Mpenzi wangu anataka ndoa haraka

Surya

JF-Expert Member
Jun 7, 2015
8,379
12,574
Mimi sio mwandishi mzuri lakini naomba niende moja kwa moja kwa mada husika. Dhumuni naomba ushauri kwenu wakuu nini cha kufanya.

Mimi nina umri wa miaka 24 (male) nimeanza kazi mwaka huu mwezi wa 7 katika zahanati (private sector). Then mwezi uliopita mwishoni ndio nilianza mahusiano rasmi na mpenzi wangu ambae nilionana nae miaka 8 iliyopita yeye kwa sasa ana miaka 21. Kazi anayofanya ni hotel magemenent, according to professional yake.

Tupo mikoa tofauti mimi kanda ya ziwa huku mashariki yeye yupo mikoa ya kaskazini. Alikuja nilipo first lakini sijamtambulisha bado kwa wazazi, lakini mimi nilipo kwenda kwao alinitambulisha kwa wazazi wake.

For sure she is sexually active. Just why anadai sana maisha ya peke yake hayataki, na pia ana heshima na ni mwanamke anayependa kusema kweli muda wote. Kwa upande wangu mimi ni mtu wa kiroho sana, nimekwisha acha kila tabia za kidunia ili tu niyafikie malengo yangu, sipo interested na tabia ya kubadili wanawake kwani mimi ni wa kiroho zaidi.

Kwa sasa tupo kwenye mzozo kuwa nitakamilisha lini process za kumuoa na tuishi nyumba moja na huku mimi hatua niliyofikia nina kitanda na godoro peke yake, na anataka endapo atakuwa mkoa ambao mimi nipo anataka nimtafutie na shuguli ambayo yeye atakuwa anafanya.

Kanipa majukumu hayo yote huku pia akidai mimi kukaa mbali na yeye ni tatizo kwani anakumbana na vishawishi vingi, nilijaribu kumueleza kuwa anipe miezi 6 ili nikamilishe maswala hayo yote lakini hataki na anadai kuwa miezi 6 ni mingi na malengo yetu itakuwa ngumu kutimia.

Naomba ushauri wenu nifanye nini na kwa sasa kazi za private zote maslahi ni madogo pande zote mbili, na pia familia zetu si familia tajiri, zote zinapambana na kusomesha watoto.

Kwa upande wangu mimi pia nampenda sana na sitaki kumpoteza, naweza kutafuta mwanamke mwingine lakini nahofia sitapata atakayenifaa zaidi yake kwani naelewa kiundani umuhimu wake na upekee wake. Pia najua yeye pia ananipenda, lakini naona swala la pesa linataka kuwa kikwazo kwetu, na yeye anashindwa kuwa mvumilivu.

Ushauri wenu wakuu, kama kuna lingine la kueleza kuhusu mimi na yeye nitaendelea kuelezea...
 
Peleka kishika uchumba kidogo na barua sio lazima utoe ila nyingi shida wajue binti yao amechumbiwa wazee ni waelewa hasa kweny masuala Kama hayo ya kheri waambie ukiwa umekamilika utakamilisha taratibu na bint yao akiwepo akuskie nadhan pia watamuelewesha


Pia mtambulishe kwenu basi hata ndugu wako wakaribu ikishindikana hata ndugu fake kumuhakikishia anaonekana ana wasiwasi muondoe wasiwasi
 
Fear is sickness!!
Peleka barua na kishika uchumba,ili akiondoka huko wazee wajue yuko wapi ,mahari na ndoa ije baadae ( mungu hapendi ).
Kuhusu hali ngumu.... ndio vizuri muanzie hali ngumu ,hii hutengeneza bond yenye nguvu sana kwa wapendanao.hata hapo mtakapofanikiwa ina jenga heshima sana.mchukue hivyo hivyo aje alale njaa kidogo ataelewa ulikuwa unamaanisha nini ulipokuwa unamwambia asubiri ujipange.
 
Kama ningekuwa mimi ndo wewe ningemwambia asubiri nijipange. Akishindwa nitamruhusu tu asombwe na hivyo vishawishi. Mwanamke anayeona miezi sita ni mingi kusubiri hanifai. Wengine wanaambiwa miaka na wanasubiri yeye tatizo ni nini!? Halafu, Je, nikishamuoa nikipata dharura ya kikazi au kiafya nisiwe naye itakuwaje!? We jua tu, kwamba hata ukimuoa huyo msichana ni dhaifu. Vishawishi haviishagi.
 
Huu uzi umenikumbusha mbali sana...
Kwa leo naomba niambatanishe tu picha
tapatalk_jpeg_1568211858235.jpeg
 
Nimekuelewa mkuu
Usichukulie maisha ya ndoa rahisi kihivyo!
Jipange kwanza, kitanda na godoro unaoa, baada ya miezi tisa mtoto, majukumu yanaongezeka!

Elewaneni tuu, avumilie ujipange!
 
Ni kweli mkuu, shida ni pale atakapokua anatoa lawama za ndani ya nyumba, nitajificha wap mm...
Fear is sickness!!
Peleka barua na kishika uchumba,ili akiondoka huko wazee wajue yuko wapi ,mahari na ndoa ije baadae ( mungu hapendi ).
Kuhusu hali ngumu.... ndio vizuri muanzie hali ngumu ,hii hutengeneza bond yenye nguvu sana kwa wapendanao.hata hapo mtakapofanikiwa ina jenga heshima sana.mchukue hivyo hivyo aje alale njaa kidogo ataelewa ulikuwa unamaanisha nini ulipokuwa unamwambia asubiri ujipange.
 
Nimekuelewa mkuu, nafanyia kazi wazo lako.
Kama ningekuwa mimi ndo wewe ningemwambia asubiri nijipange. Akishindwa nitamruhusu tu asombwe na hivyo vishawishi. Mwanamke anayeona miezi sita ni mingi kusubiri hanifai. Wengine wanaambiwa miaka na wanasubiri yeye tatizo ni nini!? Halafu, Je, nikishamuoa nikipata dharura ya kikazi au kiafya nisiwe naye itakuwaje!? We jua tu, kwamba hata ukimuoa huyo msichana ni dhaifu. Vishawishi haviishagi.
 
Mkuu Feysher, Sakayo
Naunga Mkono Hoja Zenu, Watu Wengi Sana Tunawaza Kulala Na Kuamka Tu Lakini Ndoa Ni Safari Ndefu Inayohitaji Kusomana, Kujiridhisha.
Mtakapokaa Pamoja Iwapo Hukujipanga Week Tayari Mimba
Majukumu Mapya Yanaingia.

Unatoka Family Ya Kawaida Maana Yake Majukumu Yako Ni Wewe Mwenyewe.
Tulia Angalau Uwe Na Akiba Maisha Yanabadilika Leo Una Kazi, Baadaye Unaweza Usiwe Nayo Jipe Muda
 
Kwanza, hongera kijana kwa kujielewa!

Pili, ninachoweza kukushauri tu.... Utafute nafasi, uende kwa huyo mkwe wangu, then muongee physically. Hapo wewe mueleweshe tu kwa upendo, juu ya nini mnatakiwa mkifanye hivi sasa kwenye maisha yenu, so as mfikie malengo hayo ya kuingia kwenye taasisi.

Ila in case ukiona bado akuelewi, hapo no way just fikieni tu maamuzi ya kuwa pamoja. As long as mmeridhiana and at the same time umebarikiwa kupata hiko kidogo....no mbaya mpaka hapo, take risks kijana!

And binafsi sioni kama mwenzio, anaweza kuwa headache kwako...bali ninachokiona ni utapata blesses from her. Tena nawe, ujitaidi tu usimuache awe mama wa nyumbani.....just fight for her destination.


Kila la kheri kijana.
 
Back
Top Bottom