Mpenzi wangu sio rafiki

Mpenzi wangu sio rafiki

Habari wanajamvi , kama kichwa cha uzi wangu kinavyosema , mimi ni kijana mvulana ambae nipo kwenye mahusiano na msichana wangu takribani miaka miwili sasa, kiukweli huyu msichana she is beautifull and very nice to me na ni mwaminifu kwangu lakini, kiukweli nampenda na ananipenda sana.

Shida ni moja toka naanza mahusiano nae mpenzi wangu huyu anatabia ya upole iliyopitiliza tofauti na mimi mwenyewe , mimi ni mtu mmoja mzungumzaji sana na ninayependa talks, na nikitu ambacho hata yeye anaenjoy kwangu coz namfanya kila mda anafurahi , mwanzo nilijitahidi kumchangamsha ili niende nae sawa lakini ilikuwa ngumu kubadilika.

Kiukweli naboreka sana na huu uhusiano though nampenda, my gf sio mtu ambae anaweza kuona nipo offmood kisha akanifanya nifurahi , she is not friendly yani kiukweli anabore ukiacha maswala ya mahusiano hakuna mambo mengine ya kijamii anaweza akazungumza nikafurahi, tukiwa wawili mi ndo the only person ambae nazungumza yeye ni mpenzi mtazamaji, unaweza ukakuta njia nzima nazungumza mimi au tukiwa chumbani usishangae kashika tama ananiangalia huku anatabasamu tu.

Sasa naamini kwenye mahusiano ili mpate kudumu ni lazima muwe na urafiki (watu ambao mna kitu zaidi ya mapenzi) sasa huyu mwenzangu ni msomi lakini anaonekana amekosa communication skills n social interaction na kiukweli nishazungumza nae sana ili nimbadilishe lakini jibu lake ni moja kuwa hivo ndivo alivyozaliwa na malezi ya utotoni ndio yamemfanya awe hivo plus na shughuli zake anazofanya zinamfanya akose social interaction

Sasa kiukweli mimi ndugu zangu nahisi kuchoka na hii hali coz imefikia kipindi nakuwa bored sana yani sometimes hata akipiga simu najisikia uvivu kupokea yani kama somo nimeshaelekeza lakini mwenzangu ndo imeshindikana kubadilika , imefikia kipindi natumia mda wangu mwingi na washkaji zangu na rafiki zangu wengine wakike na naenjoy zaidi kuliko nikikaa na mpenzi wangu , naombeni ushauri wenu wakuu kipi cha kufanya hapa ili nijenge kuliko kubomoa coz napata wazo la kumuacha ila nashindwa coz kiukweli nampenda and she is so loyal to me sema ndo vile no enjoyment kabisa kwenye uhusiano.

View attachment 585321
Mmmh pengene unaongea sana, yani humpi nafasi na yeye ya kuzungumza, coz hata mimi nikikaa na mtu anaongea kama chiriku huwa nanyamaza tu namuangalia.
Ushauri uwe unaongea kwa kiasi na yeye umpe nafasi ataongea...
 
Daah hiyo fursa nilikuwa naitafuta siku nyingi embu nipe namba yake kwa maana na mimi nina tabia kama yake, nadhani tutaendana nae au vipi
hahaha mkuu nilikuwa nina jibu kama lako,nimekosa cha kuandika. Hahaha ama kweli penye miti hapana wajenzi
 
Ukiona hajawahi hata kujamba mbele yako..hilo ni tatizo ndugu yangu,anakuficha mengi
 
Ukisikia utaishi nae kwenye shida na Raha, Ndio hii sasa chukulia udhaif wake km unavoona lkn sio kumuacha na uendelee nae, kumkimbia sio njia, unaeza kutana na mwnign ukajuta kuzaliwa ukaona afadhal huyo,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom