Mpenzi wangu ni mbinafsi sana

Mpenzi wangu ni mbinafsi sana

Hiyo ni roho mbaya iliyokithiri, anashindwa kukusaidia hata elfu30 tu na wewe ni mpenzi wake?

Angalia upya hayo mahusiano yenu mkuu
 
Kama mtu mnauhusiano Kwa miaka minne na Huwa unamsaidia hata angekua rafiki tu achilia mbali mpenzi na anajua unashida Hawezi shindwa kukusaidia.
Unaweza kuta ulisaidiwa hiyo 30,000 na marafiki mpenzi wako kakataa kukusaidia Akiwa nayo.
Huyo hafai kuwa mpenzi mintarafu mke hata kuwa rafiki tu hafai. Kuwa na mahusiano Na mtu asie na hisia na Wewe ni jambo Baya sana.
Unawezaje kuona mtu unaempenda anashida na unaweza kuitatua Ukaacha ateseke? Hapo Hakuna mapenzi Kuna biashara inaendelea ukifumbua macho vizuri Na masikio utaitambua.
 
Kama miaka 4 ya mahusiano yuko ivyo ujue hiyo ndiyo tabia yake na kubadilika kamwe haiwezekani

Ukiamua kuendelea nae jiandae kisaikolojia mkuu
 
Ukiweza suka mpango wa kumpima.Ujifanye umefulia na huduma zote ukate na umwombe hela ndogo ndogo max 50k kwa ajili ya matibabu n.k.Hata akija nyumbani aone kweli mambo magumu, kama ni friji ni tupu n.k

Mpime uone atareact vipi.
Umenena vyema
 
1.Kakuloga
2.jiangalie juu mpaka chini kisa uje useme nimekosa nini natembea na kikaragosi .
3.ukishapata jibu.
4.Kaombewe kwamaana huyo ni pepo chafu kabisa lisilonahaya limekuzoea na nilizimwi likujualo.
Mapenzi my foot ilikuaa secondary mama upo kimjini unasaka tonge so usiwe na stress zozote kama unajiweza .
Tafuta mwanaume wa nguvu.
Akuongezee mlo sio ajibweteke.
Fukuza hilo lipaka shume ukaoge na maji ya chumvi osterbay.
Soma vizuri huyo ni mwanaume
 
Dah kanikeraaaaaa watu wengine ni wachoyo by nature, wanapenda kutumia vya wengine, vya kwao visiguswe.
Mm roho yangu ya huruma ndio inaniponzaga Siku zote, MF. Mpz / rafiki tu aniombe hela siwezi mwambia hata kama sina naanza kujaribu kukopa kwa mashoga zangu labda hata huko nukose ndo ntaweza kumwambia sina,

Ingawa huwa Nina mkosi wa pesa yaani ikitokea nikakosa pesa nikamkopea MTU hata kwenye chama hili arudishe, huwa hawanirudishiagi na ikitokea bahati mbaya akarudisha basi ntakuwa nishabebeleza mwaka mzima, ntarejesha hiyo hela mwanzo mwisho loh!

Mleta Mada huyo Dada ndani ya hiyo miaka 4 kama hajawahi kukusaidia wakati wa shida, nakuhakikishia hawezi kubadilika, tena ukimuoa ndio kabisaaaa.

Labda nijue kitu kimoja, huwa anakununuliaga hata zawadi? Kama yeye kwake hakunaga -, kwake + tu achana nae, bora MTU akunyime kitu ujue hana ila unajua na anayo kakunyima? Loh.

Nb. Ukiona hupewi wewe jua kuna mwenzio anapewa hii ni kwa jinsia zote.
Bas we ndo mm shoga yangu yan nna huruma mm
 
Hizo ni tabia za wanawake karibu wote, they are taking advantage, selfish and hawana shukrani.
Usiseme wanawake karibia wote unakosea sana, wakati wengine wanawake ndiyo wajenzi wa uchumi kwa wapenzi wao
 
Wewe baada ya kufika dar gari usingeweka mafuta, halafu nyumbani hakuna kununua kitu unamwambia mimi nakula kwa bill kwa mama lishe mtaani uone atafanya nini, na muone wakawaida, miaka 4 usijue uhitaji wa mwenzie huna mtarajiwa mke hapo
 
Habari wakuuuu, na changamoto kidogo na mpenzi wangu, nimekuwa nae kwa mahusiano Kama miaka minne ivi mpaka Sasa, time naanza nae mahusiano alinikuta Niko vizuri kiuchumi, kifupi nilikuwa namgharamia Kama ambavyo mwanaume upaswa kumjali mpenzi wake kwa kila kitu, Hali ya kwamba uyo mpenzi wangu Ni muajiliwa serikalini Tena kazi nzuri tu na mshaara wake Ni zaidi ya Million. Katikati apa mipango yangu imeyumba kidogo, nikamuomba aniazime pesa kidogo ambayo nitaongezea kwenye Kodi ya nyumba ambayo hata yeye uwa anafikia akija Dar, kwakuwa kituo chake Cha kazi Ni nje ya Dar, akanijibu Hana pesa wakati najua kwenye account yake mpaka kiwango alicho nacho, Tena kwenye Kodi nilipungukiwa laki mbili tu kwa kwa maaana nilikuwa na million Moja na laki sita yeye aniongezeee laki mbili tu, akadai Hana pesa, dahhh nikaona isiwe tabu nikaongea na mwenye nyumba, Ana nieshimu namieshimu kanielewa Sana na kumbe wasi wasi wangu tu. Baaada ya kulipa iyo Kodi nikawa mweupe Sina hata senti, kwakuwa na miradi yangu mikubwa nje ya mkoa wa Dar nayo ikawa imekaaa vyema ivyo ikanibidi nauli tu niende uko Mkoani nikamuomba elfu 30 tu akanijibu Sina na kuniambia unadhani kila mda Mimi na pesa tu, wakati najua mshaara wake na najua kwenye account Ana kiwango gani??
Nikafanya yangu Mimi nikaenda Mkoani, kaja Dar kafikia kwenye nyumba ile ile aliyogoma kuniazima laki mbili ya Kodi, gari yangu anatumia na mafuta naweka Mimi, chakula changu anakula, starehee naampa, pesa ya matumizi naampa nikikwama yeye mgumu, nampenda ila rohoo ya kumuacha inanijia kwakuwa uyu naona Ni mbinafsi wa kiwango Cha lami....nimfanyeje uyu kiumbe Kama namchoka ivi.

MJINGA KWELI, UNACHOLALAMIKA NINI BAADA YA KUCHUKUA HATUA? NYIE NDIO MNAKUWA WAKARIBU MNATUMIKA MPAKA MNAFILISIWA MNAKUJA KUJIUA, SI UMUACHE?
 
Back
Top Bottom