Mimi sio mwandishi mzuri lakini naomba niende moja kwa moja kwa mada husika, dhumuni, naomba ushauri kwenu wakuu nin cha kufanya.
Mim nina umri wa miaka 24 (male) nimeanza kazi mwaka huu mwezi wa 7 katika zahanati (private sector).
Then mwezi uliopita mwishoni ndio nilianza mahusiano rasmi na mpenz wangu ambae nilionana nae miaka 8 iliyopita yeye kwa sasa anamiaka 21. Kazi anayofanya ni hotel magemenent, according to professional yake.
Tupo mikoa tofauti mm kanda ya ziwa huku mashariki, yeye yupo mikoa ya kaskazini.
Alikuja nilipo first lakini sijamtambulisha bado kwa wazazi, lakini mm nilipo kwenda kwao alinitambulisha kwa wazazi wake.
Fo sure she is sexual activite. Just why anadai sana maisha ya peke yake hayataki, na pia anaheshima nani mwanamke anaependa kusema kweli muda wote.
Kwa upande wangu mm ni mtu wa kiroho sana, nimekwisha acha kila tabia za kidunia ili tu niyafikie malengo yangu, sipo interested na tabia ya kubadili wanawake kwani mm niwa kiroho zaidi.
Kwa sasa tupo kwenye mzozo kuwa nitakamirisha lini process za kumuowa, na tuishi nyumba moja na huku mm hatua nilio fikia nina kitanda na godolo peke yake, na anataka endapo atakua mkoa ambao mm nipo anataka nimtafutie na shuguli ambayo yeye atakua anafanya.
Kanipa majukumu hayo yote huku pia akidai mm kukaa mbali na yeye ni tatizo kwani anakumbana na vishawishi vingi, nilijarbu kumueleza kuwa anipe miezi 6 ili nikamilishe maswala hayo yote lakini hataki na anadai kuwa miezi 6 ni mingi na malengo yetu itakua ngumu kutimia.
Naomba ushauri wenu nifanye nn na kwa sasa kazi za private zote masilahi ni madogo pande zote mbili, na pia familia zetu si familia tajiri, zote zinapambana na kusomesha watoto.
Kwa upande wangu mm pia nampenda san na sitaki kumpoteza, naweza kutafuta mwanamke mwingine lakini nahofia sita pata atakae nifaa zaidi yake kwan naelewa kiundani umuhimu wake na upekee wake.
Pia najua yeye pia ananipenda, lakini naona swala la pesa linataka kuwa kikwazo kwetu, na yeye anashindwa kuwa mvumilivu.
Ushauri wenu wakuu, kama kuna lingine la kueleza kuhusu mm na yeye nitaendelea kuelezea...