Mpenzi wa Zamani Anapokuchangamkia

platozoom

JF-Expert Member
Jan 24, 2012
9,366
11,156
Ndio, baada ya kutafakari sana mmeamua kuvunja mahusiano, kwamba hakuna mapenzi kati yenu na tofauti zenu ni kubwa. Mmoja kwenye mahusiano (Tumwite X) anajiona yeye ndiye yeye........Kifupi ujeuri mwingi na wakati mwingine hapokei hata simu anapopigiwa na mpenzi wake (Tumwite B).

Hayo yakapita majeraha yakapona na maisha yakaendelea. Katika pitapita za hapa na pale mjini mnagongana na hata kusalimiana, kimsingi hamko-close hata kirafiki. Mhanga wa mahusiano (B) haonyeshi kujali sana wala kuulizia yaliyopita, ni salamu na mwendo mdundo............

X anashangaa na anajaribu kuwauliza marafiki zake wawili "Inakuwaje B siku hizi yuko kimya hivi, sijategemea kama hatokuwa ananipigia simu hata baada ya kuachana"..........marafiki zake hata wao wanashangaa hawakutegemea yule mtu aliyekufa kaoza kwa rafiki yao X atakuwa hivyo!!

Na habari zinavuja na kumfikia B, naye anazisikiliza na kuziweka kando. Kifupi hana muda huo!...........Ingawa kadri siku zinavyokwenda X anaweweseka na Vi-SMS vya hapa na pale, lakini hajui afanye aseme nini na vipi. Taswira inayoonekana ni kuwa naye amepigika moyo, ingawa fursa kutoka kwa B haielekei kama itapatikana!

Mkasa wa kweli ambao bado uko moto...........Mimi mbea nitawafahamisha hiyo safari ya X na B kama itakoma kabisa.
 
Kweli mbea haulizwi, nimekosa hata cha kuuliza nabaki kusubiria updates tu!

Mzima lkn?

Mie mzima wa afya njema ahlan wasahlan.......weye je? Ila nitajaribu kuwa makini si unajua mwanaume kusutwa ni laana.
 
umbea kazi, ila ungewapa majina badala ya X na B, labda wape Havintishi na Mayunga.

Au Kashinde na Bageni? Tatizo nikifikiria kuweka majina huwa najikuta naweka ya watu wanaonizunguka e.g. majirani, na ndugu!
 
lol, hii nimeipenda manake yamewahi kunikuta hayo.
Kweli maisha safari ndefu.

Na ulikuwa side ya B au X.........Unajua hii ishu huwa inanishangaza sana namna ilivyopinduka juu chini. Siku zote hata kama humpendi mtu usimdharau ..............kama yanayomkuta X
 
Uzuri wa kitu huwezi kuujua kama unacho kwapani na kimejaa tele...Ila kikikuponyoka tu, ndo unagundua kuwa umepoteza Diamond.

Na wakati mwingine inakuwa too late, huwezi kukipata tena.

Hadithi hii inatufundisha kukumbuka kuwa hata kama tumeshiba, tusitupe sahani za kulia!

Babu DC!!
 
Back
Top Bottom