Habari wanajamvi , kama kichwa cha uzi wangu kinavyosema , mimi ni kijana mvulana ambae nipo kwenye mahusiano na msichana wangu takribani miaka miwili sasa, kiukweli huyu msichana she is beautifull and very nice to me na ni mwaminifu kwangu lakini, kiukweli nampenda na ananipenda sana.
Shida ni moja toka naanza mahusiano nae mpenzi wangu huyu anatabia ya upole iliyopitiliza tofauti na mimi mwenyewe , mimi ni mtu mmoja mzungumzaji sana na ninayependa talks, na nikitu ambacho hata yeye anaenjoy kwangu coz namfanya kila mda anafurahi , mwanzo nilijitahidi kumchangamsha ili niende nae sawa lakini ilikuwa ngumu kubadilika.
Kiukweli naboreka sana na huu uhusiano though nampenda, my gf sio mtu ambae anaweza kuona nipo offmood kisha akanifanya nifurahi , she is not friendly yani kiukweli anabore ukiacha maswala ya mahusiano hakuna mambo mengine ya kijamii anaweza akazungumza nikafurahi, tukiwa wawili mi ndo the only person ambae nazungumza yeye ni mpenzi mtazamaji, unaweza ukakuta njia nzima nazungumza mimi au tukiwa chumbani usishangae kashika tama ananiangalia huku anatabasamu tu.
Sasa naamini kwenye mahusiano ili mpate kudumu ni lazima muwe na urafiki (watu ambao mna kitu zaidi ya mapenzi) sasa huyu mwenzangu ni msomi lakini anaonekana amekosa communication skills n social interaction na kiukweli nishazungumza nae sana ili nimbadilishe lakini jibu lake ni moja kuwa hivo ndivo alivyozaliwa na malezi ya utotoni ndio yamemfanya awe hivo plus na shughuli zake anazofanya zinamfanya akose social interaction
Sasa kiukweli mimi ndugu zangu nahisi kuchoka na hii hali coz imefikia kipindi nakuwa bored sana yani sometimes hata akipiga simu najisikia uvivu kupokea yani kama somo nimeshaelekeza lakini mwenzangu ndo imeshindikana kubadilika , imefikia kipindi natumia mda wangu mwingi na washkaji zangu na rafiki zangu wengine wakike na naenjoy zaidi kuliko nikikaa na mpenzi wangu , naombeni ushauri wenu wakuu kipi cha kufanya hapa ili nijenge kuliko kubomoa coz napata wazo la kumuacha ila nashindwa coz kiukweli nampenda and she is so loyal to me sema ndo vile no enjoyment kabisa kwenye uhusiano.
View attachment 585321