Kwa hili jibu huendi mbingunikwanza wacha uzinzi halafu ndo nikushauri
RafikiRafiki!![]()
aachane naye kabisa.Hicho unachowaza kufanya ni sahihi.Tumia akili, weka hisia pembeni.Ukitaka kumwua kima usimwangalie usoni.
Pole sana mkuu.
mwache mara moja.Thanks mkuu....nashukuru
hao viumbe wanajijua wenyeweHizo ni tabia za wanawake karibu wote, they are taking advantage, selfish and hawana shukrani.
Wewe unafaa sana hata kuwekwa ndani, kwan umeshaolewa LuckylineDah kanikeraaaaaa watu wengine ni wachoyo by nature, wanapenda kutumia vya wengine, vya kwao visiguswe.
Mm roho yangu ya huruma ndio inaniponzaga Siku zote, MF. Mpz / rafiki tu aniombe hela siwezi mwambia hata kama sina naanza kujaribu kukopa kwa mashoga zangu labda hata huko nukose ndo ntaweza kumwambia sina,
Ingawa huwa Nina mkosi wa pesa yaani ikitokea nikakosa pesa nikamkopea MTU hata kwenye chama hili arudishe, huwa hawanirudishiagi na ikitokea bahati mbaya akarudisha basi ntakuwa nishabebeleza mwaka mzima, ntarejesha hiyo hela mwanzo mwisho loh!
Mleta Mada huyo Dada ndani ya hiyo miaka 4 kama hajawahi kukusaidia wakati wa shida, nakuhakikishia hawezi kubadilika, tena ukimuoa ndio kabisaaaa.
Labda nijue kitu kimoja, huwa anakununuliaga hata zawadi? Kama yeye kwake hakunaga -, kwake + tu achana nae, bora MTU akunyime kitu ujue hana ila unajua na anayo kakunyima? Loh.
Nb. Ukiona hupewi wewe jua kuna mwenzio anapewa hii ni kwa jinsia zote.
Huu ni Ukweli Mchungu.
Kweli watu hawafanani kabisa. Nina mpenzi wangu tena ni dent tu wa chuo yaani anavyohangaika kuniridhisha na vizawadi vyake kwa kutegemea boom la chuo hadi namuonea huruma Daah!!
Mara Kaleta Boxer Mara T-shirt, Leo Saa Keshokutwa Raba...Daah
Kuna watu Tumebarikiwa Mno. Hadi Tukiambiwa Matatizo ya Wenzetu Hatuamini.
Wanawake wa kichanga ni wa aina gani hawa, jamani?Achana na wanawake wakichanga utakuja kufa bure!
😀Wewe unafaa sana hata kuwekwa ndani, kwan umeshaolewa Luckyline
Hakuna mapenzi kabisa. Anafanya home kwa jamaa kama sehemu ya kufikia (free guest house) akiwa mjini. Most likely ana mtu anayempenda huko mkoani kwake.Mbonaa unavutwa maskio km ngirii, huoni km yuko kwa ajili ya maslahi yake pole endelea hivyoo hivyoo kuwa saccos
Lakini akija Dar si unamgegeda?Habari wakuuuu, na changamoto kidogo na mpenzi wangu, nimekuwa nae kwa mahusiano Kama miaka minne ivi mpaka Sasa, time naanza nae mahusiano alinikuta Niko vizuri kiuchumi, kifupi nilikuwa namgharamia Kama ambavyo mwanaume upaswa kumjali mpenzi wake kwa kila kitu, Hali ya kwamba uyo mpenzi wangu Ni muajiliwa serikalini Tena kazi nzuri tu na mshaara wake Ni zaidi ya Million. Katikati apa mipango yangu imeyumba kidogo, nikamuomba aniazime pesa kidogo ambayo nitaongezea kwenye Kodi ya nyumba ambayo hata yeye uwa anafikia akija Dar, kwakuwa kituo chake Cha kazi Ni nje ya Dar, akanijibu Hana pesa wakati najua kwenye account yake mpaka kiwango alicho nacho, Tena kwenye Kodi nilipungukiwa laki mbili tu kwa kwa maaana nilikuwa na million Moja na laki sita yeye aniongezeee laki mbili tu, akadai Hana pesa, dahhh nikaona isiwe tabu nikaongea na mwenye nyumba, Ana nieshimu namieshimu kanielewa Sana na kumbe wasi wasi wangu tu. Baaada ya kulipa iyo Kodi nikawa mweupe Sina hata senti, kwakuwa na miradi yangu mikubwa nje ya mkoa wa Dar nayo ikawa imekaaa vyema ivyo ikanibidi nauli tu niende uko Mkoani nikamuomba elfu 30 tu akanijibu Sina na kuniambia unadhani kila mda Mimi na pesa tu, wakati najua mshaara wake na najua kwenye account Ana kiwango gani??
Nikafanya yangu Mimi nikaenda Mkoani, kaja Dar kafikia kwenye nyumba ile ile aliyogoma kuniazima laki mbili ya Kodi, gari yangu anatumia na mafuta naweka Mimi, chakula changu anakula, starehee naampa, pesa ya matumizi naampa nikikwama yeye mgumu, nampenda ila rohoo ya kumuacha inanijia kwakuwa uyu naona Ni mbinafsi wa kiwango Cha lami....nimfanyeje uyu kiumbe Kama namchoka ivi.