Mpira Umekosa Ladha

Mpira Umekosa Ladha

juve2020 ndio maana wakubwa wa UEFA kwa kuliona hili wanataka ku impose financial rules kwamba vilabu viiendeshe ndani ya uwezo wao,of course matajiri kina Abramovich nao wanakuna vichwa wakitafuta namna ya kufanya usanii (financial engineering) ili wakwepe madhara ya kanuni hii,ngoja tuone maana itaanza kuwa effective 2015 kama sikosei.

Na hii ndio dawa. Hakuna balance of power, timu zinatumia nguvu ya fedha na hakuna anayejali ukuzaji wa vipaji. Timu inayothubutu ku-invest kwenye ukuzaji wa vipaji haiwezi kushindana na timu zinazonunua ushindi. Arsenal imeumia kwa mtindo huo. Dawa ni hiyo FF Rule
 
Teh teh teh!kwa kuwa vibonde wako wa uingereza wametolewa!!

Wachezaji wa maana huwa hawachezi ligi ya Uingereza - waliotajwa hapo juu sio kwamba hawakuwahi kucheza Uingereza tu ila pia walizigalagaza timu za Uingereza; Redondo tobo lake Man U hawatalisahau, pia hawatasahau hat trick ya Ronaldo na alichowafanya Ronaldinho kwa kisigino!
 
We Gutierez hebu ifike kipindi uwe na staha...maana naona unae kila kona ndugu yangu Juve2012
Alininyima raha kule Turati na kuanika namba yangu ya simu hadi wanaonidai ikawa kero,ila sorry natonesha donda
 
haya bwana,dah!hii yote Calciopoli ndio imetufikisha hapa.kama Juve ya akina ibra ingebakia serie a nakuambia usingekuwa unanipa pole saa hizi.tuna miaka mitano mbele ya kurudi tulipokuwa.ila uchumi unachangia sana tofauti ya soka leo.sijui italia ikifilisika wengine tutafanyaje!
Hahahaha pole no comments,usikose fainali UCL in avdance El Classico tarehe 25 May@Wembley London
 
Wanaitwa SS Lazio Roma...
1. Peruzzi
2. Paolo Negro
3. Sinisa Mihajlovic
4. Fernando Couto
5. Alesandro Nesta
6. Diego Simeone
7. Claudio Lopez
8. Juan Sebastian Veron....

Soka lilikuwa miaka ile Mungu hajaondoka Duniani...
Huyu Sinisa Mihajlovic alikuwa bingwa wa mipira iliyokufa yeye na Juninho Pernambucarno,Beckham anasubiri
 
Mnajiumiza roho soka sasa lipo Spain likiongozwa na FC Barcelona
 
Wanaitwa SS Lazio Roma...
1. Peruzzi
2. Paolo Negro
3. Sinisa Mihajlovic
4. Fernando Couto
5. Alesandro Nesta
6. Diego Simeone
7. Claudio Lopez
8. Juan Sebastian Veron....

Soka lilikuwa miaka ile Mungu hajaondoka Duniani...

uuwii!hivi list hii nyasi hazikuwa zinazungumza uwanjani kweli?ndio maana viwanja vya zamani viliota vipara mapema na hasa kwenye 18 yard box!sio siku hizi nyasi hata hazichoki bwana!
 
Sio mpira wa nje tu ata huu wetu kwisha..enzi zile ukisikia Tp lindanda Pamba..Paul rwechungula...david mwakalebela..abdallah bori..george masatu..khalfan ngassa..maonwa nkami...hussein masha..fumo felician...john makelele...etc mtangazaji dominic chillambo..rip..njoo mbeya mecco..tukuyu stars...coastal union..african stars...majimaji ya sikinde mbunga..nyota nyekundu etc...yaani TZ tulishindwa kuuza wachezaji kwenye ligi kubwa kipindi kile sijuhi ni lini tutawezakuwauza

edger Fongo,Said Zimbwe,Makumbi Juma "homa ya jiji",nicodemus mtekere,Sahau Kambi,juma Pondamali(awashukuru sana polisi maana mbwembwe zingemuua huyu siku ile mashabiki wangezaa nae),Hassan Hafif(chloroquine ya Yanga),mau mkami.dah!GANG CHOMBA HOMA YA ILALA..teh teh.!
 
Katika drama za soka ambazo sitazisahau maishani ni siku ile sami kuffor anapigapiga ngumi chini huku akilia kwa uchungu baada ya babu Ferguson kuwafanyia kitu mbaya bayern ambayo kamwe hawataisahau.dk mbili za nyongeza,sub mbili kaingiza,magoli mawili na ndoo mkononi!nyingine ilikuwa mechi ya deportivo na psg ya akina Okocha.hadi zimebakia dk saba mpira kuisha psg wanaongoza 3-1.depo wakamuingiza sub mmoja anaitwa Walter Pandiani.hadi mpira unaisha deportivo waliondoka na ushindi wa goli 4-3!walipata kona tatu,zote Pandiani aliziunganisha wavuni kwa vichwa!Okocha hakuamini macho yake!
 
Katika drama za soka ambazo sitazisahau maishani ni siku ile sami kuffor anapigapiga ngumi chini huku akilia kwa uchungu baada ya babu Ferguson kuwafanyia kitu mbaya bayern ambayo kamwe hawataisahau.dk mbili za nyongeza,sub mbili kaingiza,magoli mawili na ndoo mkononi!nyingine ilikuwa mechi ya deportivo na psg ya akina Okocha.hadi zimebakia dk saba mpira kuisha psg wanaongoza 3-1.depo wakamuingiza sub mmoja anaitwa Walter Pandiani.hadi mpira unaisha deportivo waliondoka na ushindi wa goli 4-3!walipata kona tatu,zote Pandiani aliziunganisha wavuni kwa vichwa!Okocha hakuamini macho yake!

na goli la kwanza la depo lilifungwa na sub mwingine Diego Tristan kwa kichwa pia!
 
Kilichotokea si kwamba wachezaji hawapo, bali fedha zimeharibu mpira. Nafasi ya timu zisizo na fedha kuonekana ni finyu kwa kuwa soka imekuwa monopolized na wenye fedha kiasi hakuna balance of power.

By the way, Messi juzi kamdhihirishia Gang Chomba kuwa ni yeye ndie anaibeba Barcelona kinyume na mdomo wa Gang wenye roho mbaya kiasi cha kusema bila Xavi na Iniesta Messi hafanyi kitu. Imedhihirika kuwa bila Messi, hakuna wa kuimalizia kazi ya Xavi na Iniesta hata wahangaike vipi.

Messi
Wilshere
Ronaldo
Lucas
Isco
Cazorla
Veranne

Vijana wapo, kilichoharibika mifumo


nicola Amoruso, Pavel Nedved, Nicola Ventola, Zvonimir Boban, Uncle Seedorf, Marcelo Salas, Sheva, Ivan Zamorano, Vieri, Nakata, Batistuta, Maestro Manuel Cesar Rui Costa, Alesandro del Piero, Trezeguet, Mauro German Camoranessi, Vicenzo Montella, Francesco Totti, Pippo Inzaghi, Danielle De Rossi, Tordo, Buffon, Dida, Peruzzi, usiku wa Nyota Demetrio Albertini...

Bwana weee soka limekwisha...
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom