Mpeni muda Rais Samia Suluhu aipange Serikali yake

Mpeni muda Rais Samia Suluhu aipange Serikali yake

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
34,104
Reaction score
43,357
Sijui kwanini inaonekana kuna msukumo mkubwa kwa Rais Samia Hassan kufanya hili au kufanya like. Inawezekana katika kuonesha uhuru wake kutoka kivuli cha Magufuli anajaribu kuridhisha makundi mengi. Lengo lake la kuendeleza kutekeleza ajenda ya Magufuli-Samia2020-2025 yeye ndio anajukumu la kuipanga Serikali kwa ajili ya ufanisi, weledi, na matokeo chanya (positive outcome).

Tumpe muda wa kujipanga, na kufanya makosa, na kuyasahihisha. Ikumbukwe hata Katibu Mkuu Kiongozi ni Mpya (ndiye anahusika Sana na teuzi zote za Rais). Shida ni kuwa inawezekana CCM (kama taasisi au vigogo fulani) wanataka watu fulani wakumbukwe. Hili si jipya...la maana isijekuwa wanajaribu kumdhoofisha Rais....hili halikubaliki.
 
Emb tulia wewe mzee. Kwa hiyo hata yule dogo wa Yohana university tungemuacha tuu kwakuwa tunatakiwa kumpa muda? Nikueleze tu kuwa ambaye "Sipangiwi" ameshaondoka zake. Kilichobaki ni wewe kubadili mtindo wa ngoma la sivyo sonona itakuondoa.

Na Slaa anarudi keshokutwa bongo.
 
Mzee chutama ustiri hata robo ya heshima uliyobakia nayo mbele ya wapuuzi wenzio.

Ulikua mpiga mbeta kwa mambo ya kipuuzi kwa Magufuli usimtake Samia awe kama huyo mwendazake.

Tulia zama zimebadilika huo u magufuli-Samia haupo naona unajilazimisha sana hii nchi sio ya kifalme au kifamilia kwamba Samia karithi hizo elements zenu za kishenzi.
 
Raisi hatakiwi kukubali presha kutoka kwa Mtu yoyote. Anatakiwa kusimama kile anaamini, Kama anakubali kuletewaletewa majina ya mfukoni au presha basi atapata Sana shida.
Pia ajipe muda, sioni haraka ya kuteua
Jiwe alijifanya mjuaji changamoto ikapita naye hata mabilioni aliyojikusanyia hakuyala.

Samia ni muungwana na muungwana tabia yake ni kusikiliza ushauri asije akakomaa kama mpapai mbeleya upepo
 
Mkuu, wengi wanasukumwa na chuki!

Utakuta mtu anaropoka tu eti mbona yule hajamtoa wakati aliteuliwa na jiwe! Yani kwa akili zao wanataka Samia ateue kulingana na fikra zao hasa chuki!
 
Emb tulia wewe mzee. Kwa hiyo hata yule dogo wa Yohana university tungemuacha tuu kwakuwa tunatakiwa kumpa muda? Nikueleze tu kuwa ambaye "Sipangiwi" ameshaondoka zake. Kilichobaki ni wewe kubadili mtindo wa ngoma la sivyo sonona itakuondoa.

Na Slaa anarudi keshokutwa bongo.
Wewe ndio maana mods walikupiga ban!

Kwahiyo unataka Samia ateue kwa matakwa yako?
 
Kuna watu wanajifanya kumpangia mama kila kitu kila analofanya kwao hakuna jema. Mama piga kazi kwa sasa tupo nawe na ndio unaanza baada ya muda ukizingua tunapita na wewe. Ila kwa sasa panga timu yako
 
Mkuu, wengi wanasukumwa na chuki!

Utakuta mtu anaropoka tu eti mbona yule hajamtoa wakati aliteuliwa na jiwe! Yani kwa akili zao wanataka Samia ateue kulingana na fikra zao hasa chuki!
Kama Kigogo anatokwa na povu mama akipita pembeni ya mawazo yake. Sijui nchi iendeshwe kwa mawazo yake, Kigogo is nothing but someone whose intention ni kujulikana anajua kila kitu.
 
Mzee chutama ustiri hata robo ya heshima uliyobakia nayo mbele ya wapuuzi wenzio.

Ulikua mpiga mbeta kwa mambo ya kipuuzi kwa Magufuli usimtake Samia awe kama huyo mwendazake.

Tulia zama zimebadilika huo u magufuli-Samia haupo naona unajilazimisha sana hii nchi sio ya kifalme au kifamilia kwamba Samia karithi hizo elements zenu za kishenzi.
Mbona wewe ndio mshezi sasa?

Ujinga wenu ni kutaka kumwambia Samia toa fulani pale na weka fulani pale. Huo ujinga mtampa rais wenu yule wa ubelgiji
 
Kama Kigogo anatokwa na povu mama akipita pembeni ya mawazo yake. Sijui nchi iendeshwe kwa mawazo yake, Kigogo is nothing but someone whose intention ni kujulikana anajua kila kitu.
Na bahati nzuri wenye akili wameshampuuza na kadri siku zinavyozidi kwenda anazidi kuwa mjinga zaidi.
 
Back
Top Bottom