Mpya: Tume ya Rais ya EPA yalonga

Kama ni za EPA ambazo zasemekana Zimeibiwa au Kuhujumiwa kwa kuundiwa makampuni ya mifukoni, je ni hatua gani za kisheria zitafuata?

Mchungaji, yaani hatua za kisheria zifuate baada ya makosa kusahihishwa? Hivi tunajua kuwa makosa yamefanyika na yana ushahidi kuwa yamefanyika? Kwanini mkondo wa sheria usianze kwanza? Mimi naona wamejaribu kuweka mkokoteni mbele halafu farasi nyuma! sasa yupi anamvuta yupi..

izi za CIS, mikopo inarudishwa baada ya zaidi ya miaka 10. Je wakopaji hawa wataruhusiwa kukopa tena? Je BOT na Hazina zitahakikisha vipi kuwa hawa default borrowers do not receive a positive credit rating for future loans from any financial institution? who will give them a guarantee?

Kama hawa watu walikopa, terms and conditions zilikuwa vipi? Maana kuwataka warudishe mikopo kama muda wake haujaisha inaweza kuingilia biashara za watu. Kama walitakiwa kuwa wamekwishalipa hadi hivi sasa ni jitihada gani zilifanyika kuwadai? Kama DAWASA waliweza kulikatia jeshi maji kwa kisingizio cha kudai deni, leo kwanini wanashindwa kuwakatia mitaji hawa wote?

Hata hivyo katika hayo mawili ni upande mmoja tu umeonesha kuna uhalifu umefanyika; uhalifu ambao Rais wa Jamhuri ya Muungano anajua umefanyika lakini ameamua kukwepa kuushughulikia na badala yake anatumia njia ya kidiplomasia.

Hivi kama kutokana na fedha za EPA nilifanikiwa kujenga nyumba za kupanga ishirini. Kamati ya Rais inapokuja na kuzungumza nami nakubaliana nao na kuwaambia kuwa basi nitaresha 10 kati ya hizo kwa moyo mnyofu na kuonesha uzalendo. Wale watu wa Kamati wakawatangazia wananchi kuwa "mmoja wa wahusika arejesha nyumba zilizotokana na akaunti ya EPA" itakuwa imesema uongo?

Sasa hawa wanarudisha fedha na mali sawa; zote? na wanapimaje...
 
Nadhani tumesahau nini Rais aliagiza. Ngoja niwakumbushe kidogo.

4. Rais amewaagiza; Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Inspekta Jenerali wa Polisi na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, kuchunguza na kuchukua hatua zipasazo za kisheria kwa makampuni na watu waliohusika na uhalifu huu. Rais amewataka watumie ipasavyo mamlaka na madaraka waliyo nayo kwa mujibu wa sheria. Aidha, amewataka wakamilishe kazi hiyo katika kipindi cha miezi sita.

Amemuagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali awe kiongozi wa kazi hii.

Amewataka wahakikishe kuwa fedha zilizolipwa isivyo halali zinarudishwa.


- Sasa kwa mujibu wa taarifa ya Rais ni kuwa kilichofanyika ni uhalifu na ushahidi wa uhalifu huo wao Ikulu wanao ndiyo maana wamezeza kusema pasipo kujiuma kuwa kilichofanyika ni "Uhalifu" na siyo "kupitiwa, kusahau, bahati mbaya, ajali" n.k

- Sasa kama kilichofanyika ni "Uhalifu" basi kinachotakiwa hapo siyo kuundwa Kamati au tume yenye wajumbe kadhaa; kinachofanyika ni "kuamuru kukamatwa kwa wamiliki wote wa makampuni haya, na kufikishwa mahakamani mara moja ili wajibu tuhuma mbalimbali dhidi yao."

- Baada ya kukamatwa Rais angemuagiza "Mwanasheria Mkuu kusimamia kesi dhidi ya watuhumiwa hawa ili kuhakikisha kuwa adhabu ya juu kabisa dhidi yao inapatikana.

- Kuagiza mkuu wa uchunguzi wa Makosa ya Jinai, kuanzisha uchunguzi wa kihalifu mara moja ili kujua kina, upana, n.k wa uhalifu huu. Kufikia lengo hilo DCI atapewa ushirikiano na Taasisi ya Scotland Yard na FBI (Financial Crime Unit)ili kuweza kupata ushirikiano wa kitaalamu.

- Ametoa ombi rasmi kwa Interpol kuwaweka watu wafuatao katika rada zao, Jeetu Patel n.k ili wakamatwe na kurudishwa nchini kujibu mashtaka.

Rais hakufanya hayo yote; asingeweza kutoa amri za namna hiyo!! Usiniulize kwanini.

Hayo uulizayo na usemayo kwanini, huo ni udikteta na umepitwa na wakati kwa Tanzania.

Na kwa mfano angefanya kama usemavyo wewe, ungekuja na hoja kuwa JK "dikteta" anaamrisha watu wakamatwe hovyo, watu kama nyinyi tunawajua huwa hamkosi la kumpakazia mtu. Mema hamuoni kwa chuki tu na si kama hayafanyiki. Kesha toa amri hiyo uliyoinukuu hapo juu, sasa ngoja uone ikipita muda aliotoa sheria zinachukua mkondo au la. Jikumbushe kwa kamati aliyoiunda ya Zombe, si ilichunguza kwa muda waliopewa? na baada ya hapo si wamepeleka uchunguzi wao, na sasa Zombe yuko wapi? Nna uhakika jibu unalo, kwa hiyo punguza jazba na ngoja muda ufike.
 
Hayo uulizayo na usemayo kwanini, huo ni udikteta na umepitwa na wakati kwa Tanzania.

Na kwa mfano angefanya kama usemavyo wewe, ungekuja na hoja kuwa JK "dikteta" anaamrisha watu wakamatwe hovyo, watu kama nyinyi tunawajua huwa hamkosi

mnawajua na nani..... huu wingi umeanza leo au ndiyo kazi yako hapa ya kuwakilisha watu usiowataja?

la kumpakazia mtu. Mema hamuoni kwa chuki tu na si kama hayafanyiki. Kesha toa amri hiyo uliyoinukuu hapo juu, sasa ngoja uone ikipita muda aliotoa sheria zinachukua mkondo au la. Jikumbushe kwa kamati aliyoiunda ya Zombe, si ilichunguza kwa muda waliopewa? na baada ya hapo si wamepeleka uchunguzi wao, na sasa Zombe yuko wapi? Nna uhakika jibu unalo, kwa hiyo punguza jazba na ngoja muda ufike.

Kati ya hoja za mwanakijiji na ulichoandika hapa, ni wapi kuna jazba? watu wengine sijui wanakunywa nini kabla ya kuandika comments hapa! grrrrrrr utetezi wa mafisadi hata hujui unachoandika?
 
mnawajua na nani..... huu wingi umeanza leo au ndiyo kazi yako hapa ya kuwakilisha watu usiowataja?



Kati ya hoja za mwanakijiji na ulichoandika hapa, ni wapi kuna jazba? watu wengine sijui wanakunywa nini kabla ya kuandika comments hapa! grrrrrrr utetezi wa mafisadi hata hujui unachoandika?

Ha hahahahaha ha, hauna hoja.
 
Hayo uulizayo na usemayo kwanini, huo ni udikteta na umepitwa na wakati kwa Tanzania.

Na kwa mfano angefanya kama usemavyo wewe, ungekuja na hoja kuwa JK "dikteta" anaamrisha watu wakamatwe hovyo,

Uwe unafikiria unapoandika; serikali ya nani ilifanya uchunguzi wa EPA? serikali ya nani iliyotambua kuwa fedha zaidi ya bilioni 133 zimechotwa kimtindo? na ni serikali ya nani iliyosema kilichofanyika ni uhalifu? Kama ni serikali hiyo hiyo na ikaamua kuwakamata wahalifu itakuwaje tena iwakamate "hovyo"? grrrrrr! Kukamata watu ovyo ni kama walivyowakamata vijana wa JF yaani mtu anakurupuka tu kwa vile leo anajisikia kumkamata mwanakijiji basi anamtia pingu na hamfikishi mahakamani na wala hana sababu! fikiri kabla ya kuanza kudonyoa hiyo keyboard.


watu kama nyinyi tunawajua huwa hamkosi la kumpakazia mtu. Mema hamuoni kwa chuki tu na si kama hayafanyiki. Kesha toa amri hiyo uliyoinukuu hapo juu, sasa ngoja uone ikipita muda aliotoa sheria zinachukua mkondo au la. Jikumbushe kwa kamati aliyoiunda ya Zombe, si ilichunguza kwa muda waliopewa? na baada ya hapo si wamepeleka uchunguzi wao, na sasa Zombe yuko wapi? Nna uhakika jibu unalo, kwa hiyo punguza jazba na ngoja muda ufike.


sasa kama uhalifu unachunguzwa na Kamati na kwa vile Kamati ya Zombe nayo ilifanya kazi yake basi ndio mtindo mpya wa kusimamia sheria nchini, si mlivunje jeshi la Polisi na muanzishe "Kamati za Rais za Kipolisi za Mkoa" ambazo ndani yake mnaweza kutengeneza Kamati nyingine ndogondogo kama "Kamati ya Upepelezi", "Kamati ya Kuzuia Fujo", na "Kamati ya Usalama Barabarani"?
 
umeshikwa pabaya mkuu utaishia kucheka cheka hapa baada ya kugundua kazi ya kutetea mafisadi sio rahisi kama ulivyozani

Ila anajitahidi sana, tatizo ni kama jitihada za "yule aliyeombewa aenende akawe mkuu wa mafisadi" anavyojaribu kujitetea na kwa kadiri anavyozungumza ndivyo anavyothibitisha kuwa alikuwa fisadi!
 
Uwe unafikiria unapoandika; serikali ya nani ilifanya uchunguzi wa EPA? serikali ya nani iliyotambua kuwa fedha zaidi ya bilioni 133 zimechotwa kimtindo? na ni serikali ya nani iliyosema kilichofanyika ni uhalifu? Kama ni serikali hiyo hiyo na ikaamua kuwakamata wahalifu itakuwaje tena iwakamate "hovyo"? grrrrrr! Kukamata watu ovyo ni kama walivyowakamata vijana wa JF yaani mtu anakurupuka tu kwa vile leo anajisikia kumkamata mwanakijiji basi anamtia pingu na hamfikishi mahakamani na wala hana sababu! fikiri kabla ya kuanza kudonyoa hiyo keyboard.





sasa kama uhalifu unachunguzwa na Kamati na kwa vile Kamati ya Zombe nayo ilifanya kazi yake basi ndio mtindo mpya wa kusimamia sheria nchini, si mlivunje jeshi la Polisi na muanzishe "Kamati za Rais za Kipolisi za Mkoa" ambazo ndani yake mnaweza kutengeneza Kamati nyingine ndogondogo kama "Kamati ya Upepelezi", "Kamati ya Kuzuia Fujo", na "Kamati ya Usalama Barabarani"?

Na wale earnest and young uliwaajiri wewe?
 
Ila anajitahidi sana, tatizo ni kama jitihada za "yule aliyeombewa aenende akawe mkuu wa mafisadi" anavyojaribu kujitetea na kwa kadiri anavyozungumza ndivyo anavyothibitisha kuwa alikuwa fisadi!

Pole sana naona bado unauchungu wa kiteto.

Halagu unajitahidi kwa kuandika na kujijibu mwenyewe.
 
Ila anajitahidi sana, tatizo ni kama jitihada za "yule aliyeombewa aenende akawe mkuu wa mafisadi" anavyojaribu kujitetea na kwa kadiri anavyozungumza ndivyo anavyothibitisha kuwa alikuwa fisadi!

Yaani utawaweza,

hakusubiri hata afikishe post 20 ili aanze ufisadi!?!

mimi nashuhudia explosion tu hapa.... maana the first posts tu huyo kishaanza ohhh walongalongaji... mara mwanakijiji ndiye mwafrika wa kike ili mradi explosions tu! grrrrrrrrr
 
Yaani utawaweza,

hakusubiri hata afikishe post 20 ili aanze ufisadi!?!

mimi nashuhudia explosion tu hapa.... maana the first posts tu huyo kishaanza ohhh walongalongaji... mara mwanakijiji ndiye mwafrika wa kike ili mradi explosions tu! grrrrrrrrr

Vipi, mbona unafoka kama...
 
Usanii mwingine hata unavuka maelezo ya kawaida. Yaani ni lini sheria za nchi zilibadilishwa na kuruhusu watuhumiwa wa wizi kurudisha mali na sio kupelekwa kwenye vyombo vya sheria.

Ina maana leo wale watuhumiwa wa wizi wa kuku na simu walioko Keko wanaruhusiwa kuachiwa huru as longer as wanarudisha kile walichoiba?

MWK, Sheria ilibadilishwa na mafisadi waliopeana ruhusa ya kukupua mali za Watanzania kila kona ya Tanzania. Walikubaliana kwamba watakaposhtukiwa kama wanaiba na kusaini mikataba mibovu basi wakirudisha walichokipata karika ufisadi wao mambo yote yatakuwa shwari.

Huu ni usanii wa hali ya juu, wabunge wa CCM wangechachamaa wahusika wote wa kashfa ya EPA, Richmond n.k. waswekwe rumande wakati uchunguzi unaendelea basi nina hakika hilo lingetokea.

Wabunge wamebwabwaja hakuna chochote kilichofanyika watuhumiwa wote bado wako huru wakiendelea kufaidi mapesa yao ya ufisadi.

Nilishangaa kusikia bunge limeahirishwa hadi April. Mtaahirishaje bunge wakati nchi imegubikwa na kashfa nzito nzito chungu nzima, kwani wasingeweza kuitisha kikao cha dharura cha bunge hata cha mwezi mmoja ili kuhakikisha watuhumiwa wote wanaswekwa ndani!? Usanii kila kona, halafu Chiligati atakwambia wao CCM ndio waliwawajibisha mafisadi! wakati bado wako uraiani wanapeta!
 
kuna ushahidi gani wa kuwa fedha zimerejeshwa iwapo hatutoambiwa ni nani ameiba fedha gani na amerudisha ngapi?

tutawezaje kupiga simu kuwapa maelezo zaidi pamoja na mali za wizi wa EPA iwapo hatutatajiwa hizo kampuni zinamilikiwa na nani ?

hizi sio bangi tu....ni bangi mbichi na njaa!!!
 
Seems like a premeditated game, aimed at fooling Tanzanians and rallying support which now seems to have been lost. How can my Mama in bombambili know these people, they have to tell us who they are and then we can help them to get them.
Ripoti ya EPA imetaja majina yao na wanayo, sasa kuwauliza watanzania au kutupa namba za simu tuwaambia maana yake nini? Wakitaka msaada kwentu kwanza watupe ripoti ya EPA halafu tuone majina yote na ndio tuwasaidie kuwapeleka hao jamaa! Inaonekana kama usanii fulani!
 
Back
Top Bottom