Mpenzi wangu kanipotezea, msaada wa mawazo tafadhali

Mpenzi wangu kanipotezea, msaada wa mawazo tafadhali

Kwa kuongezea alichosema MJUMBE HAPA......Dada angu dalili ya MVUA MAWINGU, na panapofuka moshi, jua chini kuna moto...Jitie ujasiri, muulize ujiridhishe baada ya hapo MTWANGE KIBUTI CHA UGOKO halafu ushike hamsini zako! Utazeeshwa halafu uachwe, mapenzi ya kupima kwa 'NAUTICAL MILES' mara nyingi mwisho wake ni kama huu.
ushaachwa wewe

cha kufanya, unfriend, then mblock kwenye fb

then kwenye simu yako mblock

nakutakia kuachwa kwema.....
 
jaribu na wewe kumrusha roho uone atajibu vipi?

tikisa dada uone kilichomo ndani..

MAPENZI YAMEINGILIWA NA MATAPELI SIKU HIZI!

Excel wengine hawabipiwi hivyo!! dada wa watu akiachwa je utampokea?
 
Last edited by a moderator:
Excel wengine hawabipiwi hivyo!! dada wa watu akiachwa je utampokea?

dah, wadada mna kazi kweli, mikosa lifanye limtu lingine tena makusudi.. aumie mwingine!
chimala njoo kangu nikupe hifadhi ya ukimbizi!

huduma zoote ntatoa! ila na wewe ucheze pati yako ifekitivule!
 
Last edited by a moderator:
inaonekana nautical miles alizotembea na wewe zimeshazidi!

hivyo anataka device mpya kabisa ya kuuzia!

jipange na wewe kutafuta wako..
 
we naye sasa unataka tupost nini, ndo maisha haya haya na chalenge zake, na ushauri unaupata kwa watu,yes yalishawatokea wengine mie sio wa kwanzal au ulitaka niende kwa mwenye kiti wa nyumba kumi ndo nimwambie

Eeh!! Mwenyekiti wa nyumba kumi anapatikana wapi Tanganyika hii?
 
Dada ukiona manyoya ujue keshaliwa. Tafakari songa mbele na mambo mengine.
 
bi dada umeachwa, kubali matokeo dada angu, akupendae hakufikishi apo,hakudhalilishi kiac icho , uo ni mthani tu wa kimaisha ukabili usikuyumbishe, usikubali kudhalilika kwake kiasi icho, na wew mpotezee mbalini.
pole kwa yote
 
Utawekaje picha ya mtu "asiye mkeo/mmeo" kwenye public? Akikupiga chini utaanzaje....mimi nashindwa kuelewa kwa kweli....

Vijana wa kisasa naombeni msaada..
 
Kwani siku hizi wanaume ni adimu kiivo?
Maana sioni unachong'ang'ania kudhalilishwa hapo.
 
Pole sana wahenga ukiona Moshi unafuka basi moto utawaka, ila kama hata kusoma hujui basi si umeona picha, jipange upya. Wknd njema.



Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom