Mpango wa kumtimua UDASA Dr. Kitila Mkumbo wasukwa

Magamba wanataka kufanya taasisi za umma kama NGO zao. Dalili za kifo ndio hizo.
 
Kama amekuwa dean hawezi tena kuwa kiongozi udasa ila haiondoi ukweli kwamba wanampiga vita
 
I trust the profesors na wahadhiri wengine kuwa hawatomfanyia hiko wanachofikiri hao wavivu wa kufikiri.Dr.Kitila hata kama alivyosema juzi kuwa wao hawagombei bali majina hupendekezwa na wajumbe na mwenye sifa hupewa nafasi ya kuongoza kwa kuchaguliwa kwa kura.Naamini atapita tena kwa kishindo na watashangaa!Aliewaambia kuwa wao wanahaki miliki ya uongozi na rasilimali za UDSM nani?waache upuuzi wao wa kijinga msomi mkubwa anakuwa na majungu majungu then anataka aheshimike how?
Godbess lema amevuliwa ubunge halafu akawa maarufu zaidi nahisi Kitila mkumbo huenda ikawa the same maana jana lunch time niko makaburini bar(rose garden ya Arusha) alivyoingia nikaona watu wote wameweka tonge chini kumlaki mheshimiwa lema
 
Hakuna shaka kwamba kuna watu wanakerwa sana na makongamano ya Nkrumah. Hawa ni wale wanaoamini kwamba ili uweze kuongoza vizuri lazima uwafiche watu taarifa na uelewa. Wanaamini katika kuongoza wajinga, na bahati mbaya makongamano ya Nkrumah yamekuwa yakiamsha watu wengi sana nchini kwa sababu yanarushwa moja kwa moja na ITV, ambaye inaangaliwa sehemu kubwa ya Tanzania. Wengi walishanivaa mimi mwenyewe mara kadhaa na kunilaumu kwa kuandaa makongamano haya na kudai kuwa nayatumia kisiasa kuinufaisha CHADEMA. Hata hivyo, wana UDASA walio wengi wanajivunia sana makongamano yanayofanyika kwani ni sehemu muhimu ya kutoa mchango wetu moja kwa moja kwa jamii ya watanzania.

Pamoja na baadhi ya watu kukerwa na makongamano yetu, bado hawana uwezo wa kutuchaguliwa nani awe kiongozi wa UDASA. Wanachama wa UDASA wapo makini mno kiasi kwamba ni vigumu kujipenyeza kijanjakijanja katika ngazi ya uongozi kama ilivyo katika siasa za kawaida za Tanzania.

Ukweli ni kwamba muda wetu wa uongozi ulikuwa umeisha na jana tumefanya uchaguzi kama nilivyotangaza katika kongamano la Nkrumah. Mimi nilikuwa sio miongoni mwa waliopigiwa kura baada ya kuwaomba wenzangu wanipumzishe kufuatia kuteuliwa kuwa mkuu wa kitivo cha elimu katika chuo chetu cha DUCE ili kuepuka mgongano wa maslahi na ukweli kwamba sasa hivi nipo mbali na makao makuu ya UDASA, yaani Mwalimu JK Nyerere Mlimani Campus. Nashukuru wenzangu walinielewa na kuniruhusu nisiendelee na uongozi wa UDASA.

Jana tulichamchagua Dkt Francis Michael kuwa Mwenyekiti mpya wa UDASA na nafasi ya makamu imechukuliwa na Dkt Vicensia Shule. Kwa wale wanaofuatilia kwa karibu harakati za CKD watakumbuka kwamba Dkt Francis Michael alikuwa Makamu wangu mimi nilipokuwa Rais wa Serikali ya Wanafunzi CKD (DARUSO) 1998/1999. Ni mtu makini kabisa na naamini ataisogeza UDASA mbele zaidi.

Mimi kwa sasa naelekeza nguvu zangu katika kuchangia kuona kuwa chuo chetu cha DUCE kinakuwa miongoni mwa vyuo bora kabisa katika bara letu katika kutoa walimu na kuchangia kikamilifu katika kuboresha elimu hapa nchini kupitia ufundishaji, tafiti na mijadala ya kina juu ya maswala ya elimu nchini mwetu na katika bara la Afrika kwa ujumla.
 
Dr nafurahi walipokupeleka. huku nako makanjanja kibao. hivi karibuni utaelewa kwanini wanajiita watoto wamama wa kambo. USISAHAU KUWAAMSHA VIONGOZI WA UDASA- DUCE. many more are behind and supporting you.All the best mkuu.
 
Kwa huo mtitiriko na kwa tabia huyo kiongozi mwandamizi ofisi ya VC ni PROF. RWEKIZA MUKANDALA na huyo muhadhiri kitivo cha sayansi ya siasa ni DR. BENSON BANA.
Hawa ndio miongoni mwa makada wakubwa wa CCM pale UDSM. Pia kuna mmoja wao yupo kitivo cha sheria PALAMAGAMBA KABUDIA kwa sasa yuko na tume ya kukusanya maoni ya katiba na mwisho ni DR. Asharose Migiro ambaye amerudi siku za karibuni.
 
Afadhali umekuja haraka kututhibitishia ukweli wa habari hizi. Pamoja na kwamba wengi hatumfahamu vizuri Dr Michael walau kupitia ushuhuda wako tunaamini UDASA itaendelea kutoa changamoto kwa CDK na serikali kiujumla. Aidha binafsi namfahamu Dr Vicensia Shule...Naamini UDASA ipo kwenye salama
 
Kama hizi habari ni za kweli na ambavyo imezoeleka kama alivyofanyiwa Prof Baregu sintashangaa. Basi UDSM iitwe university of ccm
 
Hakuna shaka kwamba kuna watu wanakerwa sana na makongamano ya Nkrumah. Hawa ni wale wanaoamini kwamba ili uweze kuongoza vizuri lazima uwafiche watu taarifa na uelewa. Wanaamini katika kuongoza wajinga, na bahati mbaya makongamano ya Nkrumah yamekuwa yakiamsha watu wengi sana nchini kwa sababu yanarushwa moja kwa moja na ITV, ambaye inaangaliwa sehemu kubwa ya Tanzania. Wengi walishanivaa mimi mwenyewe mara kadhaa na kunilaumu kwa kuandaa makongamano haya na kudai kuwa nayatumia kisiasa kuinufaisha CHADEMA. Hata hivyo, wana UDASA walio wengi wanajivunia sana makongamano yanayofanyika kwani ni sehemu muhimu ya kutoa mchango wetu moja kwa moja kwa jamii ya watanzania.

Pamoja na baadhi ya watu kukerwa na makongamano yetu, bado hawana uwezo wa kutuchaguliwa nani awe kiongozi wa UDASA. Wanachama wa UDASA wapo makini mno kiasi kwamba ni vigumu kujipenyeza kijanjakijanja katika ngazi ya uongozi kama ilivyo katika siasa za kawaida za Tanzania.

Ukweli ni kwamba muda wetu wa uongozi ulikuwa umeisha na jana tumefanya uchaguzi kama nilivyotangaza katika kongamano la Nkrumah. Mimi nilikuwa sio miongoni mwa waliopigiwa kura baada ya kuwaomba wenzangu wanipumzishe kufuatia kuteuliwa kuwa mkuu wa kitivo cha elimu katika chuo chetu cha DUCE ili kuepuka mgongano wa maslahi na ukweli kwamba sasa hivi nipo mbali na makao makuu ya UDASA, yaani Mwalimu JK Nyerere Mlimani Campus. Nashukuru wenzangu walinielewa na kuniruhusu nisiendelee na uongozi wa UDASA.

Jana tulichamchagua Dkt Francis Michael kuwa Mwenyekiti mpya wa UDASA na nafasi ya makamu imechukuliwa na Dkt Vicensia Shule. Kwa wale wanaofuatilia kwa karibu harakati za CKD watakumbuka kwamba Dkt Francis Michael alikuwa Makamu wangu mimi nilipokuwa Rais wa Serikali ya Wanafunzi CKD (DARUSO) 1998/1999. Ni mtu makini kabisa na naamini ataisogeza UDASA mbele zaidi.

Mimi kwa sasa naelekeza nguvu zangu katika kuchangia kuona kuwa chuo chetu cha DUCE kinakuwa miongoni mwa vyuo bora kabisa katika bara letu katika kutoa walimu na kuchangia kikamilifu katika kuboresha elimu hapa nchini kupitia ufundishaji, tafiti na mijadala ya kina juu ya maswala ya elimu nchini mwetu na katika bara la Afrika kwa ujumla.

umesomeka vizuri mkuu. Dk Francis Michael namfahamu vizuri sana. Amekuwa akihudhuria makongamano mbalimbali yanayofanyika Nkrumah japo hakuwa mchangiaji sana. Amenifundisha course inaitwa Human Resource Management(HR 201). He is objective japo anahasira akichukizwa hata kwak2 kidogo. Dk Kitila Mkumbo, naomba ubadilishe Duce. Zile lecture theatre mpya hasa ule ukumbi wa juu utumieni kama Nkurumah ndogo. Duce pana kumbi nzuri ila hakuna wa kuimprovise resources zilizopo. Andaa makongamano kwa kualika watoa mada mbalimbali na kuitangaza vyakutosha, ipo siku Duce itafahamika vizuri na watu watajivunia kama product toka Duce. Mtumie vizuri Prof Mfinanga kwani Prof Misana alikuwa mbanaji sana! Shirikiana na Prof Magimbi kuibadilisha Duce!
 
umesomeka vizuri mkuu. Dk Francis Michael namfahamu vizuri sana. Amekuwa akihudhuria makongamano mbalimbali yanayofanyika Nkrumah japo hakuwa mchangiaji sana. Amenifundisha course inaitwa Human Resource Management(HR 201). He is objective japo anahasira akichukizwa hata kwak2 kidogo....................

Nakupongeza Dr. Kitila kwa kuja jamvini kujib na kutoa ufafanuzi na pia niwapongeze wanaUDASA kwa ufanya uchaguzi wao. Huwa sipendi nami kuwaongelea watu lakin kwa ufupi tu kuongezea aliyoyasema ndugu "Malolella" juu ya Dr. F.Michael. Dr. huyu pia huwa anajihusisha na siasa za Mkoa wa Kigoma kwa ukamilifu ila ni mtu ambaye hajihamin sana. Nasema hvi kwa mantiki kuwa wakaz wa jimbo la Kigoma Mjin wamekuwa wakimfuata ili aweze kugombea ubunge hussusan wazee wa CCM anakuwa sitaki nataka lakin hata CDM waliwahi kumshawishi akagoma akawa mtiifu kwa CCM. Huyu bwana bado ana kadi ya CCM hajawahi kuirudisha. Kwa watu anajulikana kama mpambanaji lakin anakuwa mpambanaji pale tu anapohis ana masilahi. Amekuwa kiongozi wa RAAWU kwa muda mrefu tu akitetea maslahi ya wafanyakazi wa Chuo na amekuwa akijitahid kupambana na uongozi wa Chuo katika kutetea licha ya kuwa ni kada wa Chama tawala. Naomba tu nitoe rai na ushauri kwake kuwa amepewa cheo kikubwa sana kwenye chuo kikongwe hapa nchini.

Kwanza hadhi ya wasomi au mchango wa wasomi umeshuka ktk maendeleo ya nchi. Zamani Chuo kikuu cha DSM kilikuwa kinatoa dira na mwelekeo mambo yaendeje hvi leo wasomi hao wamebaki kutetea tu mishahara yao wameacha maslahi ya nchi pembeni. Kuna mambo mengi yanayoendelea nchini ambayo ilibidi waonekane mstari wa mbele kupinga hawaonekani wameiacha nchi hii ikiteketezwa na wanasiasa. Nao mwisho wa siku wameanza kukimbilia siasa. Ni wakati mwafaka Dr. Kitila na wenzako wa UDASA mkatathimin mchango wenu katika ustawi wa taifa hili ili kuweka historia sawa maana mnayo nafasi hamna haja ya kukaa kimya wakati nchi hii inateketea msiruhusu wanasiasa wawagawanye na kuwatawala. Naomba Dr. Kitila uchukue ujumbe huu DUCE uwaamshe vijana waache kuwa wanafik penye ukweli wasimame imara na pia mshauri Dr. Francis watu wana matumaini naye ila kuwa na kadi ya Chama kusiwe kikwazo kupigania maslahi ya TAIFA ili wananchi wa kawaida tuweze kuona mchango wenu usiishie kwenye majarida na vichapisho tu.
 
Namtakia kila la kheri Dr. Kitila kwa kuwa namkubali sana tu. Hii habari ina walakini ni kama imetungwa vile, ila ili kuwa katika upande salama ni bora kuchukulia kuwa ni kweli ili kujizatiti.

Kwa nini nimesema imetungwa, na aliyeleta bandiko hili amejisahau..

Katika maongezi ya watu wawili, hawawezi kuwa wanatajana majina kila wakati, watatajana status au vyeo. Mtu ataendelea kumtaja mwenzie Dr. Dr.. Dr..... au Prof.... Prof...... Pro... ila anapotoa hoja yake.

Kama Professor Mkandara ni Rafiki yako, Ukikutana nae utamsalimia 'mfano' Shikamoo Professor. Na sio Shikamoo Professor Luhanga.

Nauchukia uongo sana mimi.
 
Back
Top Bottom