKUWA NAHUDHURIA MI DINNER PARTY, NIMESAIDIWA KWENYE MI TENDER YANGU, NA NIMESAIDIWA WATOTO WANGU KWENDA NJE ofcourse ningesikitika, ila mimi ni mtanzania watoto wangu wamerudishwa chuo kikuu kwa sababu sina 40% ya kuwalipia, watoto wanaenda shule miguu mitupu, shule kama za Galanos hazina chakula zimefungwa kwa mwezi mzima looh halafu kuna mtu kwa uzembe anasababisha bilions za pesa zipotee kama kweli hawakugawana kwa kweli siwezi hata kumpa mkono samahani sana...
 

Nadhani tunahitaji msaada wa wataalamu kuhusu haya mambo ya sheria Vs mtazamo na imani ya jamii (public views and perception) linapokuja suala la kesi. Haya mambo ya mtu kuwa mtuhumiwa mpaka hukumu nadhani ni mambo ya kisheria hasa hasa kwa ajili ya kuwalinda wanyonge wasionewe. Hata Mramba ni mnyonge mbele ya serikali inayomshitaki kwa hiyo analindwa pia. Ila kuna suala la jamii na imani yake kuhusu usafi wa Mramba. Nadhani wananchi wengi wanaamini kuwa ni kweli Mramba ni mwizi na hajaonewa. Hapa naaminisha kuwa hukumu ya jamii dhidi ya Mramba iko wazi. Watu wanamjua toka akiwa mtoto hadi sasa na kwa hiyo kama ana kitu kinachotia shaka wanajua. Na wao hawana haja ya kusubiri hukumu ya mahakama ili waamini kwamba ni mwizi. Kwa hiyo sina shaka hata mimi kwamba ni kweli jamaa ni mwizi. Ndiyo maana ninawashangaa wote wanaojifanya kumwonea huruma.
 

In the face of law, ndio hivyo lakini kwa mshtaki everybody is guilty until proven innocent. Jamhuri kwa niaba ya WaTZ wote inaamini kuwa Mramba ana hatia ndio maana imempeleka mahakamani.
 
Na Nora Damian

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam, imempa ruhusa tena waziri wa zamani wa Fedha ambaye pia ni Mbugne wa Rombo, Basil Mramba kwenda kuhudhuria na kufanya shughuli za bunge, kutokana na kesi yake ya kutumia vibaya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Sh 11 bilioni, kupangwa kuanza kusikilizwa Machi3, mwaka huu.


Kabla ya ruhusa hiyo, mahakama iliambiwa na upande wa mashtaka kuwa upelelezi wa kesi ya kutumia madaraka vibaya inayowakabili mawaziri wa zamani, Mramba, Daniel Yona na Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonja umekamilika.


Hayo yalielezwa jana katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na wakili wa serikali, Fredrick Manyanda mbele ya Hakimu Mkazi, Hezron Mwankenja ambaye alisema washitakiwa hao watasomewa maelezo ya awali Machi 3, mwaka huu.


Wakili anayemtetea Mramba, Hubert Nyange amewasilisha barua mahakamani hapo kuomba mteja wake aruhusiwe kuhudhuria vikao na shughuli nyingine za ubunge.


Barua hiyo iliwasilishwa mahakamani hapo Januari 30 mwaka huu.


Hakimu Mwankenja alikubali ombi hilo na kumruhusu Mramba kwenda bungeni kuendelea na shughuli nyingine za ubunge, lakini akaagiza awepo mahakamani Machi 3 mwaka huu kesi yao itakapotajwa.


Washitakiwa hao wanadaiwa kutumia madaraka yao vibaya na kuisababishia hasara serikali ya zaidi ya Sh 11 bilioni.


Wanadaiwa wakiwa waajiriwa wa serikali walitumia madaraka yao vibaya na kutoa msamaha wa kodi kwa kampuni ya M/S Alex Stewart ya nchini Uingereza kinyume na ushauri uliotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).


Souce: Gazeti la Mwananchi
 
Likizo yangu moja nilienda kutembea vijiji vya sehemu fulani hapa Tanzania. Kufika kule nikakutana na habari ya mwizi mmoja kuchomwa moto na wananchi wenye 'hasira kali'. Siungi mkono jambo hili.
Nilipouliza nikaambiwa waliiba siku Tatu zilizopita hapo kijijini na walionwa ila wakakimbia na walikuwa wamejificha mpaka siku walipoonwa walipojificha
Katika kuongea na wanavijiji wale nilipata kujua kuwa wezi pale hawavumiliki
Na sio rahisi mtu wa maeneo Yale akakua akawa mwizi
Maana ingine ni kuwa hizi tabia zina asili yake - kuanzia katika familia mpaka jamii inayo kuzunguka
Kama Mtoto akiiba tunamwita mjanja, jasiri, mjasiriamali na nk tunategemea nini akishakuwa ofisin? Ni kulizwa tu
 

CCM vs UKAWA
 

mfungwa na raia
 

Attachments

  • 1436272749108.jpg
    26.3 KB · Views: 301
  • 1436272772939.jpg
    29.7 KB · Views: 288
safi sana ! umeandika kikakamavu sana !
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…