Prof Janabi wa JF
Member
- Jul 7, 2023
- 28
- 36
Umufia kwenu wakuu,
Kwa muda mrefu nilikuwa na uhitaji wa kuoa, ila nilikuwa na ugumu wa kumpata mwanamke. Katika harakati za hapa na pale mwaka huu nikampata mtu nikasema hiki chuma nakiweka ndani. Ila sijamwambia kama nataka kumuweka ndani.
Hata hivyo nilikuwa na harakati za hapa na pale ambazo nyingi alikuwa anazijua. Na ghafla nikapata mishe ya kwenda ughaibuni kwa kipindi cha miaka miwili. Hii mishe inaruhusu mtu kwenda na wategemezi wake. Mimi nikaona niongee na mama mtu ili twende wote.
Aisee huyu mrembo kanichomolea, kasema hataki kwenda. Sasa nawaza nimuache, niende zangu nikachukua mrembo wa ughaibuni nirudi naye au nichukulie poa. Fikiria miaka miwili nikae mbali, lazima nitafanya mambo yangu, na yeye najua kuna mlevi atakuja kumkaza, aisee nimekwazika nawaza nimuacha kama kupata wa kuoa natamani nipate mwingine ili tuende wote, au kama vipi nikapeperushe bendera ughaibuni
Wadau mnaniambiaje. Natarajia kukaa ughaibuni kwa miaka miwili, na kiukweli sitamani mrembo wa ughaibuni ila naona kama nalazimika iwe hivyo.
Naombeni ushauri wenu. Kataa Ndoa huu uzi hauwahusu
Kwa muda mrefu nilikuwa na uhitaji wa kuoa, ila nilikuwa na ugumu wa kumpata mwanamke. Katika harakati za hapa na pale mwaka huu nikampata mtu nikasema hiki chuma nakiweka ndani. Ila sijamwambia kama nataka kumuweka ndani.
Hata hivyo nilikuwa na harakati za hapa na pale ambazo nyingi alikuwa anazijua. Na ghafla nikapata mishe ya kwenda ughaibuni kwa kipindi cha miaka miwili. Hii mishe inaruhusu mtu kwenda na wategemezi wake. Mimi nikaona niongee na mama mtu ili twende wote.
Aisee huyu mrembo kanichomolea, kasema hataki kwenda. Sasa nawaza nimuache, niende zangu nikachukua mrembo wa ughaibuni nirudi naye au nichukulie poa. Fikiria miaka miwili nikae mbali, lazima nitafanya mambo yangu, na yeye najua kuna mlevi atakuja kumkaza, aisee nimekwazika nawaza nimuacha kama kupata wa kuoa natamani nipate mwingine ili tuende wote, au kama vipi nikapeperushe bendera ughaibuni
Wadau mnaniambiaje. Natarajia kukaa ughaibuni kwa miaka miwili, na kiukweli sitamani mrembo wa ughaibuni ila naona kama nalazimika iwe hivyo.
Naombeni ushauri wenu. Kataa Ndoa huu uzi hauwahusu