Mradi usioeleweka Mwanza

Choosen85

JF-Expert Member
Jun 22, 2022
562
1,363
Wakuu kuna rafiki yangu alikuwa anafanya kazi mkoani Mbeya sasa alipigiwa simu na kaka ake kwamba kuna mradi upo Mwanza huko atalipwa vizuri sana.

Huyo kaka mtu akamwambia anatakiwa awe na passport ya kusafiria, achome chanjo ya manjano jamaa akapambana akakopa mpk kwa jamaa zake ili akamilishe hayo mambo maana ndugu yake alimwambia vinahitajika haraka sana. Na siku si nyingi anatakiwa akaripoti huko mwanza tyr kwa kazi.

Jamaa mkataba wa kazi ulipoisha huko Mbeya hakuongeza mkataba zaidi alifunga safari kwenda Mwanza akafikia kwa rafiki yake wakati akisubiri kuanza kazi huku akiwa kauza kila kitu alichokuwa nacho Mbeya. Huo mradi ofisi zao zipo maeneo ya Mecco Mwanza inasemekana eti ni mradi wa mgodi wa madini pia mambo ya watoto na wamama pia mambo ya ukimwi.

Cha ajabu toka mwaka 2019 mpaka leo hii jamaa hao hapo ofisini wamekuwa wakitoa taarifa zisizoeleweka kabisa jamaa anateseka sana anajuta kutoongeza mkataba huko alikotoka kwani huo mradi hapo Mwanza miaka inakatika hakuna jipya zaidi ya sound tu mara waambiwe kuna hela za makabiziano mara kuna hela za uzinduzi wa mradi mara kuna magari ya mradi yapo Mombasa yaani ni ujinga ujinga tu hakuna cha maana.

Mara waambiwe siku fulani watakuwa wamewekewa pesa kwenye akaunti zao siku ikifika kinatafutwa kisingzio hapo inapita miezi tena jamaa ni mwaka wa tatu anateseka huko Mwanza kashaomba msaada kwa jamaa zake mpaka wamemchoka anaona aibu hata kurudi Mbeya.

WAKUU MLIOKO MAENEO YA MEKO MWANZA HAPO JE NI KWELI KUNA KUNDI LA WATU HUWA WANAONEKANA HUKO AU MITAA HIYO WAKISUBIRI KUANZA KWA MRADI HUO MIAKA NENDA RUDI. TUONE ABC za kinachoendelea hapo maana nasikia wengine walichomwa chanjo ya covid kwa lazima ili tu wawe kwenye mradi.
 
Miaka mitatu yote anasubiri mradi hewa ambao haujulikani utaanza lini au ndo mambo ya Qnet,uyo kaka ake nae hana huruma kbsa,so anafanya nini now?kwanini asirudi mbeya kama anateseka uko
 
Mgodi mixer huduma za watoto na kina mama mixer ukimwi dah!, hii ni kachumbali hakuna Mgodi wa hivyo
Mwambie rafiki yako yeye ndio mgodi/mradi
 
Kuna Mradi mwingine wa chanjo wa Kichocho kwa watoto wa shule za msingi umepita huko nasikia umesimamiwa na walimu wa shule hizo, sikuuelewa...labda habari fake za mitandaoni!!!
 
Wakuu kuna rafiki yangu alikuwa anafanya kazi mkoani Mbeya sasa alipigiwa simu na kaka ake kwamba kuna mradi upo Mwanza huko atalipwa vizuri sana.

Huyo kaka mtu akamwambia anatakiwa awe na passport ya kusafiria, achome chanjo ya manjano jamaa akapambana akakopa mpk kwa jamaa zake ili akamilishe hayo mambo maana ndugu yake alimwambia vinahitajika haraka sana. Na siku si nyingi anatakiwa akaripoti huko mwanza tyr kwa kazi.

Jamaa mkataba wa kazi ulipoisha huko Mbeya hakuongeza mkataba zaidi alifunga safari kwenda Mwanza akafikia kwa rafiki yake wakati akisubiri kuanza kazi huku akiwa kauza kila kitu alichokuwa nacho Mbeya. Huo mradi ofisi zao zipo maeneo ya Mecco Mwanza inasemekana eti ni mradi wa mgodi wa madini pia mambo ya watoto na wamama pia mambo ya ukimwi.

Cha ajabu toka mwaka 2019 mpaka leo hii jamaa hao hapo ofisini wamekuwa wakitoa taarifa zisizoeleweka kabisa jamaa anateseka sana anajuta kutoongeza mkataba huko alikotoka kwani huo mradi hapo Mwanza miaka inakatika hakuna jipya zaidi ya sound tu mara waambiwe kuna hela za makabiziano mara kuna hela za uzinduzi wa mradi mara kuna magari ya mradi yapo Mombasa yaani ni ujinga ujinga tu hakuna cha maana.

Mara waambiwe siku fulani watakuwa wamewekewa pesa kwenye akaunti zao siku ikifika kinatafutwa kisingzio hapo inapita miezi tena jamaa ni mwaka wa tatu anateseka huko Mwanza kashaomba msaada kwa jamaa zake mpaka wamemchoka anaona aibu hata kurudi Mbeya.

WAKUU MLIOKO MAENEO YA MEKO MWANZA HAPO JE NI KWELI KUNA KUNDI LA WATU HUWA WANAONEKANA HUKO AU MITAA HIYO WAKISUBIRI KUANZA KWA MRADI HUO MIAKA NENDA RUDI. TUONE ABC za kinachoendelea hapo maana nasikia wengine walichomwa chanjo ya covid kwa lazima ili tu wawe kwenye mradi.
Kuna miradi bubu ya Magufuli mingi tu huko Morogoro nk. Alikuwa haramia kweli kweli.
 
Mwambieni aondoke zake tuu akatafute maisha hajionei huruma kupoteza miaka mitatu bure
 
Back
Top Bottom