Huyu mpangaji wangu nimemvumilia sana, ni mwaka wa pili sasa anasema mambo yake hayako vizuri, nikienda kumdai kodi yeye na mkewe wanalia sana kwamba nizidi kuwavumilia.
Kuna binti yao yupo form four huyo naye anajiunga nao kunililia anasema baba tusaidie tu babaa tutakulipa huku kanipigia magoti kushika viatu vyangu na suruali.
Imefikia hatua mke wa jamaa ananiandikia sms kuniomba niendelee niwavumilia, hata binti naye anaandikia sms kunipa shikamoo na kuniambia baba naomba tuvumilie tu maana baba yangu hana hela kabisa hata mimi nasoma kwa shida sana babangu.
Anapofanyia kazi huyo jamaa napajua na anapofanyia kazi huyo mkewe napajua ila siwezi kuwaambia sababu ya kulinda maudhui ya hapa JF.
Nipeni ushauri ila mimi naona ni kuwatimua tu tarehe 30th November hii, kifupi kila mtu atabeba sanduku lake mwenyewe na hapa mjini kila mtu kaja kivyake.
Kuna binti yao yupo form four huyo naye anajiunga nao kunililia anasema baba tusaidie tu babaa tutakulipa huku kanipigia magoti kushika viatu vyangu na suruali.
Imefikia hatua mke wa jamaa ananiandikia sms kuniomba niendelee niwavumilia, hata binti naye anaandikia sms kunipa shikamoo na kuniambia baba naomba tuvumilie tu maana baba yangu hana hela kabisa hata mimi nasoma kwa shida sana babangu.
Anapofanyia kazi huyo jamaa napajua na anapofanyia kazi huyo mkewe napajua ila siwezi kuwaambia sababu ya kulinda maudhui ya hapa JF.
Nipeni ushauri ila mimi naona ni kuwatimua tu tarehe 30th November hii, kifupi kila mtu atabeba sanduku lake mwenyewe na hapa mjini kila mtu kaja kivyake.