Mpenzi wangu anatabia ya kukasirika bila sababu

Mpenzi wangu anatabia ya kukasirika bila sababu

Habari zenu jamani,

Nina mpenzi wangu sijui ananifanyia makusudi au ni tatizo lake tu, yani anaweza kunikasirikia hata wiki nzima kosa silijui, hanisemeshi nikimtumia meseji hajibu, simu hapokei, anaweza akawa active kwa facebook au online kwa whatsup lakini ukimtumia meseji hajibu.

Akiamua anakutafuta tena kwa mapenzi motomoto, nikimuudhi pia hasemi ananuna tuu hivyo hvyo ila siku akikaa sawa ndo anakwambia ulimuudhi kitu fulani kinachonitatizo ni huko kununna bila sababu mnaweza mkaongea vizuri usiku, asubuhi akawa amekasirika.

Hebu mnieleweshe nikwamba hanitaki nijiongeze au maana matumizi nampa ya kutosha kila wiki wenye matusi piteni kushoto kwa hii posti.

Nawasilisha
KISILANI HUYO! MWOMBEE
 
  • Thanks
Reactions: THT
Mvumilie mapenzi ni kuvumiliana hata akinuna mwaka we vumilia
 
  • Thanks
Reactions: THT
mapenzi yake kama homa za vipindi au
mapenzi ya mwendokasi au
mapenzi ya mwisho wa mwezi mapenzi yananoga kuanzia tarehe 25 hadi tarehe 5 hebu chunguza vizuri muda gani mapenzi yanamea maana mimea humea wakati wa masika
 
Siku zake za kukasirika na wewe ukasirike
 
  • Thanks
Reactions: THT
danger zone hiyo ni kwa kipindi tuu atakaa sawa..usijali...pia kuwa muwazi kwake kwa kumwambia hupendezwi na hiyo tabia yake ya kuzira..ajirekebishe ...lakini kama inatokea kwa mwezi mara moja ..usiogope ndo tulivyo tukiwa hatarini au tukikaribia..hebu chunguza ni kipindi gani anakuwa hivo...
 
Anachanalo kwa nn uwaze kisa mwamamke ivi awa wanawake wana nini lkn jamani muache jifuze kuacha mkuu
 
  • Thanks
Reactions: THT
Habari zenu jamani,

Nina mpenzi wangu sijui ananifanyia makusudi au ni tatizo lake tu, yani anaweza kunikasirikia hata wiki nzima kosa silijui, hanisemeshi nikimtumia meseji hajibu, simu hapokei, anaweza akawa active kwa facebook au online kwa whatsup lakini ukimtumia meseji hajibu.

Akiamua anakutafuta tena kwa mapenzi motomoto, nikimuudhi pia hasemi ananuna tuu hivyo hvyo ila siku akikaa sawa ndo anakwambia ulimuudhi kitu fulani kinachonitatizo ni huko kununna bila sababu mnaweza mkaongea vizuri usiku, asubuhi akawa amekasirika.

Hebu mnieleweshe nikwamba hanitaki nijiongeze au maana matumizi nampa ya kutosha kila wiki wenye matusi piteni kushoto kwa hii posti.

Nawasilisha


Wewe Ni wa matumizi tu, wapo wengine
 
  • Thanks
Reactions: THT
Piga chini mzoga huo,hata me nilikua na jitu la hvyo,yani jitu likikukosea ukalikosoa kidogo linanuna mwezi mzima,kwanza jitu la kununa hovyo litakuletea gundu maishan tu.
 
Back
Top Bottom